Mwandishi amtoa kijasho RPC mkoa wa Mwanza

PRISCUS JR

JF-Expert Member
Oct 3, 2011
448
236
Kupitia STAR TV leo nimemwona rpc povu likimtoka, kufuatia maswali yaliyoulizwa na mwandishi wa habari sikujua ni wa chombo gani cha habari yakihoji kukinzana kwa taarifa alizozitoa mwanzo kwa wana habari na za sasa kuhusu kuvamiwa kwa wabunge wa CDM, rpc kamtaka mwandishi huyo aondoke na wakati huohuo akiwataka waandishi waripoti yanayosemwa na jeshi la polisi na si za waliovamiwa. habari ili iwe habari ina sifa muhimu iitwayo fareness yaan kuwe na vyanzo tofauti ili kuweka usawa. kwa mwendo huu ni hatari
 
Huyo RPC Barlow ni kati ya watu wa hovyo sana ndani ya jeshi la polisi. Ni bahati mbaya kwamba upandaji wa vyeo ndani ya jeshi la polisi unawalenga watu fulani zaidi ya wengine ndio maana na yeye kafanikiwa kufika hapo alipo.
Tangu akiwa RCO ndipo nilimgundua hamnazo kabisa, anatumia nguvu nyingi bila logic wala akili!
 
Yule afande anaonekana anatumiwa na magmba, kwanza angalia anavyojichanganya kujieleza. Lalikin mwaka 2015 sio mbali ajichunge. Tumechoka na mapolis km hawa.
 
wakuu kwa sisi ambao hatujaweza kuangalia STAR TV na hiyo issue ya hayo maswali tunaomba msaada basi wa maswali na majibu husika tupate kujua kilichojiri,tafadhari hili ni ombi
 
Tutafute tafsiri ya neno jeshi la polis ndo tutajua nini msingi au falsafa yake katika utendaji kwa hapa tz

Tafsiri yake ni hii:
1: The police are the official organization that is responsible for making sure that people obey the law.
2: Police are men and women who are members of the official organization that is responsible for making sure that people obey the law.
3: If the police or military forces police an area or event, they make sure that law and order is preserved in that area or at that event.
4: If a person or group in authority polices a law or an area of public life, they make sure that what is done is fair and legal.

Maana ya neno POLICE NI PEOPLE'S ORDER AND LAW INVESTIGATION CRIMINAL ENFORCEMENT
 
Huyo RPC Barlow ni kati ya watu wa hovyo sana ndani ya jeshi la polisi. Ni bahati mbaya kwamba upandaji wa vyeo ndani ya jeshi la polisi unawalenga watu fulani zaidi ya wengine ndio maana na yeye kafanikiwa kufika hapo alipo.
Tangu akiwa RCO ndipo nilimgundua hamnazo kabisa, anatumia nguvu nyingi bila logic wala akili!

ni wa home! Ni kati ya lile group lililomletea kashfa IGP. Pia anapenda masifa sana na anajisikia kama yeye ndo yeye hapa tanganyika.
 
Wewe mleta mada, habari gani hii umeleta JF!!!? "Same on you" narudia tena "shame ona you!!"
Kama umechoka kuandika acha!! Hulazimishwi na mtu kuleta habari hapa!! Hebu tazama ramani ya dunia ukimaliza sema kwa sauti "kooote huku JF inafika lakini sio wote wanaangalia taarifa ya habari Tanzania!!" Alafu urudie kuiandika upya hii habari!!
 
Waheshimiwa wabunge walipigwa karibu ya kuuwawa mbele ya polisi wanaolipwa tokana na kodi zetu. Wamefika kituoni Ocd anasema sasa ninyi mnataka nifanye nini? RPC anang'aka anapoulizwa maswali ya msingi na mwandishi mahiri wa habari. Siku za polisi kama hawa zinahesabika.
 
nchi nyingi ikiwemo South Africa muundo wa polisi ni kutoa huduma ya kulinda usalama - yaani services na sio jeshi

Mfano: SAPS - South Africa Police Service

Tanzania-TPF- Tanzania Police Force
 
Hizi hujuma zinamwisho wake tu,.tumechoshwa na uonevu hasa unaotokana na jeshi la polisi.
Their days are countable.
 
Iringa waandishi wa habari waliandamana kupinga vitendo vya kuchaguliwa habari za kuandika.tena wanahabari wale wanapaswa kuonwa kwa jicho la pekee , wanajitambua wamejikomboa kifikra ,moto huo ungeambaa kote nchini kupinga vitendo vya kijinga kama hivyo ,sasa RPC wa Mwanza anapomfukuza mwandishi habari kwa kuwa alimhoji mswali magumu ambayo alishindwa kuyajibu kwa kuwa wamezoea kutumwa kufanya ujinga na mafisadi kwa maslahi yao kuwapiga wabunge wasio na hatia kisa wanataka li ccm jinga liendelee kutawala, muda wao umefika siku zinahesabika watakimbia nchi kama ben bella wa uganda .

Nawashangaa waandishi wengine walibaki kufanya nini wangeungna na mwenzao, walikuwa na uwezo wa kuandika habari ya kuprovoko ili huyo rpc na IGP wake wafafanue kwani hawajui njia yangine ya kusaka ukweli? huyo rpc kubwa jinga kweli anataka waandike anayotaka anawachagulia habari.waandishi kuweni na msimamo acheni kujikomba kwa hao vikaragosi tumieni kalamu zenu, kamera zenu na akilizenu kuweni tayari kufa kwa ajili ya taifa lenu.

Mwandishi huyo nampa hongera sana pia na wapa hongera waandishi wa Iringa walifungua njia ya ujasiri kujiamini kukataa upuunzi wa viongozi wa waliowekwa na chama cha mashetani ccm.
 
ktk yala mafungu anayopelekewa kila siku na vijana wake wanapokamata magari,wahalifu nk hakuna namna ya kushikisha burungutu ili kumjerry murro?
 
Sishangai kusikia ujinga wa rpc kwani kaletwa pale kutumikia mafisadi ili kudhibiti umma,siro alikuwa mtumishi wa uma kweli ndio maana alikubalika mza
 
Kwa namna ya pekee nampongeza Kikwete kwa kuwafungulia maelfu ya polisi mwanya wa kuhudhuria mikutano ya CDM kwani naamini wapo wachache waliofunguka akili na kuondokana na umbumbumbu waliokuwa wamejaziwa na ccm. Huenda muda mfupi ujao polisi wakakataa amri za kijinga kutoka kwa viongozi wapumbavu kama RPC wa mwanza.
 
Back
Top Bottom