Mwenyekiti wangu Magufuli, usitubu!

Mwenyekiti wangu Magufuli, usitubu!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Askofu Zakary Kakobe mpuuze na hoja igeuze. Huna haja wala hoja ya kutubu kwa toba kwakuwa unatoa tiba kwa miiba ya Tanzania. Unatibu bila tabu yaliyokuwa majaribu mujarabu kwa watanzania. Usitubu!

Usijali. Tunakuombea na kukujibia. Tutamjibu kwa mbwembwe kuliko kunyoa kwa wembe hadi Askofu ajione mzembe. Tutampa majibu ya mbali na karibu hadi aulaumu utaratibu uliomsibu. Usitubu!

Jijenge, jitenge na waingize mkenge. Jifagilie, jiandalie na jifurahie. Ni wakati wako chamani na Serikalini. Kataza hata kwa kuliza fujo za hovyo za mikutano na kuhutubia kwa kujielezea. Huna haja ya kutubu!

Kula nanasi kunahitaji nafasi. Unayo nafasi bila kufosi ya kujinafasi bila wasiwasi na kutajwatajwa wewe tu. Hutubia, tumbua, kemea, kamatia, zingatia, puuzia, koromea na kagua. Ni wewe tu, usitubu!

Demokrasia huleta ghasia. Mikutano hubadili mtazamo. Giza husaidia. Giza hulinda na kuunda. Tuache bila mikutano wala mitazamo. Tukusikie na kukufuata wewe tu. Usitubu, usijipe tabu!

Mambo ya expansion joints hayo!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (mapumzikoni Nairobi,Kenya)
 
Naona wewe unataka kumuingiza "mkenge" Mwenyekiti wako!

Unamshauri asitubu??

Akianza "kuharibikiwa" usije ukaturudia sisi tena!
 
Inapaswa ajiulize Mara mbili wapi kakosea.
Ikibidi amuite baba askofu amueleze atubu kwa lipi.
 
Kamwambie Babako atubu kwanza kwa kukuzaa!
Naona sasa laana ishaanza kuwapata.....

Kwa jinsi mnavyoporomosha matusi, nadhani kutokana na ukaidi wenu wa kutotaka kutubu, naona sasa laana ishaanza kuwatafuna!
 
Itakuwa Kakobe hakumsikiliza Mh Magu siku ya uhuru pale Dodoma.
Magufuli alisema kuwa hata yeye huwa anatubu na anamwombaga Mungu amsamehe!
Kwa hiyo Kakobe amemshauri Raisi afanye kitu ambacho kimsingi huwa anakifanya... Ushauri wa Kakobe ni mzuri lakini umekuja kwa kuchelewa.
 
Naona sasa laana ishaanza kuwapata.....

Kwa jinsi mnavyoporomosha matusi, nadhani kutokana na ukaidi wenu wa kutotaka kutubu, naona sasa laana ishaanza kuwatafuna!
Nashangaa wakati Magufuli anapenda kusema yeye ni Mpenzi wa Mungu kwa kuwa anasema kweli, mashabiki wake huwa hawaupendi ukweli unaosemwa na wengine. Hivi kutenda dhambi na kutubu lipi ni jambo jema mbele ya Mungu aliye hai?
 
Kwi kwi kwi kwi kwi mie nimekusoma Mkuu.

Askofu Zakary Kakobe mpuuze na hoja igeuze. Huna haja wala hoja ya kutubu kwa toba kwakuwa unatoa tiba kwa miiba ya Tanzania. Unatibu bila tabu yaliyokuwa majaribu mujarabu kwa watanzania. Usitubu!

Usijali. Tunakuombea na kukujibia. Tutamjibu kwa mbwembwe kuliko kunyoa kwa wembe hadi Askofu ajione mzembe. Tutampa majibu ya mbali na karibu hadi aulaumu utaratibu uliomsibu. Usitubu!

Jijenge, jitenge na waingize mkenge. Jifagilie, jiandalie na jifurahie. Ni wakati wako chamani na Serikalini. Kataza hata kwa kuliza fujo za hovyo za mikutano na kuhutubia kwa kujielezea. Huna haja ya kutubu!

Kula nanasi kunahitaji nafasi. Unayo nafasi bila kufosi ya kujinafasi bila wasiwasi na kutajwatajwa wewe tu. Hutubia, tumbua, kemea, kamatia, zingatia, puuzia, koromea na kagua. Ni wewe tu, usitubu!

Demokrasia huleta ghasia. Mikutano hubadili mtazamo. Giza husaidia. Giza hulinda na kuunda. Tuache bila mikutano wala mitazamo. Tukusikie na kukufuata wewe tu. Usitubu, usijipe tabu!

Mambo ya expansion joints hayo!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (mapumzikoni Nairobi,Kenya)
 
Kwa hiyo Kakobe amemshauri Raisi afanye kitu ambacho kimsingi huwa anakifanya... Ushauri wa Kakobe ni mzuri lakini umekuja kwa kuchelewa.
Kama ni jambo ambalo huwa analifanya hii taharuki inayoonekana toka kwa wana CCM inatoka wapi tena. Jee huwa anatubu kwa hayo yaliyohainishwa na Askofu Kakobe?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hivi kutubu mpaka ushurutishwe...? kakobe naye akili zimeanza kumruka...apleke stress zake huko..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom