Mwanaye Osama aapa kulipiza mauaji ya babake

fungi

JF-Expert Member
Mar 18, 2014
2,539
4,668
Mwanaye aliyekuwa kiongozi wa mtandao wa kigaidi wa al Qaeda Osama bin Laden, ameapa kulipiza kisasi kwa mauaji ya babake.

Katika ujumbe wa sauti uliochapishwa katika mitandao Hamza bin Laden ameapa kulipiza kisasi kwa Marekani kwa kumuua babake 2011 huko Pakistan.

Ujumbe huo wa dakika 21 wenye kichwa "We Are All Osama,", Hamza ambaye inaaminika kuwa alikuwa na babake makomando wa Marekani walipowavamia na kumtwaa ameapa kuendeleza kazi aliyoianza babake.

''Tutaendelea kuwasaka na kuwapiga popote pale mtakapokuwa mumejificha ati nyuma ya pazia za usalama kwa maovu munayoyaendeleza ,Palestina, Afghanistan, Syria, Iraq, Yemen, Somalia na kote kwenye ardhi ya waislamu mnayokalia '' shirika la habari la Reuters linamnukuu.

''na kwa wale wanaodhania kuwa tutakuwa tukilipiza kisasi mauaji ya Osma ole wenu, kwanini sisi tutakuwa tukilinda dinia ya kiislamu'' alisema Hamza.

Osama aliuawa na makomando wa marekani katika maficho yake huko Pakistan mwaka wa 2011.

Hamza ambaye kwa sasa ana umri wa kati ya miaka ishirini hivi alikuwa na babake kabla ya mashambulizi ya kigaidi ya mwaka wa 9/2001 huko Afghanistan kabla ya kukimbilia Pakistan kufuatia mashambulizi makali ya Marekani na washirika wake.

Hamza kulingana na wachanganuzi anatambulishwa na kiongozi wa kidini wa kundi hilo Ayman al-Zawahiri katika ujumbe huo unaolenga kuwavutia vijana ambao kwa sasa wamejiunga kwa wingi na kundi la Islamic state.
 
propaganda mpya ishazaliwa,dunia ijipange tena kushuhudua majeshi yakivamia halafu badae yaombe msamaha kuwa yalikosea,nyamafu hawa wanatuharibia dunia yetu,mungu awalaani na utapeli wao wa dini za watu.
 
propaganda mpya ishazaliwa,dunia ijipange tena kushuhudua majeshi yakivamia halafu badae yaombe msamaha kuwa yalikosea,nyamafu hawa wanatuharibia dunia yetu,mungu awalaani na utapeli wao wa dini za watu.
 
Back
Top Bottom