Mwanza: Wahindi sasa waufunga mtaa wa Makoroboi

Mwanza: Wahindi sasa waufunga mtaa wa Makoroboi

Joined
Mar 5, 2009
Posts
95
Reaction score
34
Kwa kipindi kirefu kumekuwepo na sintofahmu jijini Mwanza hasa katika mtaa maarufu wa Makoroboi ambao hutumiwa na waenda kwa miguu wengi sana jambo ambalo lilikuwa likiwafanya machinga kung'ang'ania kufanya eneo hilo. Sasa baada ya machinga kupewa eneo laStendi ya Tanganyika Bus kwa muda, wahindi wameamua kuweka mageti na kujenga kuta ili kuziba kabisa hiyo Njia.Kwa hiyo inabidi kutafuta njia mbadala. Sasa najiuliza hivi jiji linawezaje kuruhusu kufunga hii njia ambayo iko katkikati ya jiji kwa miaka nenda rudi. Hivi kweli hata waenda kwa miguu bado wana madhara kwa misikiti ya wahindi ambayo tayari imejengewa kuta? Sitaki kuamini kwamba watu wa jiji wamewekwa mifukoni mwa hawa wenzetu.

Update:

Leo Mkuu wa wilaya akifuatana na Mkurugenzi wa Jiji walifika Makoroboi na kutangaza kusitishwa kwa ujenzi wa kuta zilikuwa zikijengwa ili kuziba mtaa huo.
 
Nchi halina mwenyewe hili.Ila na nyie wanaume wa mwanza mnawashindwa hao wala pilipili wenye vitambi kama kama. ngao ya scania.
 
Mi binafsi hiyo njia naipenda kuitumia...kama imefungwa ujue mamlaka zinafaham na sijui ramani ya jiji kwenye hilo eneo inahalisha kama njia ama eneo la taasisi/ MTU binafsi..ila Kwa Tanzania lolote hutokea na ukihoji utaambiwa unamaslah/,unateteresha usalama
 
Sioni kama kuna ubaya hiyo njia kuwa "private walkway", isitoshe unatembea kupita hapo kuelekea wapi? kwani kuna ubaya gani ukifuata barabara, ila najiuliza wamachinga hapo walipopelekwa wateja watapata wapi? kwani wateja wao niwapita njia na hapo walipopelekwa sio njiani!
 
inamaana mamlaka ya jiji la mwanza wameuza barabara ?

kwani open space zmeisha !!

kaz kwelikweli.
 
Kama wameziba njia hayo maduka hapo yanafanyanyaje biashara?,au useme tu wameziba usawa wa msikiti wao,lakini kile kinjia cha kutokea usawa wa tanesco kipo wazi mpaka hapo usawa wa msikiti wao,ambapo tena kuna kinjia cha kuchomozea tena barabarani.
 
Kama wameziba njia hayo maduka hapo yanafanyanyaje biashara?,au useme tu wameziba usawa wa msikiti wao,lakini kile kinjia cha kutokea usawa wa tanesco kipo wazi mpaka hapo usawa wa msikiti wao,ambapo tena kuna kinjia cha kuchomozea tena barabarani.
Mkuu kwa leo nimeona wakiziba kuanzia pale ilipo shule yao ya nursery ya ruparell na baadae wanasema watafunga kutokea barabara ya Lumumba. Nilikuta watu wa posta wakihamisha nguzo. Kwa hiyo hakutakuwa na shortcut ya kukatiza kati ya misikiti yao
 
hapana, atakuwa muhindi

hahaha
ccm imenichosha jamani maana ungekuwa unakaa mwanza lazima uchoke wana maamuzi ya ajabu sna

juzi tu walikuwa wanawapiga machinga mabomu leo wamekuwa lulu wamepewa eneo la stand wakati hawalipi hata kodi na wametoa hapo kenta zinazolipa mapato na kununua mafuta yanayokatwa pesa za REA


HAWAJUI HILO
 
hahaha
ccm imenichosha jamani maana ungekuwa unakaa mwanza lazima uchoke wana maamuzi ya ajabu sna

juzi tu walikuwa wanawapiga machinga mabomu leo wamekuwa lulu wamepewa eneo la stand wakati hawalipi hata kodi na wametoa hapo kenta zinazolipa mapato na kununua mafuta yanayokatwa pesa za REA


HAWAJUI HILO

Jiji la mwanza linaongozwa na chadema kuanzia madiwani wabunge hadi meya, chakushangaza pamoja na madudu yote haya viongozi wa chadema wako kimya, wao cha muhimu ni kusimikwa uchifu tu.
 
Mkuu kwa leo nimeona wakiziba kuanzia pale ilipo shule yao ya nursery ya ruparell na baadae wanasema watafunga kutokea barabara ya Lumumba. Nilikuta watu wa posta wakihamisha nguzo. Kwa hiyo hakutakuwa na shortcut ya kukatiza kati ya misikiti yao

Sioni kama kuna tatizo kuziba kwani kuna uchochoro kutekea msikiti wa ijumaa hadi duka la vipodozi la rasasi watembea kwa muguu wanaweza utumia badala ya kukatiza kwenye nyumba za ibada.
 
Jiji la mwanza linaongozwa na chadema kuanzia madiwani wabunge hadi meya, chakushangaza pamoja na madudu yote haya viongozi wa chadema wako kimya, wao cha muhimu ni kusimikwa uchifu tu.

Dada wewe mgumu wa kuelewa hivi humjui meya wa Mwanza.
 
Wanasahau hata majanga ya moto yanahitaji njia ili kuyadhibiti.
 
Back
Top Bottom