Mwigulu Nchemba: Kodi za Tanzania ni kubwa sababu walipa Kodi ni Wachache

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 55, leo Juni 26, 2023.



Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Mwigulu Nchemba amesema fedha zinazopelekwa kwenye Mikopo ya Elimu ya juu ndani ya mwaka mmoja wa fedha kwa sasa ni kubwa zaidi kuwahi kutolewa tangu uhuru. Hali ipo hivyo pia kwenye Sekta ya Kilimo, Afya, Uvuvi na mifugo na Maji.

Aidha, fedha za mafao ya wastaafu, Maslahi ya watumishi wa Umma, kuvutia uwekezaji, Ulinzi na Usalama pamoja na miradi ya kimikakati ni nyingi kuliko kipindi chochote kile.

Amesema hoja zote zilizotolewa na wabunge wakati wa kuchangia mjadala wa Bajeti ikiwemo ujenzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza na Barabara mbalimbali nchini zitashughulikiwa.

Suala la kulipa kodi linaitambulisha nchi kwenye uhuru, uwezo wa kutekeleza miradi ya maendeleo na uwezo wa kujitegemea. Wabunge wanapaswa kuwahimiza wananchi wote kulipa kodi ili nchi iweze kushushwa. Aidha, Waziri Mwigulu amesema kodi zinazotozwa nchini ni kubwa kwa sababu watu wengi hawalipi kodi, mzigo wa kulipa kodi hudondoka kwa watu wachache.

Kuhusu hoja ya mafuta ya kula, Waziri Nchemba amesema wametoa unafuu kwa wazalishaji wa ndani kama motisha kwao, na mabadiliko hayo yatatolewa kwenye jedwali la mabadiliko (Schedule of Amendments). Pia, Serikali itadhibiti uingizwaji holela wa mafuta nchini kama sehemu ya kuwajali wakulima wa ndani.

Amemshauri Mbunge wa Kisesa Lugaha Mpina kuwa si ubingwa wala si ustaarabu kupinga kila kitu hata visipopaswa kupingwa, badala yake anaweza kuuliza kwa namna nzuri ili aeleweshwe. Ameyasema haya wakati akirejea hoja ya Mpina iliyokata biashara zifungiwe.

Ametolea mfano alivyokuwa anafunga viwanda, kuchoma nyavu akiwa Waziri kuwa matendo hayo hayakuwa ya kistaarabu. Watu wa Sekta binafsi sio maadui, ni washirika wa maendeleo.

Katika kufungia biashara za watu ni muhumu kuzingatia mitaji yao, uwekezaji na muda wanaotumia kuwekeza na kufanya biashara hizo. Hauwezi kukaa na mtaji wa mtu umeushikilia huku yeye akiumia.
 
Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

6C5AF277-5F30-4B31-BB23-A235BA3BD0AA.jpeg
 
Hauko siriazi, bora nilale kuliko kupoteza muda kuangalia bunge
 
1.Hivi hili bunge linawakilisha wananchi kweli!
2.Lina ridhaa ya wananchi kweli!
Nahisi linawakilisha maslahi binafsi ya ccm na sio wananchi hata kdg!
 
Back
Top Bottom