Mwenyekiti wangu Magufuli, usitubu!

Mwenyekiti wangu Magufuli, usitubu!

Kwa kutuma watu wasiojulikana ili wamuue Lisu pia anatakiwa akatubu maana hats Mungu aliweza muokoa Lisu
Tena hilo angetubu hadharani sio kwa uficho. Akubali kuwa Mungu kaonyesha uwezo wake
 
Askofu Zakary Kakobe mpuuze na hoja igeuze. Huna haja wala hoja ya kutubu kwa toba kwakuwa unatoa tiba kwa miiba ya Tanzania. Unatibu bila tabu yaliyokuwa majaribu mujarabu kwa watanzania. Usitubu!

Usijali. Tunakuombea na kukujibia. Tutamjibu kwa mbwembwe kuliko kunyoa kwa wembe hadi Askofu ajione mzembe. Tutampa majibu ya mbali na karibu hadi aulaumu utaratibu uliomsibu. Usitubu!

Jijenge, jitenge na waingize mkenge. Jifagilie, jiandalie na jifurahie. Ni wakati wako chamani na Serikalini. Kataza hata kwa kuliza fujo za hovyo za mikutano na kuhutubia kwa kujielezea. Huna haja ya kutubu!

Kula nanasi kunahitaji nafasi. Unayo nafasi bila kufosi ya kujinafasi bila wasiwasi na kutajwatajwa wewe tu. Hutubia, tumbua, kemea, kamatia, zingatia, puuzia, koromea na kagua. Ni wewe tu, usitubu!

Demokrasia huleta ghasia. Mikutano hubadili mtazamo. Giza husaidia. Giza hulinda na kuunda. Tuache bila mikutano wala mitazamo. Tukusikie na kukufuata wewe tu. Usitubu, usijipe tabu!

Mambo ya expansion joints hayo!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (mapumzikoni Nairobi,Kenya)

Kaka una kipaji cha “MISTARI”, kinachofuata mtafute Mr.2 au Mwana FA usimame jukwaani ili KUMG’ONG’A ukiwa na maiki mkononi.
 
Nchi hii ina safari ndefu sana yan mtu ana hadi smartphone yakuingia JF lakini kashindwa kuelewa maudhui ya mleta mada jamani? Tunaenda wapi? Usikute wote hawa walioporimosha matusi ni first, second na 3rd year, wanajiita wasomi wa vyuo vikuu. Nimeumia aisee.

Hivi hawa watu hawakusoma kabisa kiswahili form one, form two?

Dah. Elimu inapaswa kupitiwa upya nchi hii

Yan wachangiaji wote karibu 10 wa kwanza wameshindwa elawa kabisa maudhui ya mada. Leo nmejua kwanini 70% ya watoto wote wanaomaliza kidato cha nne wanafeli wakati 99.9% wanafaulu darasa la saba kwenda sekondari.

Hivi watu wa hivi ukiwapa shairi la mzee Shaban Robert wanaweza lichambua kweli? Tanzania inahtaji msamaha kutoka kwa Mungu kuna sehemu tumemkosea. Ndio maana sasa hata vichaa wanaongoza nchi
Kuwa makini mkuu kumbuka humu ulijisajili kwa E mail ID hivyo usishindane na Mamlaka, Siku ukikamatwa utakuwa pèke yako, hilo neno kichaa litakugharimu sana mkuu
 
Kuwa makini mkuu kumbuka humu ulijisajili kwa E mail ID hivyo usishindane na Mamlaka, Siku ukikamatwa utakuwa pèke yako, hilo neno kichaa litakugharimu sana mkuu
Umesoma yoootee,ukaona neno kichaa tu?Weye unaonekana mlalamishi sana.Inawezekana hata ukiwa kitandani unapata "halua" huwa ni ulalamishi tu.
 
Ushauri huu ni wa kikarumanzira.
Hivi unaambiwa utubu wewe kama shetani unasema asitubu?
Hizi akili sio hata za mbayuayu ni za bundi aiseh
Wengi wetu somo la fasihi liliwapitia kushoto.tafadhali soma tena.safari hii usiwe na haraka
 
Kuwa makini mkuu kumbuka humu ulijisajili kwa E mail ID hivyo usishindane na Mamlaka, Siku ukikamatwa utakuwa pèke yako, hilo neno kichaa litakugharimu sana mkuu
Ila tunakufa mara moja tu kaka. Sasa uoga ukizidi ukombozi hautakuja
 
Askofu Zakary Kakobe mpuuze na hoja igeuze. Huna haja wala hoja ya kutubu kwa toba kwakuwa unatoa tiba kwa miiba ya Tanzania. Unatibu bila tabu yaliyokuwa majaribu mujarabu kwa watanzania. Usitubu!

Usijali. Tunakuombea na kukujibia. Tutamjibu kwa mbwembwe kuliko kunyoa kwa wembe hadi Askofu ajione mzembe. Tutampa majibu ya mbali na karibu hadi aulaumu utaratibu uliomsibu. Usitubu!

Jijenge, jitenge na waingize mkenge. Jifagilie, jiandalie na jifurahie. Ni wakati wako chamani na Serikalini. Kataza hata kwa kuliza fujo za hovyo za mikutano na kuhutubia kwa kujielezea. Huna haja ya kutubu!

Kula nanasi kunahitaji nafasi. Unayo nafasi bila kufosi ya kujinafasi bila wasiwasi na kutajwatajwa wewe tu. Hutubia, tumbua, kemea, kamatia, zingatia, puuzia, koromea na kagua. Ni wewe tu, usitubu!

Demokrasia huleta ghasia. Mikutano hubadili mtazamo. Giza husaidia. Giza hulinda na kuunda. Tuache bila mikutano wala mitazamo. Tukusikie na kukufuata wewe tu. Usitubu, usijipe tabu!

Mambo ya expansion joints hayo!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (mapumzikoni Nairobi,Kenya)
Watanzania wengi wanalala nje ya nyumba zao,watz wengi hawana kazi,watz wengi wanazidi kulalamika hali ngumu,wanalalamika ndugu zao kupotezwa,hali hii haiwezi acha mtu salama,kutubu ni mhm mbaya zaidi mhusika ni muongo anachosema si kile anachomaanisha,
 
Ushauri huu ni wa kikarumanzira.
Hivi unaambiwa utubu wewe kama shetani unasema asitubu?
Hizi akili sio hata za mbayuayu ni za bundi aiseh
Wewe umekurupuka na kupotea njia ha ha ha.
 
Hata kwa ibilisi ukikosea masharti badala ya Kuku mwekundu unaleta mweusi ni lazima utubu
 
Hata Mimi Naunga mkono Asitubu kwa Matakwa yake... Ili Ule Moto upate Kuni za Kutosha.... USITUBU WALA KUJIREKEBISHA YAANI KAZA KWA SANA TU KAMA NEBUKDNEZA! Hapa kazi tu.
 
Hivi hao wasiomwelewa @VUTA-NIKUVUTE hapa jamvini ni wageni nini? Maana mleta uzi ni mwanaCCM pekee hapa JF huwa anaandika nyuzi zinazokosoa chama chake bila unafiki. Na hilo bandiko aliloweka lisomeni vizuri maana hapa amemkejeli mkulu.
 
Vuta nikuvute naomba kuwajua walimu wako wa fasihi maanake hii sanaa uliyoitumia hapa yatubidi wengine kurejea darasani ili tukuelewe! Very satirical! Lumumbani watapata taabu sana kukuelewa! Hongera kwa kulitendea haki somo lako la lugha!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom