Mwigulu akalia kuti kavu Iramba Magharibi

Mwigulu akalia kuti kavu Iramba Magharibi

Status
Not open for further replies.
Hali
ya chuki dhidi ya
CHADEMA inayoonyeshwa na mbunge wa Iramba Magharibi dhidi ya CHADEMA
imesababisha wafuasi wa CHADEMA kote nchini kuungana kuhakikisha CHADEMA
inamshinda kwa kishindo kwenye uchaguzi mkuu katika jimbo la Iramba
2015.

Mwigulu Nchemba anakabiliana na Msomi aliyebobea Dr Kitila Mkumbo ambaye
ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA.

Pia wafuasi wa CHADEMA wameapa kuhakikisha CHADEMA inazoa viti vyote vya
udiwani Iramba Magharibi ili kumuonyesha ni nini maana ya nguvu ya
umma.

Katika mahojiano na wafuasi kadhaa wa CHADEMA wa mikoa ya Mara,Kagera na
Mwanza wameutaka uongozi wa CHADEMA kuanzisha Akaunti maalum ambayo
itachangiwa na wanachama kuhakikisha Mwigulu harudi bungeni.

Wanachama hao wamesema chuki ya Mwigulu dhidi ya Chadema hailezeki na
ameapa kutumia njia zozote kuiangamiza CHADEMA.Wamesema hata awapo
bungeni hatetei chochote wanaIramba zaidi ya kutukana na kukashifu
viongozi wa CHADEMA.

Hii itakuwa ni Operesheni Ondoa Mwigulu Iramba(OMI) walisema wafuasi hao
wa Chadema.Pia walisema watajitolea kukaa Iramba kipindi chote cha
Kampeni kuhakikisha Mgombea wa CHADEMA anapata ushindi wa 80%.

Kwa sasa Jimboni Iramba Dr Kitila Mkumbo anazungumzwa kila kona ya Jimbo
hilo kama mwanasiasa makini,mpole na mtetezi wa dhati wa wananchi.Mzee
mmoja katika kata ya Ndago Iramba aliwahi kusema mwaka jana kuwa kwa
kawaida watu wa Iramba ni wanyenyekevu na wenye kupima maneno kabla ya
kuzungumza mfano wa Dr Kitila.Mzee huyo alisema hawakuwahi kujua kama
kuna siku wangekuwa na mbunge mwenye kuhamasisha chuki ndani ya jamii
kiasi cha kuhatarisha amani ya nchi.
Kosa Kuu la Mwigulu ni kumfungulia kesi Dk. Kitila huko Singida, hivyo
kumwezesha kwenda jimboni kila kesi inaposikilizwa, hadi kesi
inamalizika atakuwa ameshavuruga jimbo zima.
 
Wakuu chama,ritz,chris lukosi,kingukitano, bungeni,m23 nataka niwahakikushie kuwa CDM hata wakaleta ruzuku yao na michango yao yote kamwe MWIGULU hawatamuweza. Jamani acheni kujidanganya Dr Mkumbo hata nyumbani kwao MGELA hawamjuwi hv ubunge munatoa nyie humu JF? Tena anzeni kuchangisha leo.

BABU yenu mkija nae akaanza kuangalia wake wake zetu ndio utakuwa mwisho wake wahaya na wanyiramba ni tofauti. Chonde chonde BABU utakufa huku acha ulafi wako kinondoni..

shelui=mwigulu naona unaomba tafu kwa vijana wako.tembo amelitia maji time will tell
 
Nitamchangia bwana Zitto, Mnyika, Mkumbo, Mdee na Shamsi Vuai Nahodha, mkianza kampeni tu nitawasaidia

Hakika wewe umeiva kwa kumhusisha Shamsi Vuai Nahodha, najua unapanga kuchagua mtu na sio chama, good mission ila kigezo ulichotumia kuminclude huyo jamaa sikijui labda kwa kuwa mimi ni maamuma kwa siasa za Nahodha!
 
shelui=mwigulu naona unaomba tafu kwa vijana wako.tembo amelitia maji time will tell

Ni kweli mkuu naona ameona hapati suport ameingia mwenyewe nakuomva msaada kwa vibaraka wake bila kujua hata wao wamemchoka.Mwigulu asahau mjengoni 2015 hawezi kanyaga viwanja vya bunge.R I P mwigulu
 
Hakika wewe umeiva kwa kumhusisha Shamsi Vuai Nahodha, najua unapanga kuchagua mtu na sio chama, good mission ila kigezo ulichotumia kuminclude huyo jamaa sikijui labda kwa kuwa mimi ni maamuma kwa siasa za Nahodha!

Nadhani ni kwa sababu ya siasa zake zenye staha. Sijawahi kusikia Nahodha akitoa majibu ya hovyo wala lugha chafu hususani bungeni kama wanavyofanya akina Nchimbi, Wasira, Lukuvi etc.
 
Dr Mkumbo ajipange sana maana huyu dogo ni mchawi sana!
 
Mimi ni mwana Chadema, nipo Iramba. Sio kweli kuwa Mkumbo ni gumzo mji mzima wa Kiomboi. Wakazi wa Kiomboi wanaishi tu kama hawana mbunge lakini wala hawana fikra za huyo Kitila. Molemo usiwe mwongo hivyo
Post haijasema mji wa kiomboi mkuu. Imesema kila kona ya jimbo la iramba. Hata hivyo sio nia yangu kusema ni kweli au uongo ila kuonyesha kuwa inaweza ikawa sio kiomboi lakini ni maeneo mengine nje na kiomboi ambayo nayo wewe haupo. Ni hilo tu
 
Last edited by a moderator:
Naapa nipo tayari kujiunga katika kampeni OMI na kuchangia kadiri niwezavyo,tuombeni uhai
 
huyu alikuja hapa tegeta dar akagawa pikipiki eti anataka jimbo la halima mdee nikacheka sana...

yaan huyu jamaa kwa kuhonga utadhani hakula kiapo cha ccm. Ccm wana kiapo kizuri ambacho kinapiga vita rushwa lakini hakuna hata mmoja anayekitendea haki. Hebu chama au ritz tukumbushe kiapo chenu ili tujue kama mnakiishi au lah! Nawakilisha
 
Mimi ni mwana Chadema, nipo Iramba. Sio kweli kuwa Mkumbo ni gumzo mji mzima wa Kiomboi. Wakazi wa Kiomboi wanaishi tu kama hawana mbunge lakini wala hawana fikra za huyo Kitila. Molemo usiwe mwongo hivyo


we mwanachadema kweli?? uko wapi mwenzangu mi niko shelui ngome ya ushindi... hata wanaCCM wenyewe viongozi wanamzungumzia Mkumbo hawatoki mdomoni... Muulize DC kwanini Katibu tarafa wamemwambia hawamtaki Mheshimiwa wao Mwigulu kwenye chaguzi za viongozi wa vijiji kwenye kikao chao cha juzi?? Nchemba ni msomi lakini Mkumbo ndiye aliyemfundisha chuo... anayeonekana zaidi ni mwalimu ndo Mpango mzima....
 
Mwigulu ni gaidi namba moja Nchi hii,wekeni namba za akaunti ili tuchangie OMI.
 
ktk kilio cha ccm siku ya mwisho wa anguko lao ktk watu ambao hawatasahaulika ni huyu kada maarufu wa ccm Mwigulu Mchemba, ccm siku zote wameshindwa kutofautisha wanasiasa na waropokaji watanzania wengi tukiona watu wanajua kuongea kwa kupaza sauti wanaropoka ropoka tunasema jamaa anajua siasa kumbe ni mazuzu unajua nchi yetu ilipofika huitaji kumwambia mtu ona ile njano wkt yeye anaona ni blue. nimekuwa nikimfuatilia sana huyu mh tokea amepewa uongozi ndani ya ccm nikagundua kuwa ccm siraha zilikuwa zimeisha wakaamua watumie viboko yaani jama hata hajionji bungeni wenzake chadema anaoshindana nao wanajituma kujenga hoja za kujisadikisha kwa watanzania yeye anaropoka ropoka kujisadikisha kwa viongozi wa chama
 
Kitira mkumbo ni mhadhiri wa chuo kikuu cha Dar es salaam na msomi makini na mpole kiasi kwamba hamna haja ya kuwa na wasiwasi nae, namwamini mi kama mwanafunzi wake aliwahi kunifundisha pale UDSM mwaka janaye uchaguzi mkuu katika jimbo la Iramba 2015.

Mwigulu Nchemba anakabiliana na Msomi aliyebobea Dr Kitila Mkumbo ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA.

Pia wafuasi wa CHADEMA wameapa kuhakikisha CHADEMA inazoa viti vyote vya udiwani Iramba Magharibi ili kumuonyesha ni nini maana ya nguvu ya umma.

Katika mahojiano na wafuasi kadhaa wa CHADEMA wa mikoa ya Mara,Kagera na Mwanza wameutaka uongozi wa CHADEMA kuanzisha Akaunti maalum ambayo itachangiwa na wanachama kuhakikisha Mwigulu harudi bungeni.

Wanachama hao wamesema chuki ya Mwigulu dhidi ya Chadema hailezeki na ameapa kutumia njia zozote kuiangamiza CHADEMA.Wamesema hata awapo bungeni hatetei chochote wanaIramba zaidi ya kutukana na kukashifu viongozi wa CHADEMA.

Hii itakuwa ni Operesheni Ondoa Mwigulu Iramba(OMI) walisema wafu
 
Nadhani ni kwa sababu ya siasa zake zenye staha. Sijawahi kusikia Nahodha akitoa majibu ya hovyo wala lugha chafu hususani bungeni kama wanavyofanya akina Nchimbi, Wasira, Lukuvi etc.

Asante kwa kuniondolea ka -ukungu juu ya nahodha!!
 
Tunawaombeni wana Iramba fungueni Account haraka na jina ipewe ondoa mwigulu iramba (OMI) kama alivyo sema mheshimiwa mmoja hapo
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom