DALLAI LAMA
JF-Expert Member
- Jan 31, 2012
- 8,652
- 2,642
Migulubaja Savimbi ni janga kuu la amani ya nchi.
naibu katibu mkuu wa ccm na naibu waziri wa fedha mwigulu nchemba amesema chama cha mapinduzi (ccm)kinashangazwa na kitendo cha chama cha demokrasia na maendeleo (chadema)kutumia helikpota kwenye chaguzi zake huku kikidai kuwa ni mkombozi wa wananchi jambo ambalo ni kujitafutia sifa na umaarufu pekee kwa wananchi.
posted: 29 jan 2014 07:44 am pst
![]()
naibu katibu mkuu wa ccm na naibu waziri wa fedha mwigulu nchemba
---
na mwandishi wetu, arusha chama cha mapinduzi (ccm)kimesema kuwa kinashangazwa na kitendo cha chama cha demokrasia na maendeleo (chadema)kutumia helikpota kwenye chaguzi zake huku kikidai kuwa ni mkombozi wa wananchi jambo ambalo ni kujitafutia sifa na umaarufu pekee kwa wananchi.
hayo yameelezwa na naibu katibu mkuu wa ccm ambaye pia ni naibu waziri wa fedha mwigulu nchemba wakati akifungua rasmi kampeni za udiwani katika kata ya sombetini . Mwigulu alisema kuwa ccm inashangaa sana chadema kutumia helikpota kwenye chaguzi nyingi hapa nchini jambo ambalo wanaonesha wazi kuwa wanatumia gharama kubwa kwa ajili ya kuongeza sifa kwani gharama ambazo zinatumika hadi kumalizika kwa kampeni ni zaidi ya milioni 200.
alisema kuwa gharama ambayo inatumika kwenye uendeshaji wa helkopta ni gharama ambayo ingeweza kuwasaidia wanachama wao lakini hata matumizi mbalimbali ya chama hicho ambacho bado kinaonekana kukabiliwa na changamoto nyingi sana wananchi wa kata ya sombetini napendwa kuwaambia kuwa hata sisi wenyewe huwa tunashangaa sana ujio wa hii helikopta na ninapenda kusema wazi helikopta hiyo inakuja ili iweze kuwazubaisha ninyi sasa msikubali kudanganywa na helikopta baliangalieni sera za mgombea aliongeza mwigulu
pia aliwataka wananchi kuhakikisha kuwa kamwe hawatumiki kwenye siasa za sifa na ushahbiki kwani siasa hizo wakati mwingine zinasababisha hata vifo vya watu ambao hawana hatia ya kufa ovyo wananchi mnapswa kujua na kutambua kuwa siasa za sasa zimebadilika sana msikubali kuwa mashabiki wa siasa bali mnatakiwa kuangalia zaidi sera za vyama na mahitaji yenu msije mkachagua kiongozi kwa ushabiki itawagharimu sana kwenye utendajialiongeza mwigulu
awali mgombea udiwani katika kata hiyo ya sombetini kwa tiketi ya ccm alisema bw david mollel alisema kuwa ana mikakati mingi sana ya kuhakikisha kuwa anasaidia kata hiyo endapo kama atapata ridhaa ya kuongoza rasmi kama diwani david alisema kuwa changamoto ambazo atahakikisha kuwa ameweza kuzitatua ni pamoja na urekebishaji wa barabara, uboreshaji wa masoko,kna uimarishaji wa vikundi vya wanawake na jamii kwa ujumla
[huyu ndiye naibu waziri wa fedha zetu na naibu katubu mkuu bara wa ccm]
tusaidiane kuchambua hoja ya mwigulu mchemba sijui alilenga kuwambia nini wana arusha
Na huyo mkuu wa nyumba anasafiri kila kukicha tusemeje?200M ni ndogo? zinaweza kuhudumia ofisi ngapi za chama nchi nzima?