MWENGE wawafanyia 'mbaya' WALIMU...

MWENGE wawafanyia 'mbaya' WALIMU...

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Kila Mwalimu mkoa wa Morogoro amekatwa sh. 3000 kuchangia mbio za Mwenge. Watumishi wengine,tena wenye kipato kikubwa,wameachwa. Kwanini walimu hufanyiwa madhila haya? Wanaonwaje?
 
Kama ni walimu waache wapgwe za macho awasikii, hawana tofauti na sikio lakufa!! kama wameshindwa kutumia umuhmu wao na wingi wao sisi tutawatetea vip? zitafidiwa kwenye SENSA na uchaguzi mkuu 2015 wakati CDM wanashika dola
 
Jamani kwa mtazamo wangu hii ndo moja ya sifa ya walimu, mkitaka wawewanakurupuka watafanya hivyo hata darasan, hao ndo wanao jenga jamii hii ya sasa ambayo ni tolerant.
 
foooolish government!

Remote, foolish government, foolish teachers, foolish Tanzanians...... all of these participate fully to make the CCM
life span longer!!!!!

They supervise election, census ...... see themselves as part of government mkuu!
 
Nimekusoma Mkuu Paul Kijoka. Lakini,hakuna walimu wapinzani wanaoweza kuanzisha vuguvugu la mabadiliko?
 
Huo mwenge kazi yake nini hasa? Moshi wake unatia mafua!
 
Kwa walimu waache tu wakatwe, tena hata zingekuwa zaidi ya hizo, ni haki yao tu. Maana hakuna watu mambumbu kama walimu Tanzania. Yaani hii ni kada ya wafanyakazi wa serikali wasiojua haki zao wala stahili zao halali. Ni watu wanaoonewa kunyanyaswa na kudharauliwa na serikali kupindukia lakini ndiyo wa kwanza pia kujipendekeza serikalini. Ukiwaambia tugome hawataki, tulikubaliana mwaka 2010, tugome kuandikisha na kusimamia uchaguzi, kuja kushitukia ndiyo kwanza baadhi ya walimu wamekwenda kuomba kabisa. Yaani walimu ni headache katika nchi hii. Acha tuumie tu, pengine siku moja tutaamka usingizini na kuelewa ni nini tunachokistahili.
 
Sababu walimu ni DHAIFU! hawajijali! Acha wakomeshwe washike adabu, walijua mashati na kanga za kijani ni bure, acha walipe sasa.

unawaonea walimu! Watu wenye mchango mkubwa katika mageuzi ni walimu! Chadema ina uhakika wa wasomi sababu ya walimu.
 
Walimu nguvu moja sauti moja
hii ndio kauli mbiu ya walimu.
Kwa sasa haina maana yoyote kwani hakuna sauti moja wala nguvu moja.
Mgomo uendelee mpaka kieleweke.
Hivi pasipo MWALIMU nini kingeendelea hapa nchini.
Mwalimu ni chanzo cha kila kitu kama Rais wabunge mawaziri madaktari na kada zingine mbalimbali.
Serikali iache manyanyaso na madharau kwa walimu!
 
Walimu wengi wanapenda sana sirikali yao ndio maana wanachanga mbio za mwenge ili mwenge wetu uwezo songa mbele. Viva ccm viva walimu. Migomo kwetu mwiko.
 
Waje Arusha na hizo sera zao waone!nyoooo!hao si wa majimbo wanaotukuza ccm?waacheni waliwe,labda watazinduka!
 
Kila Mwalimu mkoa wa Morogoro amekatwa sh. 3000 kuchangia mbio za Mwenge. Watumishi wengine,tena wenye kipato kikubwa,wameachwa. Kwanini walimu hufanyiwa madhila haya? Wanaonwaje?

walimu wakimaliza miezi mitatu bila mishahara yao kukatwa, huwa hawajisikii vizuri. huwa wanapenda sana kukatwa mishahara.
 
Back
Top Bottom