Mwanza hii ni aibu

Mwanza hii ni aibu

kakolaki

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2017
Posts
1,611
Reaction score
2,014
Jiji la Mwanza likijiandaa kumpokea Mheshimiwa Rais Mama yetu SSH ndio uongozi umekurupuka tangu juzi kuzibua mitaro, kuondoa taka na mchanga, kichekesho zaidi ni Tanesco kufunga bulb za LED za matumizi ya kawaida kwenye nguzo za barabarani anakopitia Mheshimiwa Rais wetu kumhadaa jiji huwa lipo hivyo siku zote. Kiuhalisia jiji huwa ni chafu na lisilo na mikakati ya kutunza taswira na hadhi ya jiji, mama akitaka kujua anafanyiwa sanaa ashtukize ziara za kushtukiza maeneo ambayo hakupangiwa ajionee mwenyewe. Ni vibaya kumhadaa kiongozi wa nchi.
 
Wewe ushachukua hatua gani? Au na wewe umesema baada ya kuona Mama yetu anakuja? #kazinaiendelee
 
Wewe ushachukua hatua gani? Au na wewe umesema baada ya kuona Mama yetu anakuja? #kazinaiendelee
Kutoa taarifa umma ujue na taarifa zimfikie mama kupitia wasaidizi wake wanaosoma mitandao
 
Kwa kuusaidia ubongo wako kufikiria nipo Mwanza kikazi nina siku 4
Ndio maana huijui vzur Mwanza itakuwa ulipitishwa kwenye uchafu....Sasa una siku nne zoezi la usafi limeanza lini? Maana sio rahisi kusafsha mazingra kwa siku moja? Taa za barabaran unaongelea njia ipi?
 
Ndio maana huijui vzur Mwanza itakuwa ulipitishwa kwenye uchafu....Sasa una siku nne zoezi la usafi limeanza lini? Maana sio rahisi kusafsha mazingra kwa siku moja? Taa za barabaran unaongelea njia ipi?
Pamoja na kujaribu kuponda mtoa mada kukinga ujinga na ubabaishaji wenu au wale unawakingia kifua taarifa ziko pele, endeleeni na maigizo yenu, ikibidi mdeki barabara kabisa
 
Ndio maana huijui vzur Mwanza itakuwa ulipitishwa kwenye uchafu....Sasa una siku nne zoezi la usafi limeanza lini? Maana sio rahisi kusafsha mazingra kwa siku moja? Taa za barabaran unaongelea njia ipi?
Usitetea ni ukweli kabisa
Makongoro road taa zilikua haziawaki
Kenyata road kuanzia pale stand ya igombe had round about ya ccm kwenda nyerere road wamefunga taa za bulb ambazo zinawaka siku nzima.
Wanafanya maigizo tu hakuna jipya hapo
 
Usitetea ni ukweli kabisa
Makongoro road taa zilikua haziawaki
Kenyata road kuanzia pale stand ya igombe had round about ya ccm kwenda nyerere road wamefunga taa za bulb ambazo zinawaka siku nzima.
Wanafanya maigizo tu hakuna jipya hapo
Sikuendelea kumjibu kwa sababu Inaonekana yeye ni sehemu ya mfumo ambao haukutekeleza wajibu na wanafanya maigizo hivyo asingeyapenda maneno yale
 
Sikuendelea kumjibu kwa sababu Inaonekana yeye ni sehemu ya mfumo ambao haukutekeleza wajibu na wanafanya maigizo hivyo asingeyapenda maneno yale
Hapo hizo taa zitawaka siku 3 tu
Baadae tunarudi kule kule
Hiv kwa nn jiji na manispaa wasitoe tender kwa private company ili wawe wanafanyia maintainance hizo taa za barabaran? Maana temesa wameshindwa kabisa
 
Back
Top Bottom