Mweka hazina Iringa press club mwanahabari Vicky Macha afariki dunia ghafla!

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797

TAARIFA kutoka mkoani Iringa ambazo zimeufikia mtandao huu wawww.francisgodwin.blogspot.com asubuhi hii zinadai kuwa aliyekuwa mweka hazina wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Iringa(IPC) na mwandishi wa magazeti ya NIpashe mkoa wa Iringa Vichky Macha (pichani) amefariki dunia asubuhi hii.


Vicky Macha kabla ya kifo chake alikuwa amelazwa katika hospitali ya mkoa wa Iringa akisumbulia ugonjwa wa Maralia na kulazwa katika Hospitali ya mkoa wa Iringa kabla ya leo asubuhi hii kufariki dunia.

Vicky Macha katika uhai wake alipata kufanya kazi kwa karibu na marehemu Daudi Mwangosi ambaye alikuwa ni mwenyekiti wa (IPC) na hata siku aliyefariki dunia Vicky Macha kama mweka hazina wa IPC mara baada ya kumweleza juu ya kifo cha Mwangosi alipoteza fahamu kwa muda katika ofisi za IPC .

Hata hivyo kutokana na siku ya tukio viongozi mkuu nilikuwa ni mimi Francis Godwin ambaye nilikuwa ni naibu katibu mkuu wa IPC kwa kushirikiana na vema na Vicky tuliweza kujikaza na kuhakikisha mambo yanakwenda vema japo mara kwa mara mwenzake alikuwa akiishiwa nguvu na mimi pia nikiishiwa nguvu na kujikuta tukibembelezana na kujikaza.



Rais wa umoja wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzania (UTPC) Keneth Simbaya (kulia) akikabidhi mchango wa rambi rambi ya kifo cha Mwangosi kwa makamu mwenyekiti wa IPC Francis Godwin kutoka kwa vilabu mbali mbali vya wanabari nchini kwa ajili ya kifo hicho , katikati ni marehemu Vicky Macha akilia kwa uchungu na kushoto ni katibu mtendaji wa IPC Frank Leonard.



Taarifa zaidi tutaendelea kuwaletea hapa
jambo kwa sasa naweza kusema Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake na lihimidiwe milele

Chanzo Francis Godwin



 
Sad news.
BWANA alitoa, BWANA ametwaa, jina lake lihimidiwe.
 
Nilipita mida fulani karibu na ofisi zao nikaona baadhi ya waandishi wa habari wakiwa wamekusanyika sikujua kilichokuwa kinaendelea kumbe msiba tena poleni sana wafiwa! Mungu aipumzishe roho ya marehemu mahali pema peponi Amen.
 
Back
Top Bottom