barafuyamoto
JF-Expert Member
- Jul 26, 2014
- 32,329
- 29,594
Ushahidi muulize ue mwenyewe, alisema angeweka kila kitu hadharani akala maneno yake mwenyewe.Kati ya watia nia wanaoshambuliwa zaidi kwa propaganda mfu ni Lowassa. Kuna mambo mawili yanayomfanya ashambuliwe sana. Moja, ni utajiri wake na pili, ni watendaji wa 'business as usual'!
Karibu watia nia wengi (sio wote) waliojiotokeza CCM hadi sasa wamewahi kupatwa na dhoruba za kisiasa kwa namna moja ama nyingine! Lakini hili la richmond la Lowassa limekuwa ruba! Kwa maneno mengine richmond inafanywa moja kwa moja kama vile ni mradi wa Lowassa, kiasi kwamba Lowassa anapachikwa jina la fisadi japo hakuna ushahidi wowote ulio dhahiri!
Mwenye ushahidi wowote ule wa uhusika wa Lowassa kwenye ufisadi wowote ule hapa nchini auweke hadharani ili tukate mizizi ya fitna!