Mtafaruku umezuka Wilaya ya Bagamoyo baada ya watu wanaodhaniwa kuwa waumini wa dini ya Kiislamu wa msikiti wa Majani Mapana kuvamia makaburi ya kiislamu ya Tandika Kata ya Magomeni kwa lengo la kutaka kubomoa kaburi moja la mtoto Aruina Rolan Mitaban.
Watu hao walitaka kubomoa kaburi hilo wakidai kuwa mtoto aliyezikwa katika makaburi hayo ni Mkristo, hivyo haruhusiwi kwa kuwa si muumini wa dini ya Kiislamu.
Tukio hilo limetokea juzi wa Jumapili na waumini hao baada ya kulibomoa kaburi hilo, waliwataka ndugu wa marehemu kufukua mwili wa mtoto huyo kabla wao hawajachukua hatua za kufukua.
Walisema kitendo cha Wakristo kwenda kuuzika mwili huo katika makaburi hayo na kuujengea kwa marumaru na kuweka msalaba ni uchokozi kwa waumini wa dini ya Kiislamu.
Kutokana na tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi, alilazimika kuitisha kikao cha dharura cha Kamati ya Ulinzi na Usalama suala hilo ili kulipatia ufumbuzi.
Kipozi aliwataka waumini wa dini zote mbili kujenga tabia ya kuvumiliana wanapokuwa na matatizo badala ya kuendekeza jazba na hasira ambazo haziwezi kuleta tija.
Mwili wa mtoto huo baada ya kufukuliwa na ndugu wa marehemu walikwenda kuuzika upya jijini Dar es salaam.
Watu hao walitaka kubomoa kaburi hilo wakidai kuwa mtoto aliyezikwa katika makaburi hayo ni Mkristo, hivyo haruhusiwi kwa kuwa si muumini wa dini ya Kiislamu.
Tukio hilo limetokea juzi wa Jumapili na waumini hao baada ya kulibomoa kaburi hilo, waliwataka ndugu wa marehemu kufukua mwili wa mtoto huyo kabla wao hawajachukua hatua za kufukua.
Walisema kitendo cha Wakristo kwenda kuuzika mwili huo katika makaburi hayo na kuujengea kwa marumaru na kuweka msalaba ni uchokozi kwa waumini wa dini ya Kiislamu.
Kutokana na tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi, alilazimika kuitisha kikao cha dharura cha Kamati ya Ulinzi na Usalama suala hilo ili kulipatia ufumbuzi.
Kipozi aliwataka waumini wa dini zote mbili kujenga tabia ya kuvumiliana wanapokuwa na matatizo badala ya kuendekeza jazba na hasira ambazo haziwezi kuleta tija.
Mwili wa mtoto huo baada ya kufukuliwa na ndugu wa marehemu walikwenda kuuzika upya jijini Dar es salaam.