Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,446
- 7,822
Akiwa bungeni leo Juni 26, 2023, waziri wa fedha, Mwigulu Nchemba wakati akihitimisha hoja ya makadirio ya bajeti amemkalia kooni mbunge mwenzeke, Luhaga Mpina kwa madai alikuwa anafungia viwanda alipokuwa waziri huku akifurahia. Mwigulu amesema Mpina alikuwa anafanya sherehe kwa kuchoma nyavu bila kuzidhibiti kuingia.
Mwigulu amesema Rais Samia anawafundisha shughuli za uzalishaji ziheshimiwe na inapotokea matatizo kuwe na utaratibu wa kiungwana wa kurekebisha na kuacha kufunga biashara.
Mwigulu amemwambia Mpina kuwa si ubingwa wala ustaarabu kupinga kila kitu hata ambavyo havistahili kupingwa.
======
Amemshauri Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina kuwa si ubingwa wala si ustaarabu kupinga kila kitu hata visipopaswa kupingwa, badala yake anaweza kuuliza kwa namna nzuri ili aeleweshwe. Ameyasema haya wakati akirejea hoja ya Mpina iliyokata biashara zifungiwe.
Ametolea mfano alivyokuwa anafunga viwanda, kuchoma nyavu akiwa Waziri kuwa matendo hayo hayakuwa ya kistaarabu. Watu wa Sekta binafsi sio maadui, ni washirika wa maendeleo.
Katika kufungia biashara za watu ni muhumu kuzingatia mitaji yao, uwekezaji na muda wanaotumia kuwekeza na kufanya biashara hizo. Hauwezi kukaa na mtaji wa mtu umeushikilia huku yeye akiumia.
Mwigulu amesema Rais Samia anawafundisha shughuli za uzalishaji ziheshimiwe na inapotokea matatizo kuwe na utaratibu wa kiungwana wa kurekebisha na kuacha kufunga biashara.
Mwigulu amemwambia Mpina kuwa si ubingwa wala ustaarabu kupinga kila kitu hata ambavyo havistahili kupingwa.
======
Amemshauri Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina kuwa si ubingwa wala si ustaarabu kupinga kila kitu hata visipopaswa kupingwa, badala yake anaweza kuuliza kwa namna nzuri ili aeleweshwe. Ameyasema haya wakati akirejea hoja ya Mpina iliyokata biashara zifungiwe.
Ametolea mfano alivyokuwa anafunga viwanda, kuchoma nyavu akiwa Waziri kuwa matendo hayo hayakuwa ya kistaarabu. Watu wa Sekta binafsi sio maadui, ni washirika wa maendeleo.
Katika kufungia biashara za watu ni muhumu kuzingatia mitaji yao, uwekezaji na muda wanaotumia kuwekeza na kufanya biashara hizo. Hauwezi kukaa na mtaji wa mtu umeushikilia huku yeye akiumia.