Kaa la Moto
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 7,903
- 1,053
Mwenyekiti UWT: CCM majungu yatatumaliza
Monday, 04 October 2010 18:45
Mwandishi Wetu, Bukoba
MWENYEKITI wa Umoja wa wananwake (UWT) Bukoba Mjini , Mulungi Kichwabuta,jana aliibuka mjini hapa na kuwataka wanaCCM kupigania ushindi wa chama chao badala ya kuanzisha majungu katika kipindi hiki cha Kampeni.
Mulungi alisema hayo kufuatia taarifa iliyotolewa kwenye kikao cha Mama Salma Kikwete na Katibu wa CCM kwamba mwenyekiti huyo anashiriki kuivuruga CCM.
Akizungumza jana mjini hapa Mulungi alisema kuwa wakati wanachama na viongozi wa chama hicho wakipambana kuhakikisha ushindi unapatikana katika chama chao kuna baadhi ya watu wameanza kuchafuana hali inayoweza kuwapatia mwanya wapinzani.
Ni kweli wametoa shutuma kuhusu mimi kwamba nampigia kampeni Mstahiki Meya, lakini ninachoamini ni kwamba wakati huu ni kuhakikisha ushindi wa mbunge, diwani na rais, mambo ya umeya ni baada ya ushindi alisema.
Mulungi alisema kuna baadhi ya watu ambao wamekuwa wakichanganya wapigakura kwa kuanza mikakati ya umeya wakati bado hawajapata hata udiwani kitu ambacho kinaweza kutoa mwanya kwa wapinzani.
Nadhani Mzee Ruhangisa ni mgombea wa CCM katika kata ya Kitendagulo, hivyo nguvu za kumtetea apate ushindi ni wajibu wetu sote baada ya uchaguzi wakipatikana madiwani watawajibika kuchagua meya.
Naye muasisi wa CCM, na mkazi wa Kitendagulu, Mzee Kassim Kalwandira alisema jana kuwa amepata taarifa za mvutano uliotokea katika kikao hicho cha CCM , mbele ya mke wa rais mama Salma Kikwete, lakini alisikitika kwa kuwa Mzee Ruhangisa hayupo nchini kufafanua.
Nimeyasikia hayo na hayajaanza leo, lakini kikubwa ni kujua kuwa kuna watu walianza zamani kutaka Ruhangisa asirejee katika udiwani, lakini walishindwa kwa kuwa wananchi bado wanampenda na kumkubali alisema Mzee Kalwandira ambaye alikuwa Mwenyekiti wa halmashauri ya Bukoba.
Alisema kuna baadhi ya watu ambao bado wana vidonda vya kura za maoni ambao walikuwa wanatarajia kuwaangusha baadhi ya wagombea, lakini waliposhindwa wamekuwa wakihaha kutafuta jinsi ya kuharibu.
Kuna maneno kuwa watu walikuwa wamechangiwa pesa na wafanyabiashara na wanasiasa ili kuwaangusha watu kama Ruhangisa, lakini wanashindwa kwa kuwa watu wana imani nao
Monday, 04 October 2010 18:45
Mwandishi Wetu, Bukoba
MWENYEKITI wa Umoja wa wananwake (UWT) Bukoba Mjini , Mulungi Kichwabuta,jana aliibuka mjini hapa na kuwataka wanaCCM kupigania ushindi wa chama chao badala ya kuanzisha majungu katika kipindi hiki cha Kampeni.
Mulungi alisema hayo kufuatia taarifa iliyotolewa kwenye kikao cha Mama Salma Kikwete na Katibu wa CCM kwamba mwenyekiti huyo anashiriki kuivuruga CCM.
Akizungumza jana mjini hapa Mulungi alisema kuwa wakati wanachama na viongozi wa chama hicho wakipambana kuhakikisha ushindi unapatikana katika chama chao kuna baadhi ya watu wameanza kuchafuana hali inayoweza kuwapatia mwanya wapinzani.
Ni kweli wametoa shutuma kuhusu mimi kwamba nampigia kampeni Mstahiki Meya, lakini ninachoamini ni kwamba wakati huu ni kuhakikisha ushindi wa mbunge, diwani na rais, mambo ya umeya ni baada ya ushindi alisema.
Mulungi alisema kuna baadhi ya watu ambao wamekuwa wakichanganya wapigakura kwa kuanza mikakati ya umeya wakati bado hawajapata hata udiwani kitu ambacho kinaweza kutoa mwanya kwa wapinzani.
Nadhani Mzee Ruhangisa ni mgombea wa CCM katika kata ya Kitendagulo, hivyo nguvu za kumtetea apate ushindi ni wajibu wetu sote baada ya uchaguzi wakipatikana madiwani watawajibika kuchagua meya.
Naye muasisi wa CCM, na mkazi wa Kitendagulu, Mzee Kassim Kalwandira alisema jana kuwa amepata taarifa za mvutano uliotokea katika kikao hicho cha CCM , mbele ya mke wa rais mama Salma Kikwete, lakini alisikitika kwa kuwa Mzee Ruhangisa hayupo nchini kufafanua.
Nimeyasikia hayo na hayajaanza leo, lakini kikubwa ni kujua kuwa kuna watu walianza zamani kutaka Ruhangisa asirejee katika udiwani, lakini walishindwa kwa kuwa wananchi bado wanampenda na kumkubali alisema Mzee Kalwandira ambaye alikuwa Mwenyekiti wa halmashauri ya Bukoba.
Alisema kuna baadhi ya watu ambao bado wana vidonda vya kura za maoni ambao walikuwa wanatarajia kuwaangusha baadhi ya wagombea, lakini waliposhindwa wamekuwa wakihaha kutafuta jinsi ya kuharibu.
Kuna maneno kuwa watu walikuwa wamechangiwa pesa na wafanyabiashara na wanasiasa ili kuwaangusha watu kama Ruhangisa, lakini wanashindwa kwa kuwa watu wana imani nao