Mwenyekiti wa CCM Geita: Ni zamu ya kanda ya ziwa kutoa rais

mcfm40

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
4,452
3,150
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Geita, Joseph Msukuma amesema ana siri kubwa ya Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kuhamia Chadema na kupewa nafasi ya kugombea urais akiwakilisha vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Aliwataka wananchi kumpuuza mgombea huyo wa Ukawa na badala yake wananchi waelekeze nguvu zao kumchagua mgombea urais wa CCM, Dk. John Magufuli huku akisisitiza kuwa ni muda wa Kanda ya Ziwa kumtoa rais.
Matata

Aliyewahi kuwa Meya wa Jiji la Mwanza kupitia Chadema, Henry Matata naye ametoboa siri baada ya kudai alijiunga na chama hicho akiwa pandikizi kutoka CCM na kwamba alichokipata kinatosha.

"Mimi nilikuwa pandikizi wa CCM ndani ya Chadema, baada ya kuona Mbowe natekeleza Ilani ya CCM katika kipindi changu cha Uongozi wakanifukuza," alidai Matata.

Aliongeza kuwa akiwa Chadema amekaa humo na kujua matatizo na siri zote za chama hicho pamoja na matatizo yote ya Mbowe.

Hata hivyo, aliwataka wanachama wa CCM Wilaya ya Geita ambao bado wamegawanyika kutokana na makovu ya uchaguzi wa kura za maoni kuvunja makambi ili kujihakikishia ushindi katika jimbo hilo la Geita.


Source: Jambo leo
NB. Nilikuwa nalinganisha tu maneno ya Nape leo kumtuhumu Lowasa kutumia udini, je hapo kwenye bold mwenyeketi wa ccm hajatumia ukanda kumnadi mgombea wake? je hili ni sawa kwa Nape lakini la Lowasa ndio kosa? Nasema hvi kwa sababu simjamsikia kiongozi yeyyote wa ccm akimkemea msukuma. je magufuli achaguliwe kwa sababu anatoka kanda ya ziwa?
 
Kweli elimu ni muhimu sana.... Lowassa atamteuwaje Sumaye kuwa waziri Mkuu wakati Sumaye ajagombea jimbo lolote....
 
20150907211238.jpg

20150907211205.jpg

Magufuli ni chaguo la watanzania
 

Attachments

  • 11960047_771464726309178_7949217950611815340_n.jpg
    11960047_771464726309178_7949217950611815340_n.jpg
    26.2 KB · Views: 779
Kumbe Wanasumbuliwa Na Ukanda ya Ziwa; na Pia Wamegawanyika, basi shauri Lao Wafie Mbali.
 
Kweli elimu ni muhimu sana.... Lowassa atamteuwaje Sumaye kuwa waziri Mkuu wakati Sumaye ajagombea jimbo lolote....

Kama mwenyekiti wa CCM mkoa ni ngumbaru kiasi cha kutojua sifa za Waziri mkuu ni tatizo kubwa.Hii inaonyesha hii hadithi kaitunga tu kufurahisha umma.Uongo mwingine bwana,sijui anafikiri sisi ni mambumbumbu
 
Kweli elimu ni muhimu sana.... Lowassa atamteuwaje Sumaye kuwa waziri Mkuu wakati Sumaye ajagombea jimbo lolote....

Makubwa, eti huyu MSUKUMA ana siri nzito za ENL!!! Kama anasema UKANDA utamfanya amteue SUMAYE kuwa waziri mkuu wakati katiba iliyopo sasa inatamka bayana kuwa WAZIRI MKUU atatokana na wabunge wa KUCHAGULIWA.

Iweje Sumaye awe waziri mkuu. Hapo hakuna siri ila ni uropokaji tu.

Tarehe 25/10 ni mbali na yetu macho na masikio.
 
Msukuma hapa anasema wazi kwamba Magufuli achaguliwe kwa sababu anatoka kanda ya ziwa. Je huu si ubaguzi wa kikanda amabao Nape amemnukuu Nyerere leo akiukemea? mbona lionekne tu kwa lowasa? Tumchague magufuli kwa sababu ni wa kanda ya ziwa? je sisi wa kanda nyingine zamu yetu lini?
 
''zamu ya kanda ya ziwa''

what a disgrace to this poor country jamani
 
Makubwa, eti huyu MSUKUMA ana siri nzito za ENL!!! Kama anasema UKANDA utamfanya amteue SUMAYE kuwa waziri mkuu wakati katiba iliyopo sasa inatamka bayana kuwa WAZIRI MKUU atatokana na wabunge wa KUCHAGULIWA.

Iweje Sumaye awe waziri mkuu. Hapo hakuna siri ila ni uropokaji tu.

Tarehe 25/10 ni mbali na yetu macho na masikio.

hivi unamjua lowasa wewe,....huyo mmeru wa kenya hawezi kuzuiwa na katiba kufanya lolote analolitaka ikitokea kawa rais
 
Makubwa, eti huyu MSUKUMA ana siri nzito za ENL!!! Kama anasema UKANDA utamfanya amteue SUMAYE kuwa waziri mkuu wakati katiba iliyopo sasa inatamka bayana kuwa WAZIRI MKUU atatokana na wabunge wa KUCHAGULIWA.

Iweje Sumaye awe waziri mkuu. Hapo hakuna siri ila ni uropokaji tu.

Tarehe 25/10 ni mbali na yetu macho na masikio.

hivi waziri mkuu akistaafu anaweza rudia tena uwaziri mkuu?
 
Kumbe nyie ndio mnatuharibia amani sasa kanda ya ziwa ndio zamu yao maana yake nini?
 
Nipo Geita kampeni ya ukanda ndiyo inayotumiwa na ccm kama mbinu ya kuvunja nguvu kubwa ya UKAWA kanda ya ziwa. Lakin watu hawadanganyiki mpaka nyumbani kwa magufuli ni Pipoooz tu.
 
Kumbe nyie ndio mnatuharibia amani sasa kanda ya ziwa ndio zamu yao maana yake nini?

Maana yake ni Magufuli atashinda kwa kura nyingi sana na kuwa Rais wako na watanzania wote bila kumsahau huyo lowassa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom