Mwenye notes za lugha ya kifaransa

Mwenye notes za lugha ya kifaransa

L'AMOUR

Senior Member
Joined
Mar 8, 2011
Posts
111
Reaction score
24
Wana JF naomba msaada wa mtu mwenye notes za kifaransa hasa kuanzia intermediate level ili niweze kujiendeleza. Pia nakaribisha ushauri wowote utakaonisaidia katika kujiendeleza katika lugha hii. Asanteni
 
Mimi nina copy ya kitabu. Sijui utakipataje. Ni kizuri.
 
Nitashukuru kujua kama naweza kutoa kopi yake please. Labda unisadie namna ya kukipata. Asante
 
Jamani mambo ya elimu hayana mzaha niko Dar, Ukonga Mombasa kama nitasaidiwa nitashukuru nimeshafanya mitihani ya awali na kwa sasa nataka nijiendeleze zaidi. Thanks Gobegobe limocha nimeiona na kujisajiri ina msaada mkubwa. Ila pia nikiwa na hard copy pia ni nzuri kwani sio kila wakati ninakuwa kwenye computer. Hard copy itanisaidia sana katika kujisomea wakati wowote maana notes kwa advanced french hazipatikani kwa urahisi. Thanks kwa wote mnaoshauri vizuri Mungu awabariki.
 
Ushauri wangu kwa kujifunza lugha ya kigeni ni mazoezi ya kusoma na kusema (ningelikwambia kuzungumza lakini kwa kwetu ni shida kupata watu wa kuzungumza nao.

Kwa uzoefu kusoma vitabu itakusaidia sana kujua sarufi na kupasi mitihani, lakini ili uweze kuzungumza fanya yafuatayo:
1. Soma vitabu, magazeti au maandishi yoyote katika lugha ya kifaransa. Si lazima uelewe kila unachokisoma. Lengo ni kuuzowesha ulimi wako kutamka kwa haraka na kwa ufasaha.
2. Wakati wa kusoma, soma kwa sauti badala ya kusoma kimya kimya. Kusoma kwa sauti kutakurahisishia hilo hapo juu.
3. Sikiliza radio za kifaransa na iga wanavyozungumza ili kupata "tune yao".
4. Nunu kinasa sauti (kwa sasa unaweza kutumia hata simu yako) ili wakati unapokuwa unasoma kwa sauti "ujirekodi" unachosoma, baadaye jisikilize. Mwanzo mwanzo naamini hutojipenda, lakini kadiri unavyofanya mazoezi ndivyo utavyoona unapiga hatua.
Kila la heri.
 
Asante sana mammamia nashukuru kwa ushauri mzuri nitafuata mambo haya kwa kifupi nimeshafanya DELF A1,A2 na B1 lakini naona bado niko nyuma sana. Nadhani nitatafuta channel za kifaransa na magazeti ili nisome tu kama ulivyonishauri. Thank you very much
 
kunakitabu kinaitwa on y va 1-3 pamoja na cd zake vitafute,ht mm nnajifunza french,vitakusaidia..ve bok 1 +cd
 
Thanks nitafuatilia kwenye bookshops za hapa Dar
 
L'amour angalia Google language tool its a good tool you can use that for basics, I actually used that in communicating with a spanish vendor who sold the car I own today.

Pia jaribu kuwa unakiongea unajua tena "practice makes perfect" hata kama wakikucheka keep on practicing.
 
Merci beaucoup pour les information. Je vais faire comme vous m'explique. Ca aide comme ca.
 
Nonda nashukuru sana kwa hizi links, nimepitia hii ya BBC na kufurahia kwa namna inavyotoa sauti na maandishi yake. Nafikiri hii itanipa speed ya kujua haraka. Nitazipitia hizo nyingine pia nione zikoje ila kama una wazo la kujenga zaidi nitalikaribisha. Otherwise nikushukuru sana kwa hizi link tatu hapa ni kuhakikisha niko kwenye internet na nadhani nikijiunga na club ya alliance itasaidia kwenda kufanya mazoezi zaidi. Thank you very much
 
Merci beaucoup pour les information. Je vais faire comme vous m'explique. Ca aide comme ca.
Nous avons aussi une page ou on parle exclusivement en francais sur des sujets et d'autres, pour vous permettre d'ameliorer le style parle et ecrit. c'est "peut-on savoir qui sur JF parle francais", Jukwaa la lugha.
Bienvenue sur notre page francophonie JF!
 
dah na mimi ukizipata nipm ninajifunza ila sipati watu wa kuchonga nao french mpaka niende kule alliance....
 
mkuu kwa kuwa upo huko maeneo ya Mumbasa,nenda hapo shule ya sekondari air wing.uongee na mwalimu wa french atakupa msingi mzuri.anaweza hata akawa anakufundisha.uzuri wa hao wanajeshi hawana longolongo.utapata kila ukitakacho.
 
Nous avons aussi une page ou on parle exclusivement en francais sur des sujets et d'autres, pour vous permettre d'ameliorer le style parle et ecrit. c'est "peut-on savoir qui sur JF parle francais", Jukwaa la lugha.
Bienvenue sur notre page francophonie JF!

bonjour Roulette. comment retrouver la page JF parlé francais.Je suis interresé car je dois donner des cours privés à des Professionnels.je voulais savoir que la page peu aider .Merçi
 
Back
Top Bottom