Kwanza abiria wanakata tiketi, kisha wanasubiri gari zaidi ya saa moja.
Kinachosikitisha ni kuwa baadhi ya vituo havina viti vya kupumzika abiria wala vyoo.
Yaani abiria wa mwendokasi wamekuwa kama watumwa kwani ukisha ingia kituoni huwezi kutoka kwenda kujisaidia nje ya kituo kisha urudi na kuendelea na safari yako.
Endepo ukifanya hivyo lazima ukate tena tiketi, sasa jamani mnategemea watu wajisaidie wapi ilhali wanasubiri magari muda mrefu?