Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 303
MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi (CCM), katika kata ya Kukirango wilayani Butiama mkoani Mara, Lucas Magweiga (43), amejiengua kwenye chama hicho na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Kufuatia hatua hiyo, Magwaiga aliamua kumnadi mgombea wa CHADEMA Issa Ihunyo Khazi kwa madai kuwa amechoshwa na vitendo vya ufisadi vilivyofanywa na mgombea wa kiti hicho kupitia CCM Fidelis Kisuka tangu awe diwani wa kata hiyo miaka 16 iliyopita.
Akiwa amevalia mavazi ya CCM kwenye mikutano ya CHADEMA jana, iliyofanyika katika vijiji tofauti vya Kamugegi na Kyawazaru, Magwaiga ambaye alijivua cheo cha uenyekiti na uanachama wa kawaida, alisema CCM imepoteza dira na mwalekeo kwa kumteua tena Kisuka kuwania nafasi hiyo kwa kipindi kingine cha miaka minne kutokana na fedha zake.
"Huyu mtu hakubaliki hata kidogo, lakini amepitishwa kutokana na fedha zake, CCM imepoteza mwelekeo…siwezi kuendelea kubaki kwenye chama hiki hata kwa dawa," alisema Magwaiga.
Sababu kubwa ya kumpigia debe mgombea wa CHADEMA inatokana na kutambua uwezo wake na umakini na kuwa mwenye nia ya dhati ya kuleta maendeleo katika kata hiyo.
Akihutubia mamia ya wananchi wa vijiji hivyo, mwenyekiti huyo maarufu kwa jina la ‘Kichomi' aliwaomba wana CCM waungane na kumchagua mgombea wa CHADEMA kwa ajili ya kupata ukombozi mpya.
"Mimi siogopi kuulizwa wala kunyang'anywa kadi ya CCM, lakini ukweli utabaki pale pale kuwa chama hiki kimepoteza mwelekeo… ukweli unabaki pale pale kuwa CHADEMA imeleta mgombea makini ambaye ni chaguo la wana Kukirango," alisema Khazi.
Pamoja na Kisuka kuwa diwani kwa kipindi chote na kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri kwa kipindi cha miaka 10, wananchi wake wameendelea kuwa maskini wa kutupwa kutokana na kutafuta fedha nyingi za miradi mbalimbali kutoka kwa wafadhili.
Chanzo: Tanzania Daima
Kufuatia hatua hiyo, Magwaiga aliamua kumnadi mgombea wa CHADEMA Issa Ihunyo Khazi kwa madai kuwa amechoshwa na vitendo vya ufisadi vilivyofanywa na mgombea wa kiti hicho kupitia CCM Fidelis Kisuka tangu awe diwani wa kata hiyo miaka 16 iliyopita.
Akiwa amevalia mavazi ya CCM kwenye mikutano ya CHADEMA jana, iliyofanyika katika vijiji tofauti vya Kamugegi na Kyawazaru, Magwaiga ambaye alijivua cheo cha uenyekiti na uanachama wa kawaida, alisema CCM imepoteza dira na mwalekeo kwa kumteua tena Kisuka kuwania nafasi hiyo kwa kipindi kingine cha miaka minne kutokana na fedha zake.
"Huyu mtu hakubaliki hata kidogo, lakini amepitishwa kutokana na fedha zake, CCM imepoteza mwelekeo…siwezi kuendelea kubaki kwenye chama hiki hata kwa dawa," alisema Magwaiga.
Sababu kubwa ya kumpigia debe mgombea wa CHADEMA inatokana na kutambua uwezo wake na umakini na kuwa mwenye nia ya dhati ya kuleta maendeleo katika kata hiyo.
Akihutubia mamia ya wananchi wa vijiji hivyo, mwenyekiti huyo maarufu kwa jina la ‘Kichomi' aliwaomba wana CCM waungane na kumchagua mgombea wa CHADEMA kwa ajili ya kupata ukombozi mpya.
"Mimi siogopi kuulizwa wala kunyang'anywa kadi ya CCM, lakini ukweli utabaki pale pale kuwa chama hiki kimepoteza mwelekeo… ukweli unabaki pale pale kuwa CHADEMA imeleta mgombea makini ambaye ni chaguo la wana Kukirango," alisema Khazi.
Pamoja na Kisuka kuwa diwani kwa kipindi chote na kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri kwa kipindi cha miaka 10, wananchi wake wameendelea kuwa maskini wa kutupwa kutokana na kutafuta fedha nyingi za miradi mbalimbali kutoka kwa wafadhili.
Chanzo: Tanzania Daima