Mwezi mmoja ni wa dalali, madalali hii tabia mmeitoa wapi?

Asante sana kwa ushauri murua
 
Naona mmekutana wazurumati mnatujadili madalali. Katika watu wanaoongoza kwakuzurumiwa pesa nisisi madalali, jitu mnakubaliana vizuri ila sumu likimjua mwenye nyumba2 kosa lajinai linajifanya kama vile halikujui tena.

Acheni hizo jamani
 
ukienda kichwakichwa unakula za mbavu
 
Duuuuhh akikugundua atakuloga
 
Kumbe!
 
mimi nilichofanya wakati ananitembeza kwenye nyumba mbali mbali,namuandalia posho ya usumbufu.wengi huwa ni 10,hii mara zote ni kabla ya nyumba kupatikana,yaani akuzururishe tu.

Sasa hizo nyumba unazoonyeshwa unazikataa zote.halafu baadae unarudi kwa uliyoielewa.unaita faza house.*Mzee kodi hii hapa unaandika mkataba au mpaka umuone dalali wako hapa???mzee na usawa huu wa kusikilizia wateja lazima alete makaratasi.yule dalali akija.ni kavu moja tu,kwamba that day mlimalizana.over.
 
Ni bora ikabaki hivihivi isije ikafika siku eti dalali alipe kodi, cha moto tutakuona. Kadiri matumizi ya smart phone yanavyoongezeka itafika wakati itabidi hawa jamaa wakatafute kazi nyingine maana mwenye nyumba na mpangaji watakutana mtandaoni.
 
Kupangisha nyumba ni biashara, kwa hiyo mwenye nyumba kwa vile hawezi au hataki kutafuta wateja mwenyewe basi yeye ndiye anatakiwa kumpatia commission dalali, na siyo mteja nd'o awe mtoa commission. Hivyo mwaka wa kwanza mwenye nyumba anapaswa kupokea pesa ya miezi 11 (japo sijaelewa uhalali wa dalali kulipwa pesa ya mwezi mmoja ni katika mkataba wa muda gani).
Tatizo mnafanya mambo kwa mazoea hata pale inapoonekana kabisa kuwa jambo fulani si sawa kabisa.
 
Kuna mtaa mmoja dalali mmoja wanamwita mngoni ukimzingua anakuja kukata gogo kila siku mpaka umpe hela yake hata ubadili kitasa cha geti.Hata kama fensi ina umeme asubuhi ukiamka unakuta nnya mlangoni.
Dawa yake mbwa tuu, nina bonge la mbwa huwa halipigi kelele... Ukilifungua usiku linatafuta sehemu linabana kimyaa.... Likisikia kitu au mtu linanyata kimya kimya utashangaa nyama ya tako imeenda... Ukisema ooh unakuja na nyama yako, hali wala hagusi....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…