Safi sana Mwigulu kwa kazi nzuri ya ku-update itikadi ya chama cha mapinduzi, kwa ufupi ni kwamba CCM inakubalika na watanzania wengi na kama mfumo wa vyama vingi ulivyo anaependwa na wengi anachukua dola, haijalishi walioshindwa kama itawauma sana rohoni au watakubali kimya kimya, CCM itaongoza Tanzania kwa sababu ya kuaminiwa na watanzania walio wengi kuwa na viongozi waadilifu, wanyenyekevu na wenye uzalendo. Hiyo ni imani ambayo vyama pinzani hawawezi kuipata kwa hali na mali, hata wakitumia matusi, maandamo na fujo hawawezi kuipata. Maeneo ninayoishi watu walimpa Mhe.Mnyika kura kwa kuwa CCM alisimamishwa mtu ambae hakuwa na sifa tajwa hapo, ila naamini kwa ubovu wa utekelezaji wa ahadi za Mhe. Mnyika jimbo la ubungo halipati aendelee na uongozi ndani ya chama chake lakini sio ubungo, wananchi tunachukizwa na kususa kwa kiongozi huyu na kutoka nje ya ukumbi wa bunge bila kuwa na sababu za msingi, nidhamu na kauli mbovu za kiongozi huyu Mhe. Mnyika kumempotezea mvuto kisiasa, WATU TUNAANGALIA WATU SIO UCHAMA.