Mwarabu wa Dubai, Emirates National Group (ENG) wapewa kazi ya kuendesha Mabasi ya Mwendokasi

Kwa lugha nyepesi kabisa ni kwamba ''Watanzania tumeshindwa kuendesha mradi wa Mwendo kasi''

Inashangaza kiasi, inawezekanaje watu binafsi wanaweza kumiliki mabasi na kuendesha huduma za usafirishaji tena ikitumia watu wa kawaida kabisa lakini serikali na taasisi zake na wake wake wasomi wanashindwa kuendesha usafirishaji wa abiria kwenye mji mmoja, tena kwenye njia chache kati ya nyingi za mji huo.
Route:
Mbezi - Kivukoni
Mbezi - Kkoo
Mbezi - Kibaha
Mbezi- Kimara
Mbezi - Morocco
Kkoo - Morocco
Morocco - Kivukoni

Hizi route ni chini ya asilimia kumi ya route za usafirishaji wa abiria hapa Dar.

Nini tunaweza kukifanya kwa ufanisi?
Ni wizi, rushwa, soga, chuki, uongo, uzushi, ngono..............
wizi, rushwa
 
Serikali imedhamiria kusaini mkataba wa ubia na Shirika la Emirates National Group (ENG) lenye makao yake makuu Dubai ili kuendesha usafiri wa mabasi yaendayo haraka Dar (DART) awamu ya 1 mwezi ujao.

ENG chini ya Mkurugenzi Bw. Ahmed Abood Al Boasy (Pichani) inamiliki na kuendesha makampuni ambayo yanashughulika na njia zote za usafiri wa kibinafsi na wa umma, pamoja na huduma zao za ziada.

Kamishna wa Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), David Kafulila amesema kuwa ENG ilishinda zabuni hiyo.

Serikali imechukua hatua ya kukaribisha sekta binafsi kuendesha DART ili kuboresha huduma za usafiri mijini kutokana na kasi kubwa ya mabasi kuharibika, kuruka abiria kwenye stendi nyingi za mabasi mbali na vituo vikuu na mabasi mazima kubaki machache.

Mwekezaji huyo atapewa nafasi ya kupewa ruti kwenye awamu ya pili ya mradi iwapo itathibitika kuwa ameweza kuboresha huduma kwa kiasi kikubwa.

Kafulila aliongeza kuwa kuwa mwekezaji mpya anatarajiwa kuleta idadi ya kutosha ya mabasi ili kumaliza msongamano huo.

Kafulila alisema pia kuwa utiaji saini unatarajiwa kufanyika wiki mbili zijazo, huku ENG ikitarajiwa kununua mabasi na kutoa huduma za usafiri “wakati jukumu la DART litakuwa ni kusimamia mapato.”
serikali ya ccm wameshindwa kusimamia mali za umma wapishe
 
Hii nchi tuna viongozi wenye mawazo mgando sana, kwanini tunatoa kila kitu chetu kwa wageni bila kujaribu kutoa kwa sekta binafsi hasa wazawa tuwape wao wafanye kazi atleast kwa miaka mitatu mpaka mitano ili tuone ufanisi wao?

Hiyo kazi naamini kabisa wapo wenye mabasi yao ya usafiri wangepewa waifanye kwa uzuri bila kuhangaika kutafuta wageni wawekeze kwenye kila kitu, sasa tumekuwa kama taifa la mazombi lisiloweza kufanya chochote.

Hata hizo sababu alizotoa Kafulila za mabasi kuchakaa, na kuruka abiria kwenye vituo vyake, ni sababu za kitoto kabisa..

Kwanini mabasi yachakae ikiwa mradi miaka yote unakusanya pesa kwenye nauli za abiria? hizo pesa zilikuwa zinakwenda wapi? hapa tatizo sio la mradi, tatizo ni serikali ndio imefeli.

Halafu hili la mwekezaji kuleta mabasi mapya lakini yeye asikusanye mapato mbona haliingii akilini? ina maana huyo mwekezaji badala ya kuja kufanya biashara hapa kwetu amekuja kutoa sadaka?!

Inawezekana vipi mwekezaji alete mabasi mapya kwa gharama zake bila kupata chochote toka kwetu? naamini kuna kitu cha muhimu Kafulila ametuficha kwenye huo mkataba.
 
Nyerere aliwaamini Wachina kwenye uwekezaji
Mwinyi aliwaamini Wananchi wake kwenye uwekezaji
Mkapa aliwaamini Makaburu kwenye uwekezaji
Kikwete aliwaamini Wazungu kwenye uwekezaji
Magufuli aliwaamini Wahindi na Mawaziri na Ma RC wake waongo uanzishwaji viwanda
Mama Samia anawaamini Waarabu kwenye uwekezaji

Ngoja tuone!
Tuliwahi sana kupata uhuru sisi, mkoloni hapa angesepa kama 2010 hivi, tungekua fiti kidogo
 
Hii nchi tuna viongozi wenye mawazo mgando sana, kwanini tunatoa kila kitu chetu kwa wageni bila kujaribu kutoa kwa sekta binafsi wazawa tuone wao watafanye kazi atleast kwa miaka mitatu mpaka mitano?
Tofauti itakua ni nini?
 
Kwani sisi Wa-Bongo, nini tunachokiweza? Tukisoma chuo tunaona sifa kujiita Daktari, Injinia, CPA, Wakili msomi, Chifu, Mheshimiwa, Mstahiki, Archtecture, Profesa, Komredi, PhD, nk...Lakini kumbe hta mradi wa daladala hatuwezi; kusimamia bandari /viwanja vya ndege hatuwezi, Loh! Nasubiri kuona stendi ya Magufuli nayo wakipewa hao ENG..!!
 
Kwani sisi Wa-Bongo, nini tunachokiweza? Tukisoma chuo tunaona sifa kujiita Daktari, Injinia, CPA, Wakili msomi, Chifu, Mheshimiwa, Mstahiki, Archtecture, Profesa, Komredi, PhD, nk...Lakini kumbe hta mradi wa daladala hatuwezi; kusimamia bandari /viwanja vya ndege hatuwezi, Loh! Nasubiri kuona stendi ya Magufuli nayo wakipewa hao ENG..!!
Taifa lime-collapse.
 
Kwa lugha nyepesi kabisa ni kwamba ''Watanzania tumeshindwa kuendesha mradi wa Mwendo kasi''

Inashangaza kiasi, inawezekanaje watu binafsi wanaweza kumiliki mabasi na kuendesha huduma za usafirishaji tena ikitumia watu wa kawaida kabisa lakini serikali na taasisi zake na wake wake wasomi wanashindwa kuendesha usafirishaji wa abiria kwenye mji mmoja, tena kwenye njia chache kati ya nyingi za mji huo.
Route:
Mbezi - Kivukoni
Mbezi - Kkoo
Mbezi - Kibaha
Mbezi- Kimara
Mbezi - Morocco
Kkoo - Morocco
Morocco - Kivukoni

Hizi route ni chini ya asilimia kumi ya route za usafirishaji wa abiria hapa Dar.

Nini tunaweza kukifanya kwa ufanisi?
Ni wizi, rushwa, soga, chuki, uongo, uzushi, ngono..............
Mashirika mengi ya serikali na serikali kwa ujumla hakuna ufanisi kwa sababu ya tumbo na ubinafsi kuwa na nguvu kuliko akili na ubunifu, na upendo kwa vizazi vijavyo na hili ni chimbuko kutoka kwenye familia zetu. Ukimwibia mwajiri jamii inakusifia.
Watanzania tuamke jamani tunaisema ccm lakini nimegundua kila mtu ni CCM (chukua chako mapema).
Huku serikalini ni rahisi kukuta mtumishi mshahara ni 1.7M na hana biashara lakini ana Discover 4 na tako la nyani (Anaconda) na Kasri kubwa madale.
Kuna msemo kuwa ukipata pa kupiga piga hadi panyooke. Matokeo yake mashirikia yanakufa nchi inabaki masikini miaka nenda rudi.

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
Vizuri tunachotaka na efficiency na serikali kuwa na hisa kwenye kampuni itakayotengenezwa kwaajili ya kuendesha mwendokasi
 
Kwani sisi Wa-Bongo, nini tunachokiweza? Tukisoma chuo tunaona sifa kujiita Daktari, Injinia, CPA, Wakili msomi, Chifu, Mheshimiwa, Mstahiki, Archtecture, Profesa, Komredi, PhD, nk...Lakini kumbe hta mradi wa daladala hatuwezi; kusimamia bandari /viwanja vya ndege hatuwezi, Loh! Nasubiri kuona stendi ya Magufuli nayo wakipewa hao ENG..!!
Education system yetu ni mbovu mkuu, ukitoka hapo viongozi wetu nao ni shida kabisayani bongo hakuna mamlaka ambayo huwezi itoa kasoro

Bila kusahau sisi wananchi nawenyewe ni mzigo mwingine
 
Kwani sisi Wa-Bongo, nini tunachokiweza? Tukisoma chuo tunaona sifa kujiita Daktari, Injinia, CPA, Wakili msomi, Chifu, Mheshimiwa, Mstahiki, Archtecture, Profesa, Komredi, PhD, nk...Lakini kumbe hta mradi wa daladala hatuwezi; kusimamia bandari /viwanja vya ndege hatuwezi, Loh! Nasubiri kuona stendi ya Magufuli nayo wakipewa hao ENG..!!
Dr Doto, Dr musukuma, Dr Sir -100,
Hii biashara hii, itawaumiza wengi SANA
 
Back
Top Bottom