Mkuu
Mwigulu Nchemba,leo hukuongea kauli nzuri kiutawala. Leo umemkosea heshima Rais wa Tanzania. Afadhali ungeishia kusema tu kuwa unatamani kuwa Rais wa Tanzania (lengo kuu la kila mwanasiasa wa Tanzania). Kusema kuwa unatamani kuwa Rais ili uwafunze watu adabu ni kumkosea heshima Rais wa nchi. Ina maana kuwa Rais anaongoza watanzania/wapinzani wasio na adabu?
Ina maana kuwa Rais wa Tanzania hana uwezo wa kuwashikisha/kuwafunza adabu wananchi wake na wapinzani wake? Hii si kauli ya kiuongozi na kiungwana. Ukiwa kama Naibu Waziri wa Fedha wa Serikali inayoongozwa na Rais Kikwete, na kwa staha na ustaarabu wa kisiasa, ingawa umetamka maneno hayo Bungeni, huna budi kumuomba msamaha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Na maneno yako au ya aina hiyo hayapaswi kurudiwa tena.