Mwanamayu
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 11,349
- 6,476
Jijini Dar es Salaam, mwezi wa nne mwaka huu Padri wa Shirika la White Fathers, Kanisa Katoliki, alitoweka na mwili wake kukutwa kwenye tank la maji akiwa hana uhai.
Padri huyo alikuwa ni Raia wa Zambia. Jijini Mbeya, mwezi huu Padri mwingine wa shirika hilo hilo kutokea Malawi alitoweka na siku ya pili kukutwa amekufa kwa kukatwa shingo na mwili wake kuviringishwa kwenye blanketi.
Maswali: 1. kwa nini vifo hivi vya kutatanisha vinatokea kwa Mapadri wa shirika la White Fathers? 2. Kwa nini kwa Mapadre wa White Fathers wa kutoka nje ya nchi?
Je, yaweza kuwa wao kwa wao? Parokiani kwetu tumeambiwa sasa kuna CCTV cameras, je ni kuongeza usalama juu ya matukio haya, je zitasaidia?
Je, wahusika waweza kuwa ni wa kutoka kwenye nchi zao kama inavyodhaniwa? Kama ni watu kutoka nje ya nchi, je nchi yetu ina ulinzi wa kutosha? Mpaka haya yote yanatokea, usalama wa Taifa wako wapi?
Vyanzo: Mwili wa padre waokotwa Mbeya
VIDEO-Polisi yachunguza chanzo cha mauaji Padre Mbeya
Padri huyo alikuwa ni Raia wa Zambia. Jijini Mbeya, mwezi huu Padri mwingine wa shirika hilo hilo kutokea Malawi alitoweka na siku ya pili kukutwa amekufa kwa kukatwa shingo na mwili wake kuviringishwa kwenye blanketi.
Maswali: 1. kwa nini vifo hivi vya kutatanisha vinatokea kwa Mapadri wa shirika la White Fathers? 2. Kwa nini kwa Mapadre wa White Fathers wa kutoka nje ya nchi?
Je, yaweza kuwa wao kwa wao? Parokiani kwetu tumeambiwa sasa kuna CCTV cameras, je ni kuongeza usalama juu ya matukio haya, je zitasaidia?
Je, wahusika waweza kuwa ni wa kutoka kwenye nchi zao kama inavyodhaniwa? Kama ni watu kutoka nje ya nchi, je nchi yetu ina ulinzi wa kutosha? Mpaka haya yote yanatokea, usalama wa Taifa wako wapi?
Vyanzo: Mwili wa padre waokotwa Mbeya
VIDEO-Polisi yachunguza chanzo cha mauaji Padre Mbeya