Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
MWINJILISTI wa Kanisa la Penuel Healing Ministry, Alphonce Temba amewataka wachungaji na maaskofu kuacha kushinikiza kubadilishwa kwa siku ya kupiga kura na badala yake kuwataka watumie siku hiyo kuliombea taifa na kupiga kura.
Jumanne iliyopita Jukwaa la Wakristo Tanzania liliiomba serikali kubadilisha siku ya uchaguzi kutoka Jumapili hadi siku nyingine ya katikati ya wiki, likieleza kuwa Jumapili ni siku ya kuabudu na hivyo isitumiwe kuamua mustakabali wa nchi.
Jukwaa hilo ni chombo kipya kinachoundwa na Baraza la Maaskofu Tanzania (Tec), Baraza la Maaskofu wa Pentekoste( PCT) na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), ambayo inahusisha makanisa ya Kiprotestanti.
Lakini Mwinjilisti Temba alisema haoni sababu ya viongozi wa chombo hicho kuanza kuhamasishana kuipinga siku ya Jumapili, akisema kila siku ni siku ya kuabudu kwa kila aliye hai.
Alisema viongozi hao walipaswa kuwahimiza waumini wao wajiandikishe kabla na kisha waitumie siku ya Jumapili ya uchaguzi kufanya maombi maalumu, ili taifa liondokane na majanga na baadaye wapige kura kama watu walio na upako.
"Sioni kama kuna tatizo, sioni kwa sababu kila aliye hai, ni lazima amche Mwenyezi Mungu kila siku... na Jumapili imetengwa rasmi kwa ajili ya wote tuwe ndani ya ibada," alisema mwinjilisti huyo ambaye kanisa lake lipo Ubungo Kibangu.
"Kwa maoni yangu kama Mungu anasema mamlaka zote ameziweka yeye na tusizipinge, basi tungetumia hiyo siku ya Jumapili kufanya maombi maalumu na ibada ihusu uchaguzi halafu tukaenda kupiga kura," alisema.
"Kama wachungaji, maaskofu na wainjilisti wangeweza kufanya maombi nchi nzima; wakaliombea taifa kwa ajili ya uchaguzi na baada ya hapo wakaenda kupiga kura, wasingepoteza lolote.
"Mwaka 2006 nilienda DRC ambako kulikuwa kunafanyika uchaguzi mkuu kwa mara ya kwanza wa kidemokrasia na kulikuwa na hofu nyingi sana, lakini nchi nzima ilihamasishwa na walifanya ibada kuanzia asubuhi mpaka saa 4:00... ibada ilikuwa maalumu kwa ajili ya kuombea uchaguzi; kuombea taifa liwe na amani na baadaye watu wakaenda kupiga kura.
"Ni siku nzuri kwa sababu tunataka majanga mbalimbali kama udanganyifu yaondoke."
Juzi mwinjilisti huyo alimtembelea Rais Jakaya Kikwete kwenye Ikulu ndogo ya mjini Moshi mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya kumtia moyo wakati huu ambao uchaguzi mkuu unakaribia.
"Nilifanya hivyo sababu kama mtumishi wa Mungu, kamisheni yangu mimi ni kufanya maombi kwenye jambo lolote lile. Sisi ni watu tunaopeleka matatizo ya waumini kwa Mungu kwa kuwa Biblia inazungumza wazi katika Warumi 13:13," alisema akifafanua kuwa Wakristo wote wanapaswa kuzitii mamlaka kuu za nchi kwa kuwa zimewekwa na Mungu.
"Mwaka 2005 tulifanya naye maombi na magazeti yaliandika kwamba ni chaguo la Mungu na nisingeweza kuacha kurudi tena," alisema.
Mwinjilisti apinga maaskofu kuhusu siku ya uchaguzi
Jumanne iliyopita Jukwaa la Wakristo Tanzania liliiomba serikali kubadilisha siku ya uchaguzi kutoka Jumapili hadi siku nyingine ya katikati ya wiki, likieleza kuwa Jumapili ni siku ya kuabudu na hivyo isitumiwe kuamua mustakabali wa nchi.
Jukwaa hilo ni chombo kipya kinachoundwa na Baraza la Maaskofu Tanzania (Tec), Baraza la Maaskofu wa Pentekoste( PCT) na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), ambayo inahusisha makanisa ya Kiprotestanti.
Lakini Mwinjilisti Temba alisema haoni sababu ya viongozi wa chombo hicho kuanza kuhamasishana kuipinga siku ya Jumapili, akisema kila siku ni siku ya kuabudu kwa kila aliye hai.
Alisema viongozi hao walipaswa kuwahimiza waumini wao wajiandikishe kabla na kisha waitumie siku ya Jumapili ya uchaguzi kufanya maombi maalumu, ili taifa liondokane na majanga na baadaye wapige kura kama watu walio na upako.
"Sioni kama kuna tatizo, sioni kwa sababu kila aliye hai, ni lazima amche Mwenyezi Mungu kila siku... na Jumapili imetengwa rasmi kwa ajili ya wote tuwe ndani ya ibada," alisema mwinjilisti huyo ambaye kanisa lake lipo Ubungo Kibangu.
"Kwa maoni yangu kama Mungu anasema mamlaka zote ameziweka yeye na tusizipinge, basi tungetumia hiyo siku ya Jumapili kufanya maombi maalumu na ibada ihusu uchaguzi halafu tukaenda kupiga kura," alisema.
"Kama wachungaji, maaskofu na wainjilisti wangeweza kufanya maombi nchi nzima; wakaliombea taifa kwa ajili ya uchaguzi na baada ya hapo wakaenda kupiga kura, wasingepoteza lolote.
"Mwaka 2006 nilienda DRC ambako kulikuwa kunafanyika uchaguzi mkuu kwa mara ya kwanza wa kidemokrasia na kulikuwa na hofu nyingi sana, lakini nchi nzima ilihamasishwa na walifanya ibada kuanzia asubuhi mpaka saa 4:00... ibada ilikuwa maalumu kwa ajili ya kuombea uchaguzi; kuombea taifa liwe na amani na baadaye watu wakaenda kupiga kura.
"Ni siku nzuri kwa sababu tunataka majanga mbalimbali kama udanganyifu yaondoke."
Juzi mwinjilisti huyo alimtembelea Rais Jakaya Kikwete kwenye Ikulu ndogo ya mjini Moshi mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya kumtia moyo wakati huu ambao uchaguzi mkuu unakaribia.
"Nilifanya hivyo sababu kama mtumishi wa Mungu, kamisheni yangu mimi ni kufanya maombi kwenye jambo lolote lile. Sisi ni watu tunaopeleka matatizo ya waumini kwa Mungu kwa kuwa Biblia inazungumza wazi katika Warumi 13:13," alisema akifafanua kuwa Wakristo wote wanapaswa kuzitii mamlaka kuu za nchi kwa kuwa zimewekwa na Mungu.
"Mwaka 2005 tulifanya naye maombi na magazeti yaliandika kwamba ni chaguo la Mungu na nisingeweza kuacha kurudi tena," alisema.
Mwinjilisti apinga maaskofu kuhusu siku ya uchaguzi