Mwanza: Wahindi sasa waufunga mtaa wa Makoroboi

Mwanza: Wahindi sasa waufunga mtaa wa Makoroboi

Kwa kipindi kirefu kumekuwepo na sintofahmu jijini Mwanza hasa katika mtaa maarufu wa Makoroboi ambao hutumiwa na waenda kwa miguu wengi sana jambo ambalo lilikuwa likiwafanya machinga kung'ang'ania kufanya eneo hilo. Sasa baada ya machinga kupewa eneo laStendi ya Tanganyika Bus kwa muda, wahindi wameamua kuweka mageti na kujenga kuta ili kuziba kabisa hiyo Njia.Kwa hiyo inabidi kutafuta njia mbadala. Sasa najiuliza hivi jiji linawezaje kuruhusu kufunga hii njia ambayo iko katkikati ya jiji kwa miaka nenda rudi. Hivi kweli hata waenda kwa miguu bado wana madhara kwa misikiti ya wahindi ambayo tayari imejengewa kuta? Sitaki kuamini kwamba watu wa jiji wamewekwa mifukoni mwa hawa wenzetu.
Hujui historia ya Mwanza toka enzi ya mkoloni hayo yote ni maeneo ya wahindi, pamoja na Nyerere kuwapora mali zao.

Nyie wote mmetoka maporini mmewakuta wahindi hapo.

Hata hapo standi ni sehemu ya Tanganyika bus.
 
hiyo njia ya kutokea msikiti wa ijumaa hadi duka la rasasi kuna tatizo gani kupita? unayosema tangu zamani ilikuwa njia ya kwenda msikitini. na maamuzi ya kufunga njia yamefanywa na madiwani wa chadema akiwemo mbunge wao.
Kama ni kutoka msikiti wa ijumaa labda unamaanisha wapitie nyerere rd. Mkuu unamaanisha barabara zote zinazoelekea kwenye nyumba za ibada zifungwe k.m sheikh amin st, lumumba,bugando n.k? Halafu kwa nini sisi watanzania kila ikizuka hoja yoyote majibu yanakimbilia kwenye siasa? Hii ni fashion ama ni udhaifu katika kujenga hoja?
 
Hujui historia ya Mwanza toka enzi ya mkoloni hayo yote ni maeneo ya wahindi, pamoja na Nyerere kuwapora mali zao.

Nyie wote mmetoka maporini mmewakuta wahindi hapo.

Hata hapo standi ni sehemu ya Tanganyika bus.
Unamaanisha kuwa hata Tanganyika yote ilikuwa ya watanganyika tena weusi. Kwa hiyo tuache misingi ya utu na ubinadamu na sie tuwaambie waarabu wahindi na wengineo warudi? Kwani kama sisi tumetoka maporini wao pia wametoka mashariki ya mbali saana. Sidhani kama ni hoja mujarabu.
 
Unamaanisha kuwa hata Tanganyika yote ilikuwa ya watanganyika tena weusi. Kwa hiyo tuache misingi ya utu na ubinadamu na sie tuwaambie waarabu wahindi na wengineo warudi? Kwani kama sisi tumetoka maporini wao pia wametoka mashariki ya mbali saana. Sidhani kama ni hoja mujarabu.
Sina maana hiyo mimi naongelea standi ya tanganyika pale Mwanza ni mali ya wahindi City wameichukuwa, hata hapo makoroboi na majengo yao na kuna shehemu yao ya ibada toka wakati wa mkoloni hawa wahindi ni watanzania kama wewe.
 
Kama ni kutoka msikiti wa ijumaa labda unamaanisha wapitie nyerere rd. Mkuu unamaanisha barabara zote zinazoelekea kwenye nyumba za ibada zifungwe k.m sheikh amin st, lumumba,bugando n.k? Halafu kwa nini sisi watanzania kila ikizuka hoja yoyote majibu yanakimbilia kwenye siasa? Hii ni fashion ama ni udhaifu katika kujenga hoja?

inaonekana hauko mwanza nikusaidie katikati ya duka la gupta trading na duka la magodoro ya vitaform kuna njia kubwa tu hadi kutokeza duka la vipodozi la rasasi hiyo ndo walkway na kuna maduka mengi tu hapo katikati kwanini kunganganie kuziba njia ya kuingia msikitini?
 
Sina maana hiyo mimi naongelea standi ya tanganyika pale Mwanza ni mali ya wahindi City wameichukuwa, hata hapo makoroboi na majengo yao na kuna shehemu yao ya ibada toka wakati wa mkoloni hawa wahindi ni watanzania kama wewe.

Wahindi waarabu wazungu wote wahamiaji tuu katika bara la Africa ila mimi/ sisi waafrika weusi Bantu, Khoisan, Cushitic na Nilo Saharan ndyo wenyewe na wewe unayeshoboka na Imani au Tamuduni au Mila za hao Wahindi/ Waarab/ Wazungu Wewe ni kafir tuu hata kwa majina yenu yanathibitisha Ukafir wenu
 
Wahindi waarabu wazungu wote wahamiaji tuu katika bara la Africa ila mimi/ sisi waafrika weusi Bantu, Khoisan, Cushitic na Nilo Saharan ndyo wenyewe na wewe unayeshoboka na Imani au Tamuduni au Mila za hao Wahindi/ Waarab/ Wazungu Wewe ni kafir tuu hata kwa majina yenu yanathibitisha Ukafir wenu
Kwa hiyo wewe kama ngozi nyeusi upewe tu duka Nyerere road au makoroboi kisa mweusi tafuta pesa acha upuuzi na uvivu.
 
Jikusanyeni wote kwa umoja wenu, nendeni mkauvunje ukuta wote, na msipofanya hivyo ndio imetoka hiyo!
 
Sioni kama kuna ubaya hiyo njia kuwa "private walkway", isitoshe unatembea kupita hapo kuelekea wapi? kwani kuna ubaya gani ukifuata barabara, ila najiuliza wamachinga hapo walipopelekwa wateja watapata wapi? kwani wateja wao niwapita njia na hapo walipopelekwa sio njiani!

Seriously?!!!
 
Hujui historia ya Mwanza toka enzi ya mkoloni hayo yote ni maeneo ya wahindi, pamoja na Nyerere kuwapora mali zao.

Nyie wote mmetoka maporini mmewakuta wahindi hapo.

Hata hapo standi ni sehemu ya Tanganyika bus.

We unawashwa sio bure afu nyie mnaoabudu Koran hua mnajihisi nyie mna undugu na waarabu/wahindi coz mnatumia lugha yao kwenye kusali, hiv kati ya mhindi na mtanganyika nani kamkuta mwenzake,takbiiir
 
inaonekana hauko mwanza nikusaidie katikati ya duka la gupta trading na duka la magodoro ya vitaform kuna njia kubwa tu hadi kutokeza duka la vipodozi la rasasi hiyo ndo walkway na kuna maduka mengi tu hapo katikati kwanini kunganganie kuziba njia ya kuingia msikitini?
Boss kwanza bado ni yale yale tu kwani bado utapita nyuma ya ukuta huo huo wa swaminarayan temple iliyokuwa hospitali zamani(bochasanas swaminarayan sanstha)lile jengo linalonakshiwa,pili hivi unaweza kulinganisha ukubwa wa kile kichochoro na hiki kinachozibwa? Sasa nina hakika hujui idadi ama wingi wa watu wanaopita mtaa huo maana itakuwa ni kubanana zaidi hata ya mtaa wa Kongo.Sasa wapita njia tena nje ya ukuta wa misikiti wana madhara gani na isitoshe wahindi wenyewe mara nyingi huenda kusali saa za usiku ambapo karibu wapita njia huwa hawapo.
update:
Leo Mkuu wa wilaya ya Nyamagana akiwa amefuatana na Mkurugenzi wa Jiji walifika wenyewe mtaa wa makoroboi na kushuhuhudia kile kinachofanywa na Wahindi. Hatimaye viongozi hao wametangaza KUSITISHA ujenzi huo.
 
Back
Top Bottom