Mwongozo juu matumizi ya "Loud Speakers" kwenye Nyumba za Ibada katikati Makazi ya raia

Kimsingi lazima tuwe wakweli jamani, tunaheshimu sana imani za watu ila haya maspika yanayotumiwa ktk makanisa yanayoota kama uyoga ktk makazi ya watu, ni KERO kubwa sana kwa watu. Utakuta ibada inafanyika kuanzia asbh mpaka jioni ni makelele mpaka vichwa vinauma mnaokaa karibu hapo. wakati mwingine unalazimika kuondoka nyumbani kwako kupisha hiyo mitetemo ya maspika mpaka wamalize ndo urudi. sasa ya nini kutesana hivi???

Kuna haja ya kutungwa sheria juu ya mambo haya, vinginevyo tutaendelea kuumizana bila sababu za msingi. Na mabar ambayo yapo karibu na makazi hali kadhalika ambayo music unapigwa utadhani hall la music. Kama vp haya majumba yao wawe wanaweka sound proof ili kutokuwaathiri wenzao
 
Mtaani kwetu wezi wanatumia fursa hiyo kufanya yao a kutogundulika kirahici kutokana na makelele ya bar na makanisan.

Ni vema kuwe na mikesha maalumu inayotambulika kitaifa na ulinzi uimarishwe na pia sheria ya kuanzisha makanisa ipitiwe upya coz kila mtu anataka kuanzisha ni wakati wa kuwaondolea misamaha ya kodi
Izi baar ziwe na kikiomo watu wafanye kazi ni aibu kwa taifa kukutana na walevi asubuh.
Ni hayo tu Mh.

Hii ni aina mojawapo ya uchafuzi wa mazingira: Sound pollution.
 
daaa kweli shetani na watu wake hivi kweli mkuu sauti za nyimbo za dini au neno LA mwenyezi mungu na mafundisho ya dini wasema nikelele?? na kero kwako?? aisee pole sana kuna mambo mengi. sana kuna madanguro madada poa wametapakaaa wanafanya machafuko na machukizo KWA mwenyezi mungu hilo hamlioni ila chukizo kwako ni neno LA mungu tuu??.

makanisa na misikiti iongezwe ili kupunguza madhambi

Ww unadhani watu wote tunaamini?? Point sio neno la mungu topic ni kelele za nyumba hizo za kuabudu yani watu washindwe kulala kisa ww unamsifu bwana yesu au mtume!? Fungeni soundproof. hamuwezi acheni. mnaboa sana nyie wafia dini
 
Sizan kama kuna iman inamtaka mtu afungulie maspika usiku kucha, n ratiba zao tu wanaeza shauriwa kuzibadili, kuna madhehebu wakikesha taifa linajua na ulinzi unaimarishwa
n vema na haya madogo madogo kila kona wajitahid kupanga cku maalum..point yangu ni usalama na utulivu kwa watu wengine
Okay hilo ni suala la watendaji wa mitaa kukaa na watu wao na kushauriana & sio la Rais wa JMT.
 
Mmh,ngoja wengine wachangie kwanza!

mkuu ngoja namie nitie neno.
yanayofanywa hasa kwenye nyumba za ibada naziita ni fujo na pia ni ubakaji wa imani kwa sababu umeisha waita waumini wako kwa loud speaker wamekuja upo nao ndani tayari sasa kwanini usizime hizo speaker au kupunguza sauti ili msikilizane nyinyi tu humo ndani na unajua hii nchi sio ya dini moja kila mtu anadini yake sasa badala ya kuwahubiria waumini wako ulio nao ndani unataka imani yako wewe ndiyo utuhubirie tuisikie mtaa mzima sasa kwa kutuhubiria kitu ambacho sisi hatukitaki ni sawa na kutubaka kiimani
 
Wana JF,

Habari za leo hii,

Kwa muda sasa nimekuwa nikijiuliza juu ya suala hili la matumizi ya loud speakers kwenye nyumba za ibada (Makanisa na Misikiti) yaliyoko katikati ya makazi ya watu. Hivi kuna sheria yoyote au mwongozo unaolekekeza juu ya hili? I beg to remain neutral kwa hili.

Utakuta mtu kajinunulia residentian plot anaweka nguzo nne, turubai juu annazisha kanisa (hapa amebadilisha matumizi), halafu anakesha mwenyewe na familia yake huku akiwa amefungulia spika hadi mwisho usiku kucha! au Msikiti uko katikati ya makazi ya watu asubuhi na mapema baada kuwaamsha watu kwa adhana, wanaendelea kuomba kwenye loud speakers bika kujali kuwa wamezungukwa na waumuni wa imani nyingine ambao hawahitaji kuamshwa kwa sauti za maombi/sala zinazofanyika makanisani au misikitini!

Kwa kweli najiuliza sana hivi hakuna mwongozo juu ya hilli katika nchi yetu yenye utulivu wa kiimani?

Naomba tujadili hili ila kama kuna mwongozo basi tupate
Umesahau Vigodoro.Au havihusiki?
 
Back
Top Bottom