Mwili wa Marehemu Jaji Harold Nsekela waagwa Dodoma, Rais Magufuli ahudhuria

Brightg

JF-Expert Member
Sep 24, 2013
373
660
TBC kuna mchungazi kwenye msiba wa Judge Nsekela anashusha nondo msikilizeni. Siamini masikio yangu, msikilizeni mchungaji.

Pia, Soma=>Kamishna wa Maadili, Jaji Harold Nsekela afariki dunia

========
Nsekela.jpg

WASIFU WA MAREHEMU NSEKELA

Kuzaliwa:
29 Oct 1944

Alisoma shule ya msingi na kati Mpuguso, Rungwe kati ya mwaka 1951 na mwaka 1958 kisha akaendelea na masomo ya shule ya sekondari Malangali kati ya mwaka 1959 na mwaka 1962. Mwaka 1963 alijiunga na shule ya sekondari wavulana Tabora na kuhitimu mwaka 1964.

Alihitimu Shahada ya sheria chuo kikuu cha Afrika Mashariki mwaka 1968 na mwaka 1970 alihitimu shahada ya uzamili chuo kikuu cha Yale nchini Marekani.

AJIRA
1968-1970:
Mhadhari msaidizi kitivo cha sheria chuo kikuu cha Afrika Mashariki

1971-1974: Mhadhiri chuo kikuu cha Dar es Salaam

1975-1976: Mhadhiri chuo kikuu cha usimamizi wa fedha

1976-1997: Alifanya kazi katika nafasi mbalimbali kwenye shirika la sheria Tanzania

Mei 1997: Aliteuliwa kuwa Jaji wa mahakama kuu ya Tanzania

Februari 2003: Aliteuliwa kuwa Jaji wa mahaka ya rufaa Tanzania

Novemba 2006: Aliteuliwa kuwa Jaji wa mahakama ya Afrika Mashariki

Julai 2008: Aliteuliwa kuwa makamu wa Rais wa mahakama ya Afrika Mashariki

Novemba 2008- June 2014: Rais Mahakama ya Afrika Mashariki

Mei 2014: Mjumbe wa Taasisi wa waamuzi(Tanzania Institute of Arbitrators)

Disemba 2016: Aliteuliwa kuwa kamishna wa maadili na amekuwa katika nafasi hiyo hadi mauti yalipomkuta Disemba 6, 2020 saa mbili asubuhi.

NDOA NA FAMILIA

Marehemu alifunga ndoa na mke wake Subilaga Nsekela Julai 9, 1977. Marehemu ameacha watoto wanne na wajukuu watatu.

UGONJWA NA KIFO
Marehemu aliugua kwa muda mfupi na kufariki tarehe 06/12/2020 saa mbili asubuhi.

NENO LA SHUKRANI(FAMILIA)
Andende Kisye Nsekela(Mtoto wa marehemu):
Natanguliza shukrani zangu binafsi na familia nzima kwa waganga wote wa hospitali ya mission ya DCMC iliyopo Ntyuka, waganga wote wa hospitali ya Dodoma, wafanyakazi wote wa tume ya maadili Tanzania, wafanyakazi wote wa mahakama zote Tanzania, serikali kwa ujumla wote. Kipekee ningependa kumshukuru mheshimiwa Rais Magufuli ambae alimuamini baba yetu na kuweza kumpatia kazi ya kutumika nae katika Taifa.

 
Huyu ndiye alishirikiana na Ndugai kumpokonya ubunge Tundu Lissu. Alisema kuwa Tundu Lissu hajapeleka tatamko la mali zake wakati alikuwa anafahamu kuwa Tundu Lissu hakuwa nchini kwa sababu ya matibabu. Ndugai akamfuta ubunge.
 
Siwezi kumsahau abadani huyu jaji Nsekela, alipindisha haki ya mirathi ya baba yetu enzi zile. Tulikosa kila kitu, ila Mungu ni mwema wote tuna maisha yetu mazuri tu.
Msamehe mkuu wanadamu wote tunamapungufu na mara nyingi tunapopata madaraka tunajisahau sana, Power and money comes and goes but our humanity lives forever,may Almighty God of universe strengthen the bereaved family,
 
Kuna baadhi ya vitu utavifahamu baadae - huyo alikuwa hazina


[IMG alt="Evarm"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/25/25747.jpg?1395864701[/IMG]

Evarm

JF-Expert Member​

Aug 30, 2010 1,775 2,000

Siwezi kumsahau abadani huyu jaji Nsekela, alipindisha haki ya mirathi ya baba yetu enzi zile. Tulikosa kila kitu, ila Mungu ni mwema wote tuna maisha yetu mazuri tu.

Everything in your life is a reflection of a choice you have made. If you want a different result, make a different choice.
Thanks Quote Reply
Report
  • Thanks
Reactions: Msingida
 
Huyu ndiye alishirikiana na Ndugai kumpokonya ubunge Tundu Lissu. Alisema kuwa Tundu Lissu hajapeleka tatamko la mali zake wakati alikuwa anafahamu kuwa Tundu Lissu hakuwa nchini kwa sababu ya matibabu. Ndugai akamfuta ubunge.
Kwa hiyo tatizo lipo wapi hapo?
 
Huyu ndiye alishirikiana na Ndugai kumpokonya ubunge Tundu Lissu. Alisema kuwa Tundu Lissu hajapeleka tatamko la mali zake wakati alikuwa anafahamu kuwa Tundu Lissu hakuwa nchini kwa sababu ya matibabu. Ndugai akamfuta ubunge.
Upo sahihi mkuu amepata haki yake, pia anatoka kabila gani?
 
[IMG alt="Evarm"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/25/25747.jpg?1395864701[/IMG]

Evarm

JF-Expert Member​

Aug 30, 2010 1,775 2,000

Siwezi kumsahau abadani huyu jaji Nsekela, alipindisha haki ya mirathi ya baba yetu enzi zile. Tulikosa kila kitu, ila Mungu ni mwema wote tuna maisha yetu mazuri tu.

Everything in your life is a reflection of a choice you have made. If you want a different result, make a different choice.
Thanks Quote Reply
Report
Reactions: Msingida
Safi kabisa hakuna kusamehe ni pua kwa pua
 
Huyu ndiye alishirikiana na Ndugai kumpokonya ubunge Tundu Lissu. Alisema kuwa Tundu Lissu hajapeleka tatamko la mali zake wakati alikuwa anafahamu kuwa Tundu Lissu hakuwa nchini kwa sababu ya matibabu. Ndugai akamfuta ubunge.
Pamoja na kumfanyia unyama wote. kamwacha Tundu Lissu akipata Oxygen ya Mwenyezi Mungu yeye katangulia kuliwa na sisimizi.
 
Huyu ndiye alishirikiana na Ndugai kumpokonya ubunge Tundu Lissu. Alisema kuwa Tundu Lissu hajapeleka tatamko la mali zake wakati alikuwa anafahamu kuwa Tundu Lissu hakuwa nchini kwa sababu ya matibabu. Ndugai akamfuta ubunge.
Kumbe
Huyu ndiye alishirikiana na Ndugai kumpokonya ubunge Tundu Lissu. Alisema kuwa Tundu Lissu hajapeleka tatamko la mali zake wakati alikuwa anafahamu kuwa Tundu Lissu hakuwa nchini kwa sababu ya matibabu. Ndugai akamfuta ubunge.
Kumbe marehemu alikuwa na roho mbaya hivyo?
 
Back
Top Bottom