tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
Mgombea wa urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema serikali itaendelea kutekeleza mikakati ya kuinua sekta ya kilimo kwa kujenga skimu mpya za umwagiliaji, kuongeza upatikanaji wa zana za kisasa, na kujenga maghala ya kuhifadhia mazao ili kudhibiti bei ya mchele nchini.
Akizungumza na wakulima wa mpunga, mwani na wavuvi katika uwanja wa Marumbi, wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, Dk. Mwinyi amesema serikali inatambua changamoto zinazowakabili wakulima wa mpunga, ikiwemo uhaba wa zana za kilimo na pembejeo, na kwamba hatua madhubuti zimeanza kuchukuliwa ili kuboresha sekta hiyo.
“Serikali inaendelea kuhakikisha tunapanua skimu za umwagiliaji ili kuongeza uzalishaji wa mpunga. Tunajua tunahitaji zana za kisasa, na ahadi yetu ni kuleta matrekta makubwa, ‘powertillers’, pamoja na mashine za kuvunia. Vifaa hivyo vitasaidia kuongeza tija na kupunguza gharama za uzalishaji,” amesema Dk. Mwinyi.
Soma pia: Dkt. Mwinyi: Miaka 5 ijayo tutajenga soko kubwa Kinyasini
Akizungumza na wakulima wa mpunga, mwani na wavuvi katika uwanja wa Marumbi, wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, Dk. Mwinyi amesema serikali inatambua changamoto zinazowakabili wakulima wa mpunga, ikiwemo uhaba wa zana za kilimo na pembejeo, na kwamba hatua madhubuti zimeanza kuchukuliwa ili kuboresha sekta hiyo.
“Serikali inaendelea kuhakikisha tunapanua skimu za umwagiliaji ili kuongeza uzalishaji wa mpunga. Tunajua tunahitaji zana za kisasa, na ahadi yetu ni kuleta matrekta makubwa, ‘powertillers’, pamoja na mashine za kuvunia. Vifaa hivyo vitasaidia kuongeza tija na kupunguza gharama za uzalishaji,” amesema Dk. Mwinyi.
Soma pia: Dkt. Mwinyi: Miaka 5 ijayo tutajenga soko kubwa Kinyasini