View attachment 3355833
Mmoja wa waasisi wa Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), Eugene Kabendera leo Jumatano, Juni 4, 2025 ametangaza kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Mei 27, Kabendera alitangaz akujiondoa CHAUMMA kwa kile alichosema kuwa ni kukiukwa kwa msingi ya chama hicho, ambacho nacho kimepokea waliokuwa makada wa CHADEMA waliokuwa wameunda kundi la G55.
Kabendera ametambulishwa mbele ya waandishi wa habari na Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Bara, Aman Golugwa, makao makuu ya Chadema, Mikocheni jijini Dar es Salaam.