Mwigulu hili hapana

kwanza hata kabla hatujaenda mbali lile swala la clouds yeye kama ni waziri analiona lipo sahihi..? kama lipo sahihi iweje hili la nape lisiwe sahihi hlf lile liwe sahihi..? ama ndo kuuma na kupuliza kwa kuogopa meno ya bwana mkubwa!
Hapo mkuu umemaliza! Mkanda ulianzia clouds hiyo tarehe 17/03/2017 kwa uvamizi wa Bashite ukihusisha askari wenye silaha waliowatisha wafanyakazi wa clouds TV, Ukahitimishwa kwa Nape kutishiwa bastola hadharani na watu wa kitengo!

Kama Mwigulu umeamua kushughulikia anzia mwanzo wa drama kule clouds hadi huyu aliyetoa bastola! Askari wote waliohusika mnawafahamu vizuri maana walitumwa na wakubwa wao! Sio wa kutafutwa! Ni wa kukamatwa! Kama hamna dhamira ya dhati acheni! Watanzania wana akili wala hawawezi kudanganywa katika hili!
 
Yule aliyemwambia mwenzake arudishe bastola uso wake ulionekana vizuri kwenye kamera na anaonekana alikuwa na busara walau! Si wakutafutwa hawa ni wa kumamatwa na mshitakiwa namba moja ni RPC wa kinondoni maana ndiye aliyewatuma na ndiye aliyetoa amri ya kuzuia mkutano kwa mujibu wa yule mfanyakazi wa hoteli.
 
Kauli ya mhe. Mwigulu ilinishangaza sana eti achunguzwe inamaana alijiamulia tu kuzuia mkutano
 
Nakuhakikishia yule si askari bali ni mtu aliyepangwa kufanya maigizo na kitenge....


Na mimi nakuunga mkono kabisaaa.

Tangu nilipokuwa naangalia clip ile kwa mara ya kwanza, nilijimbia maigizo haya huku nacheka.

Tatizo wote wanaoshinda humu kuiponda Serikali ndio wanashindilia kama haya.

M & M oyeeeeeee
 
Hivi hawa watu 2020 wataomba kura kwa watanzania tena au 2020 hakutakuwa na uchaguzi? Inanipa shida sana ninapoona hizi comedy zinazoendeshwa na hawa wanasiasa wetu.
Mh Mwigulu kaibukia kwenye bastora,siku ya silaha nzito za Clouds hajaambiwa na wala hana taarifa nazo.
 

Excellent analogy. Mkuu umetoa taswira yenyewe kabisa ya wale watetezi wakuu wa tawala dhalimu. Ni kawaida yao kukanyagana kujipendekeza kwa madikteta bila kujali wenzao wanavyopigwa panga na kudondokea njiani. Akidondoka mtu hiyo ni fursa kwa mnafiki mwingine.

Na wengi tu wameshadondoka kimyakimya. Ukishauri tuachane na ujinga huo; tujenge mfumo wa utawala wa haki na demokrasia ya kweli (katiba mpya) wanawahi kukuita mchochezi unayetaka kuvuruga amani ya nchi!

Nakumbuka ilipoletwa hoja Bungeni kuhusu haja ya rais kupunguziwa madaraka, mama Kilango alikuja juu na kudai "wanataka kumpunguzia rais wetu madaraka ili wamchezeechezee, hatutakubali!" Bila shaka kufikia leo atakuwa keshapata muda wa kutosha kutafakari upya hoja hiyo. Manake ile swanif aliyopata ya kutumbuliwa kwa kudhalilishwa kisha kufanyiwa maombi ya nguvu halafu kupewa ubunge kwenye kisahani ni shule tosha kabisa. Hapo akijisahau atake kuleta ule ujuaji wa enzi zile, kisahani kinageuzwa juu chini!

Bahati mbaya huwa ikitokea busara ikawarejea wenzetu hawa, hubakia kuwa siri yao; hatupati mrejesho; wanaingia mitini moja kwa moja!
 
Yule jamaa ni jasusi wa Kagame. Magufuli anaendeshwa na Kagame.

Inawezekana kabisa Mwigulu hamjui kweli.

Sasa hivi kuna sehemu ya serikali inaendeshwa na Magufuli binafsi hata mambo hayapitii wizarani.
 
Ufalme wa Ufaransa uliondolewa kwa kitu kilichosemwa innocently 'let them eat cake'. Hiyo kauli iliamsha kutokuridhika kulikokuwa kunafukuta chini kwa chini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…