Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,650
- 218,126
Je, watekaji na wauaji bado wapo? na je ni nini kosa lake?
====
Mtangazaji wa ITV Renatus Mtabuzi, akiongea kwa Uchungu na Maumivu, ameiambia JamiiForums kwamba, Jana muda wa saa mbili na nusu Usiku, amevaiwa na Watu Wawili waliokuwa kwenye pikipiki na kupigwa sana hadi akavunjwa bega.
Amedai kuna Mtu alimfuata nyumbani kwake Madale Nguzo (Jina limehifadhiwa) wakatoka naye waende kutoa hela kwenye kwenye simu Dukani. Huyu mtu aliyemfuata alikuwa na Pikipiki lakini wakati wanaenda Dukani akakata kuondoka na Pikipiki hivyo ikabidi waende kwa Mguu.
Walipofika Sehemu yenye giza Wakavamiwa na Watu Wawili waliokuwa kwenye Pikipiki wakaanza kumpiga na kumkagua Mfukoni. Baada ya hapo wakaondoka. Yule jamaa aliyekuwa naye hakutoa msaada wowote, wala hakupiga kelele wakati alikuwa eneo la tukio.
Baada ya Kuondoka ikabidi waende Polisi kutoa taarifa na kuvamiwa, ajabu huyo mtu aliyekuwa naye alipofika Polisi akabidisha mjadala kwamba Renatus amevunjika bega wakati anakimbia. Kauli hiyo limfanya Renatus kuhisi huyo mtu aliyemfuata anahusika.
Kwa sababu Renatus alikuwa ana maaumivu, alikimbizwa Hospitali ya Kitengule Tegeta ambao nao Wakamuamishia MOI Muhimbili kutokana na kwamba hawakuwa na Uwezo ya kumudumia kutokana na jinsi alivyo Vunjika.
Baada ya Kupata huduma MOI waliweza kumruhusu arudi nyumbani leo asubuhi.
Hivyo hajui kama yule mtu Polisi bado Wamemshikilia au Wamemuachilia.
Tutaendelea kuwajulisha kitakachojiri.
Pole sana Renatus.