Mwigulu Nchemba aivaa CHADEMA na Dr. Slaa

Mwigulu Nchemba aivaa CHADEMA na Dr. Slaa

utaifakwanza

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2013
Posts
14,193
Reaction score
2,815
MH>MWIGULU LAMECK NCHEMBA AMVAA DR.SLAA NA CHADEMA YAKE,AMUSIHI DR.SLAA AREJEE KUCHUNGA KONDOO WA BWANA KWA SABABU MUNGU ANASEMA HATAKAMA DHAMBI ZAKO NI NYEKUNDU KAMA DAMU,ATAZITAKASA NA KUWA NYEUPE KAMA THERUJI.

AFANIKISHA HARAMBEE YA TSH.MILIONI 19,AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO JIMBONI KWAKE IRAMBA MAGHARIBI.

Naibu katibu mkuu wa CCM na mbunge wa jimbo la Iramba magharibi ameshiriki kikamilifu kwenye harambee ya ujenzi wa kanisa wilaya ya singida Vijijini,kata ya Kijota Usharika wa Mijuhu jimbo la Mashariki Dayosisi ya kati KKKT.

Mbunge huyo amefanikisha upatikanaji wa Tsh.Milioni 19 na laki tisa na themanini.Pia amefakisha upatikanaji wa viti 500 vya plastic kama hatua ya awali katika kufanikisha ujenzi wa kanisa hilo.

Ikumbukwe Mbunge huyo anayevuma kwenye medani za siasa yawezekana kuliko mbunge yeyote kwa sasa hapa nchini,yupo jimboni kwake kukagua na kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo.Jana alianza kwa kufanya vikao vya ndani na madiwani na viongozi mbalimbali wa chama na serikali.

Pia siku ya jana alitumia kuhamasisha michezo jimboni kwake na wilaya mpya ya Mkalama ambapo Mbunge huyo alishiriki kucheza mechi ya mpira wa miguu akiwa upande wa madiwani.

Kwenye harambee ya leo mbunge huyo Mh.Mwigulu Lameck nchemba madelu alitumia nafasi kuongea na washarika na wananchi wa kata ya kijota,kijiji cha Ikuwi kuwaomba kuachana na tabia ya kulishwa maneno na wanasiasa na viongozi mbalimbali kuhusu serikali yao eti haifanyi kazi.

Amesisitiza kuwa endapo wananchi na viongozi wa vyama vya siasa wangemrudia mungu,wangejikita kusaidia ujenzi wa nyumba za ibada,kushiriki kwenye huduma za kiroho leo hii Tanzania tusingekuwa na aina hii ya viongozi wa vyama vya siasa hasa upinzani wenye uroho wa madaraka,wanaomwaga damu za watanzania ili tu wapate madaraka ndani ya nchi hii.

Mh.Mwigulu nchemba amekwenda mbali zaidi kwa kulaani vikali kauli ya kiongozi wa CHADEMA Dr.slaa yakuwambia viongozi wa dini waache kuombea amani ya nchi.Amesema viongozi kama hao ni wakupuuzwa kabisa kabisa,na niwazi Dr.slaa na chama chake hana nia njema kwa nchi yetu.Ni kwasababu aliachana na misingi ya dini na kiroho ndio maana uwezo wake wa kufikiri kuhusu amani ya nchi ni hafifu kupita kiasi.

Leo Mh.Mwigulu Nchemba ametembelea ujenzi wa barabara mbali mbali ndani ya jimbo lake.Akiwa ameambatana na DC na Mkurugenzi wa wilaya,Mh.Mwigulu Nchemba ameona ujenzi wa barabara kata ya Kidalu barabara inayounganisha wananchi na makao makuu ya wilaya.

Ni barabara inayojengwa na TANROAD kwa kiwango cha changalawe.Pia amezungukia sehemu kadhaa za barabara zinazotajwa kuwa ni korofi kipindi cha masika,lengo likiwa ni kujenga miundombinu safi kabla masika hayajaanza.

Katika kuonesha mshikamano wa kiutendaji uliopo ndani ya jimbo la Iramba,Mbunge huyo aliambatana na madiwani wa kata na makatibu wake pamoja na viongozi wa serikali + Injinia wa wilaya ilikushauriana namna ya kufanikisha ujenzi imara na bora wa miundombinu ya barabara ndani ya jimbo la Iramba.
 
Mwigulu wako kawaweka pabaya Polisi kwa unyama wake..angalia wanavyoteseka kutoa majibu mepesi

Jeshi la Polisi limeendeleza ngonjera katika tukio la kutekwa na kuteswa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda (pichani), baada ya kushindwa kutaja watuhumiwa wa tukio hilo la kinyama kama lilivyokuwa limeahidi awali.


Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Isaya Mngulu, akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, alishindwa kutaja majina ya watu waliohusika katika matukio mbalimbali likiwamo la Kibanda ingawa alisema uchunguzi wake umeanza muda mrefu.

Mngulu akizungumzia tukio la kutekwa na kuteswa kwa Kibanda na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk. Stephen Ulimboka, alisema uchunguzi wa matukio hayo bado unaendelea.

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Said Mwema amesema upelelezi wa kesi ya kutekwa, kuteswa na kutupwa katika msitu wa Mabwepande, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk. Steven Ulimboka bado haujakamilika.

Mbali na Dk. Ulimboka, IGP alisema kesi nyingine zote za aina hiyo pamoja na za mauaji ya watu mbalimbali, akiwemo Padri wa Kanisa Katoliki la Minara Miwili lililopo Mji Mkongwe Zanzibar, Evaristus Mushi (56), uchunguzi wake unaendelea.
 
MH>MWIGULU LAMECK NCHEMBA AMVAA DR.SLAA NA CHADEMA YAKE,AMUSIHI DR.SLAA AREJEE KUCHUNGA KONDOO WA BWANA KWA SABABU MUNGU ANASEMA HATAKAMA DHAMBI ZAKO NI NYEKUNDU KAMA DAMU,ATAZITAKASA NA KUWA NYEUPE KAMA THERUJI.......
sioni cha kuchangia rekebisha tu hiyo pumba yako hapo kwenye red.
 
Mwigilu kwanza kalee yule mtoto wako - ile mimba ya yule kada wa CCM Igunga uliyobementa usiku wa kampeni.
 
Hivi Mwigulu mbona unahangaika kila siku na CHADEMA, kuliko hata Mabosi wako akina Kinana, Mangula & Jk?
 
Wadanganye wasiokujua wewe hajawahii ng,aa kwenye medali ya siasa hata ckumoja hii kuamuru watu wapigwe ndyo kung,aa kisiasa mrudie mungu wewe
 
MH>MWIGULU LAMECK NCHEMBA AMVAA DR.SLAA NA CHADEMA YAKE,AMUSIHI DR.SLAA AREJEE KUCHUNGA KONDOO WA BWANA KWA SABABU MUNGU ANASEMA HATAKAMA DHAMBI ZAKO NI NYEKUNDU KAMA DAMU,ATAZITAKASA NA KUWA NYEUPE KAMA THERUJI.
Kwa hiyo anataka kutuambia kwamba hata baada ya kufadhili mauaji ya mabomu huko arusha ambayo yaliua watu wasiokuwa na kosa lolote wakiwemo watoto, basi atasamehewa na Mungu na kuwa na Moyo msafi kama theluji? Mwigulu Nchemba mnafiki wewe! Tazama kwanza lile boriti lililo katika jicho lako ndipo utakapoona vyema kile kibanzi katika jicho la mwenzako.Umesikia Jana Meya huko ilemela naye Anatishia Kumuua Mbunge Kiwia; Kipindi kile walivyomakata kata na mapanga bado tu hawajaridhika !.Ninyi mtawadhuru binadamu wenzenu kwa maslahi ya dunia hii lakini mwishowe lazma muende motoni. Shauri yenu.
 
Last edited by a moderator:
ETI ANAONGOZA KUTAjwa na vyombo vya habari kivipi wakati cdm ndio inachangia
 
Na kweli, maana tuna punda wa unga, punda wa kucha, punda wa meno, punda wa risasi, punda wa bomoa bomoa, punda wa kukwepa kodi, punda wa kamat kamata ya polisi na JWTZ, punda wa..... punda wa......

Hahaa, huyu punda atafika kweli? Ngoja mtaji wa kisiasa wa Tesha ukiisha amwagiwe tindikali, apelekwe India halafu arudi aanze kuzunguka na Nchemba.
 
Tumeambiwa Mwigulu, kwa CCM ni Mwenyekiti, Katibu Mkuu na Katibu Mwenezi. Kwa Serikali, ni: AG, IGP, DCI, DPP. PM, Tenwa. Mahakamani ni, CJ. Bungeni ni Speaker. Swali: Mtamweza Mwigulu kwa hali hii kweli?
 
Naamini katika Wanasiasa wanaongea pumba always Mwigulu Nchemba is among of them na sijui CCM walimpa hiko cheo kwa sifa gani kwakuwa muda mwingi yeye ni kutafuta chokochoko tu badala ya kuangalia mustakabali wa Tanzania na Watanzania kwa miaka kadhaa ijayo watakuwa wapi na kwa njia ipi......ni upuuzi mtupu
 
Back
Top Bottom