Elections 2010 Mwenyekiti UWT: CCM majungu yatatumaliza

Kaa la Moto

JF-Expert Member
Apr 24, 2008
7,903
1,053
Mwenyekiti UWT: CCM majungu yatatumaliza
Monday, 04 October 2010 18:45

Mwandishi Wetu, Bukoba

MWENYEKITI wa Umoja wa wananwake (UWT) Bukoba Mjini , Mulungi Kichwabuta,jana aliibuka mjini hapa na kuwataka wanaCCM kupigania ushindi wa chama chao badala ya kuanzisha majungu katika kipindi hiki cha Kampeni.

Mulungi alisema hayo kufuatia taarifa iliyotolewa kwenye kikao cha Mama Salma Kikwete na Katibu wa CCM kwamba mwenyekiti huyo anashiriki kuivuruga CCM.

Akizungumza jana mjini hapa Mulungi alisema kuwa wakati wanachama na viongozi wa chama hicho wakipambana kuhakikisha ushindi unapatikana katika chama chao kuna baadhi ya watu wameanza kuchafuana hali inayoweza kuwapatia mwanya wapinzani.

“Ni kweli wametoa shutuma kuhusu mimi kwamba nampigia kampeni Mstahiki Meya, lakini ninachoamini ni kwamba wakati huu ni kuhakikisha ushindi wa mbunge, diwani na rais, mambo ya umeya ni baada ya ushindi” alisema.

Mulungi alisema kuna baadhi ya watu ambao wamekuwa wakichanganya wapigakura kwa kuanza mikakati ya umeya wakati bado hawajapata hata udiwani kitu ambacho kinaweza kutoa mwanya kwa wapinzani.

“Nadhani Mzee Ruhangisa ni mgombea wa CCM katika kata ya Kitendagulo, hivyo nguvu za kumtetea apate ushindi ni wajibu wetu sote baada ya uchaguzi wakipatikana madiwani watawajibika kuchagua meya”.

Naye muasisi wa CCM, na mkazi wa Kitendagulu, Mzee Kassim Kalwandira alisema jana kuwa amepata taarifa za mvutano uliotokea katika kikao hicho cha CCM , mbele ya mke wa rais mama Salma Kikwete, lakini alisikitika kwa kuwa Mzee Ruhangisa hayupo nchini kufafanua.

“Nimeyasikia hayo na hayajaanza leo, lakini kikubwa ni kujua kuwa kuna watu walianza zamani kutaka Ruhangisa asirejee katika udiwani, lakini walishindwa kwa kuwa wananchi bado wanampenda na kumkubali” alisema Mzee Kalwandira ambaye alikuwa Mwenyekiti wa halmashauri ya Bukoba.

Alisema kuna baadhi ya watu ambao bado wana vidonda vya kura za maoni ambao walikuwa wanatarajia kuwaangusha baadhi ya wagombea, lakini waliposhindwa wamekuwa wakihaha kutafuta jinsi ya kuharibu.

“Kuna maneno kuwa watu walikuwa wamechangiwa pesa na wafanyabiashara na wanasiasa ili kuwaangusha watu kama Ruhangisa, lakini wanashindwa kwa kuwa watu wana imani nao”
 
Mwenyekiti UWT: CCM majungu yatatumaliza
Monday, 04 October 2010 18:45

Mwandishi Wetu, Bukoba

MWENYEKITI wa Umoja wa wananwake (UWT) Bukoba Mjini , Mulungi Kichwabuta,jana aliibuka mjini hapa na kuwataka wanaCCM kupigania ushindi wa chama chao badala ya kuanzisha majungu katika kipindi hiki cha Kampeni.

Mulungi alisema hayo kufuatia taarifa iliyotolewa kwenye kikao cha Mama Salma Kikwete na Katibu wa CCM kwamba mwenyekiti huyo anashiriki kuivuruga CCM.

Akizungumza jana mjini hapa Mulungi alisema kuwa wakati wanachama na viongozi wa chama hicho wakipambana kuhakikisha ushindi unapatikana katika chama chao kuna baadhi ya watu wameanza kuchafuana hali inayoweza kuwapatia mwanya wapinzani.

"Ni kweli wametoa shutuma kuhusu mimi kwamba nampigia kampeni Mstahiki Meya, lakini ninachoamini ni kwamba wakati huu ni kuhakikisha ushindi wa mbunge, diwani na rais, mambo ya umeya ni baada ya ushindi" alisema.

Mulungi alisema kuna baadhi ya watu ambao wamekuwa wakichanganya wapigakura kwa kuanza mikakati ya umeya wakati bado hawajapata hata udiwani kitu ambacho kinaweza kutoa mwanya kwa wapinzani.

"Nadhani Mzee Ruhangisa ni mgombea wa CCM katika kata ya Kitendagulo, hivyo nguvu za kumtetea apate ushindi ni wajibu wetu sote baada ya uchaguzi wakipatikana madiwani watawajibika kuchagua meya".

Naye muasisi wa CCM, na mkazi wa Kitendagulu, Mzee Kassim Kalwandira alisema jana kuwa amepata taarifa za mvutano uliotokea katika kikao hicho cha CCM , mbele ya mke wa rais mama Salma Kikwete, lakini alisikitika kwa kuwa Mzee Ruhangisa hayupo nchini kufafanua.

"Nimeyasikia hayo na hayajaanza leo, lakini kikubwa ni kujua kuwa kuna watu walianza zamani kutaka Ruhangisa asirejee katika udiwani, lakini walishindwa kwa kuwa wananchi bado wanampenda na kumkubali" alisema Mzee Kalwandira ambaye alikuwa Mwenyekiti wa halmashauri ya Bukoba.

Alisema kuna baadhi ya watu ambao bado wana vidonda vya kura za maoni ambao walikuwa wanatarajia kuwaangusha baadhi ya wagombea, lakini waliposhindwa wamekuwa wakihaha kutafuta jinsi ya kuharibu.

"Kuna maneno kuwa watu walikuwa wamechangiwa pesa na wafanyabiashara na wanasiasa ili kuwaangusha watu kama Ruhangisa, lakini wanashindwa kwa kuwa watu wana imani nao"

Mkuu kwenye Red vipi hapo unamili chombo cha habari nini! au wewe mwandishi wa habari
 
Mwenyekiti UWT: CCM majungu yatatumaliza
Monday, 04 October 2010 18:45

Mwandishi Wetu, Bukoba

MWENYEKITI wa Umoja wa wananwake (UWT) Bukoba Mjini , Mulungi Kichwabuta,jana aliibuka mjini hapa na kuwataka wanaCCM kupigania ushindi wa chama chao badala ya kuanzisha majungu katika kipindi hiki cha Kampeni.

Mulungi alisema hayo kufuatia taarifa iliyotolewa kwenye kikao cha Mama Salma Kikwete na Katibu wa CCM kwamba mwenyekiti huyo anashiriki kuivuruga CCM.

Akizungumza jana mjini hapa Mulungi alisema kuwa wakati wanachama na viongozi wa chama hicho wakipambana kuhakikisha ushindi unapatikana katika chama chao kuna baadhi ya watu wameanza kuchafuana hali inayoweza kuwapatia mwanya wapinzani.

"Ni kweli wametoa shutuma kuhusu mimi kwamba nampigia kampeni Mstahiki Meya, lakini ninachoamini ni kwamba wakati huu ni kuhakikisha ushindi wa mbunge, diwani na rais, mambo ya umeya ni baada ya ushindi" alisema.

Mulungi alisema kuna baadhi ya watu ambao wamekuwa wakichanganya wapigakura kwa kuanza mikakati ya umeya wakati bado hawajapata hata udiwani kitu ambacho kinaweza kutoa mwanya kwa wapinzani.

"Nadhani Mzee Ruhangisa ni mgombea wa CCM katika kata ya Kitendagulo, hivyo nguvu za kumtetea apate ushindi ni wajibu wetu sote baada ya uchaguzi wakipatikana madiwani watawajibika kuchagua meya".

Naye muasisi wa CCM, na mkazi wa Kitendagulu, Mzee Kassim Kalwandira alisema jana kuwa amepata taarifa za mvutano uliotokea katika kikao hicho cha CCM , mbele ya mke wa rais mama Salma Kikwete, lakini alisikitika kwa kuwa Mzee Ruhangisa hayupo nchini kufafanua.

"Nimeyasikia hayo na hayajaanza leo, lakini kikubwa ni kujua kuwa kuna watu walianza zamani kutaka Ruhangisa asirejee katika udiwani, lakini walishindwa kwa kuwa wananchi bado wanampenda na kumkubali" alisema Mzee Kalwandira ambaye alikuwa Mwenyekiti wa halmashauri ya Bukoba.

Alisema kuna baadhi ya watu ambao bado wana vidonda vya kura za maoni ambao walikuwa wanatarajia kuwaangusha baadhi ya wagombea, lakini waliposhindwa wamekuwa wakihaha kutafuta jinsi ya kuharibu.

"Kuna maneno kuwa watu walikuwa wamechangiwa pesa na wafanyabiashara na wanasiasa ili kuwaangusha watu kama Ruhangisa, lakini wanashindwa kwa kuwa watu wana imani nao"

Huo ndio ujira wa kubinafsisha urais, UWT, JWTZ, Chama kuwa ni vya kifamilia!!!
 
Mkuu kwenye Red vipi hapo unamili chombo cha habari nini! au wewe mwandishi wa habari
Hii ni direct quote toka gazeti la majira mkuu. Mimi sikai Bukoba na wala sijawahi kuwa mwandishi wa habari.:A S wink:
 
Mwaka huu watatoana macho. Salma Kikwete anachezea pesa yetu tu bure hakuna atakaloweza kufanya maana wanacheka na kusema mambo yamekwisha lakini pembeni tunajua nani w kutopigiwa kura.
Kigumu chama
 
Mtaji wetu ni kura zetu.Usimpigie kura fisadi hata kama umechukua Mkwanja.Kuna watu wanapita nyumba kwa nyumba wakiwa na daftari na sh.5000 - 10,000 wanakupa wanaomba waorodheshe namba ya kadi ya kupigia kura.Hii ni usanii,kwani kwenye kupiga kura ukishapiga kura hakuna mtu anayehakiki kuona kweli jina aliloandika kura imekwenda kwa mhusika .Wadau naomba muwaelimishe wananchi kuhusu hilo,maana maeneo ya Jangwani hili limetokea,ilibidi nimwelimishe yule dada.Sasa hapa ni Dar mambo ndio hivi,tuelimishe wasio na uelewa wa kura.
 
Back
Top Bottom