Sahihi. Anapaswa atukamatie watuhumiwa wa kuleeee Kibiti. Hiyo ndiyo kazi hasaa. Hiyo ya walokengeuka tabia ni kama "homework" tu anaweza kuifanya hata jua likiwa limeenda sana.Anapwaya sana huku sio size yake kabisa!
Afanye nini sasa na nchi inaendeshwa kwa kiki?Anapwaya sana huku sio size yake kabisa!
.Waziri Nchemba amesema kama kuna taasisi yoyote imesajiliwa nchini na inafanya kampeni za haki za ushoga basi atafuta usajili huo na watu wake kukamata na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
“Wanaotaka haki za ushoga watafute tu nchi yao nyingine ambayo inaruhusu mambo hayo wakakae huko, kama ni taasisi imesajiliwa kwenye nchi yetu tukaigundua inafanya kampeni ya haki hizo na bahati nzuri zinasajiliwa Wizara ya Mambo ya Ndani nitazifutia usajili wao…
…..na kama ni raia wa Tanzania anaendesha kampeni hizo tutamkamata na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria, na kama si raia amekuja kwenye nchi yetu kuja kuendesha haki hizo tutampa amri ya kuondoka ndani ya nchi yetu hatapata fursa hata ya kuchomoa chaji ya simu kwenye soketi ya umeme” amesema Nchemba.
Kwa upande mwingine Waziri Nchemba amemuunga mkono kauli ya Rais Magufuli dhidi ya wanafunzi ambao watapata ujauzito wakiwa shuleni na kusema watu wanaopinga jambo hilo wasitumie nguvu kubwa kupinga bali wajenge shule zao wao watoe hiyo haki ya kusomesha wanafunzi wajawazito au wale ambao tayari wamejifungua na siyo kulazimisha serikali kufanya hayo.