Mwenye neno lolote aniambie japo kupoza akili yangu

Lakini ukweli ni kwamba watoto wanaweza kuwa mali wakitunzwa
Wasipotunzwa wanakuja kuwa mizigo na hata chanzo cha kuongezeka uhalifu
Hapa utunzwaji watoto sio tija mana fursa ni chache. Haya mambo yameelezwa na wasomi. Suluhu hapa ni kuwa na population ambayo ni CONTROLED tu. Sera inashindwa kuendana na idadi ya watu Kwa sabb ya kuzaana sana. Leo hii utasikia muhimbili haitoshi na nafasi ndogo wakati mwaka juzi ilitosha kabisa
 
Ni matumaini yangu kuwa wote ni wazima. Niende kwenye mada moja kwa Moja.

Mimi ni Kijana wa kitanzania na hivi sasa nipo chuo kikuu kimoja hapa Tanzania jijini Dar es Salaam, nachukua shahada ya kwanza ya ualimu sayansi.

Natoka katika familia ya kawaida sana yenye jumla ya watoto tisa huku mimi ni wa kwanza yaani first born.

Hali ya uchumi ya wazazi ni duni sana hadi kufika hapa kwa Kweli ni kwa neema tu, kiufupi familia na wadogo zangu nane wananitazama mimi kama mkombozi. Hali unanifanya niishi kwa msongo mkali sana wa mawazo.

Nawaza sana mwakani nitakapomaliza chuo maisha yangu yatakuwaje? Familia na wadogo zangu tawashikaje mkono? Moyo wangu una madonda mabichi sana.

Nilibahatika kupata mkopo wa elimu ya juu lakini kwa hali ya nyumbani pesa yangu ya meals and Accomodation yaan boom huwa naikata mara mbili nusu nabaki nayo nusu natuma nyumbani.

Wanabodi nahisi maneno haya hayawezi eleza nachotaka kufikisha kwenu.

Na umri mdogo lakini sonona nahisi inanitafuna. Nataman nikimbilie South Africa kujaribu bahati yangu.

Muwe na asubuhi njema, hapa nipo njiani naelekea shule maana tupo Field lakini akili haipo Sawa.
Wala usiwe na wasiwasi, hivi ndio maana halisi ya maisha yaani ku Struggle, kila mmoja unaemuona mbele yako ana yake anapitia kama wewe lakini kubwa kuwa na tumaini, wakati mzuri upo mbele, wakati huu uliopo uwe ni wa maandalizi ya wakati mzuri unaokuja.
Maisha bila ya changamoto hayajawa maisha.
 
Akapake kucha akina Leejay49 ni rahisi na Haina mtaji mkubwa ila Hela ni Nene

Mimi nikikosaga Hela za kubetia huchukua kapu langu la rangi,nazama vijijini huku Tanganyika ambako hawanifahamu,nikipiga deiwaka ya jumamosi na jumapili sikosi 100k

Kupaka kucha 2k mpaka 3k

Kubandika kucha ni kati ya 5k mpaka 10k

Malala gesti safi,nakula Milo safi na utelezi napata bila kutongoza

Ikifika Jumatatu narudi zangu kushika chaki
Sasa si hadi uwe na taaluma kidogo? Au mtu yoyote anaweza kufanya huo kazi bila kupata darasa
 
Usijiangaishe Kwa masuala ambayo yapo nje ya uwezo wako,hebu jiulize pamoja na kuwaza sanaaa kuhusu Hali ya uchumi wa familia Yako,Je Kuna mabadiliko yoyote? Jibu ni hamna. Muhimu ishi Leo maisha ni mafupi sana unapoishi Kwa stress muhimu zaidi hautaweza kumsaidia yoyote kuinuka kiuchumi kama wewe hujasimama sawa sawa,yaani inakuhitaji wewe kwanza ukae sawa kiuchumi ndipo unanze kumsaidia ndugu,jamaa. Umaskini upo na hautaweza kuumaliza kamwe pambania ndoto zako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukimaliza chuo,nenda veta kozi fupi ya ufundi yakukuweka mtaani,ukishindwa jifunze hata kupaka kucha na kubandika

Kama una kichwa kizuri ndani ya wiki moja ushajua,ukiongozana na wale chinga,na mtaji wake ni chini ya laki moja
Huu ni ushauri mzuri, anaweza hata akapangilia vizuri ratiba zake akaanza kujifunza ufundi kabla haja maliza chuo, fundi hajawahi kulala na njaa.
 
Pambana maisha ndo hayo. Kuna wenzio wanategemewa wakati hawana hata pa kupata mkopo wala nini. Usikate tamaa huenda ndo njia ya kufanikiwa hiyo.
 
Oooyaaaaa wee! Mkurugenzi una zingua! Sasa stress za nini hapo? Wew wa MUNGU, wadogo zako wa MUNGU, yeye ndo anadili na matatizo ya binadam wake! Sasa saivi una sonona toka mzaliwe mbona mnakua tu freshi? Na usipo angalia na kua makini kama uko chuo tu una sema una stress ,wadogo zako wanakupa sonona,wazazi wanataka uwashike mkono.usipo badili mtazamo hasi huo bas ukija mtaan ujue wadogo zako na wazazi wewe ndo utawapa shida maana utachanganyikiwa
 
Ni matumaini yangu kuwa wote ni wazima. Niende kwenye mada moja kwa Moja.

Mimi ni Kijana wa kitanzania na hivi sasa nipo chuo kikuu kimoja hapa Tanzania jijini Dar es Salaam, nachukua shahada ya kwanza ya ualimu sayansi.

Natoka katika familia ya kawaida sana yenye jumla ya watoto tisa huku mimi ni wa kwanza yaani first born.

Hali ya uchumi ya wazazi ni duni sana hadi kufika hapa kwa Kweli ni kwa neema tu, kiufupi familia na wadogo zangu nane wananitazama mimi kama mkombozi. Hali unanifanya niishi kwa msongo mkali sana wa mawazo.

Nawaza sana mwakani nitakapomaliza chuo maisha yangu yatakuwaje? Familia na wadogo zangu tawashikaje mkono? Moyo wangu una madonda mabichi sana.

Nilibahatika kupata mkopo wa elimu ya juu lakini kwa hali ya nyumbani pesa yangu ya meals and Accomodation yaan boom huwa naikata mara mbili nusu nabaki nayo nusu natuma nyumbani.

Wanabodi nahisi maneno haya hayawezi eleza nachotaka kufikisha kwenu.

Na umri mdogo lakini sonona nahisi inanitafuna. Nataman nikimbilie South Africa kujaribu bahati yangu.

Muwe na asubuhi njema, hapa nipo njiani naelekea shule maana tupo Field lakini akili haipo Sawa.
Yaani unajipa stress kisa watoto waliozaliwa na mtu mwingine? Come on

Ukweli ni kuwa bado wewe ni kapuku sana kuwa first born haikufanyi ubebe majukumu yasiyokuhusu jitafute wewe mwenyewe ukijipata ndiyo hangaika na hao nduguzo but mbali na hapo ipambanie future yako acha kiherehere kwenye mambo yasiyokuhusu .

Ni ushauri tu maana unajipa stress vitu vya kijingakijinga lakini kwenye orientation uliambiwa hela ya accomodation na meals ni ya kuwatumia wazazi ??

Acha ujinga stress unajitafutia ww mwenyewe kwani kabla ya kupata mkopo hao watoto na wazazi wako waliishije? Tafakari mdogo wangu .

Lakini vipi nasikia eti kipa wa Simba mbarazil haruhusiwi kucheza bongo hivi ni kweli kaka mkubwa ?

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Ni matumaini yangu kuwa wote ni wazima. Niende kwenye mada moja kwa Moja.

Mimi ni Kijana wa kitanzania na hivi sasa nipo chuo kikuu kimoja hapa Tanzania jijini Dar es Salaam, nachukua shahada ya kwanza ya ualimu sayansi.

Natoka katika familia ya kawaida sana yenye jumla ya watoto tisa huku mimi ni wa kwanza yaani first born.

Hali ya uchumi ya wazazi ni duni sana hadi kufika hapa kwa Kweli ni kwa neema tu, kiufupi familia na wadogo zangu nane wananitazama mimi kama mkombozi. Hali unanifanya niishi kwa msongo mkali sana wa mawazo.

Nawaza sana mwakani nitakapomaliza chuo maisha yangu yatakuwaje? Familia na wadogo zangu tawashikaje mkono? Moyo wangu una madonda mabichi sana.

Nilibahatika kupata mkopo wa elimu ya juu lakini kwa hali ya nyumbani pesa yangu ya meals and Accomodation yaan boom huwa naikata mara mbili nusu nabaki nayo nusu natuma nyumbani.

Wanabodi nahisi maneno haya hayawezi eleza nachotaka kufikisha kwenu.

Na umri mdogo lakini sonona nahisi inanitafuna. Nataman nikimbilie South Africa kujaribu bahati yangu.

Muwe na asubuhi njema, hapa nipo njiani naelekea shule maana tupo Field lakini akili haipo Sawa.
Usijisumbue kwa neno lolote, bali Kwa kila neno Kwa kufunga na kusali.
Haja zako na zijulikane kwa Mungu aliye hai.


Aonavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo.
Na unavyokiri ndivyo unavyopokea.
 
Ni matumaini yangu kuwa wote ni wazima. Niende kwenye mada moja kwa Moja.

Mimi ni Kijana wa kitanzania na hivi sasa nipo chuo kikuu kimoja hapa Tanzania jijini Dar es Salaam, nachukua shahada ya kwanza ya ualimu sayansi.

Natoka katika familia ya kawaida sana yenye jumla ya watoto tisa huku mimi ni wa kwanza yaani first born.

Hali ya uchumi ya wazazi ni duni sana hadi kufika hapa kwa Kweli ni kwa neema tu, kiufupi familia na wadogo zangu nane wananitazama mimi kama mkombozi. Hali unanifanya niishi kwa msongo mkali sana wa mawazo.

Nawaza sana mwakani nitakapomaliza chuo maisha yangu yatakuwaje? Familia na wadogo zangu tawashikaje mkono? Moyo wangu una madonda mabichi sana.

Nilibahatika kupata mkopo wa elimu ya juu lakini kwa hali ya nyumbani pesa yangu ya meals and Accomodation yaan boom huwa naikata mara mbili nusu nabaki nayo nusu natuma nyumbani.

Wanabodi nahisi maneno haya hayawezi eleza nachotaka kufikisha kwenu.

Na umri mdogo lakini sonona nahisi inanitafuna. Nataman nikimbilie South Africa kujaribu bahati yangu.

Muwe na asubuhi njema, hapa nipo njiani naelekea shule maana tupo Field lakini akili haipo Sawa.


Akili huwa inafikia mwisho wakati mwingine maana ina ukomo, ni logic, ndivyo ulivyoumbwa, kwa uliyoyasema nakuelewa sana.

Ila akili zinapofikia mwisho kuna matuamini, kuna Neema, ambayo inatoka na ahadi za Mungu na hizo ndo kimbilia.

Maisha utakayoishi kutoka sasa mpaka umalize chuo yataamua uendelee na sonona au uso utakate na ufanikiwe.

Mimi kama Mkristo, nikiwa na hali kama yako, tumaini langu huwa katika ukiri wa neno la Mungu tu na hivyo huona matokeo.

Imani ni jambo la Muhimu sana kwa mwanadamu, maana uwezo wake una mwisho, ila ana roho na access ya kuunganishwa na ulimwengo usio na mipaka.
 
Pambana na Hali yako Mzee baba,hao nane waliobaki waache wapambane na Hali zao Kwani ni walemavu au watoto?
Mambo ikikaa saw ndio ugeuke nyuma
 
Back
Top Bottom