Mwanaume usimwachie mkeo hela chumbani

Mwanaume usimwachie mkeo hela chumbani

MWACHIE MBELE YA WATOTO NA UMWAMBIE NA MATUMIZI YAKE, NA WATOTO WASIKIE, USIJE KUISHI MAISHA YA UPWEKE UZEENI.

[emoji1427][emoji1427][emoji1427][emoji1427][emoji1427][emoji1427][emoji1427][emoji1427]

MWANAUME
Unamwachia mkeo hela ya chakula chumbani. Mke anatoka na kapu, anaenda kununua chakula. Anapika, anawaambia watoto, "njooni wanangu mle. Nimewapikia chakula kitaaamu!" Watoto wakishakula Wanasema "Asante Mama".

MWANAUME
Unamwachia mkeo hela ya nguo za sikukuu chumbani,
Kesho yake anatoka kwenda kununua nguo. Akirudi anawaambia, "wanangu nimewanunulieni nguo za sikukuu, njooni mjipimie!" Watoto wakishajipima, anawaambia, "Wanangu mmependeza eeeh! Si mnaona ninavyowapenda!?" Watoto wanafurahi na kusema, "Asante Mama".

MWANAUME
Kila aina ya pesa ya matumizi unamwachia mkeo chumbani...

MWANANUME
Ukifika muda wa kutoa ada unamkabidhi mkeo hela chumbani. Kesho yake mkeo anawaambia watoto kuwa anaenda kuwalipia ada ya shule. Akirudi anawaambia, "Wanangu nimeshawalipia ada, na gari za shule zitakua zinawapitia. Nataka msome wanangu ili baadae mje mnitunze". Watoto wanasema, "Asante Mama".

KIBAYA ZAIDI:
Ukifika muda wa kutoa adhabu, mkeo yeye hatoi adhabu. Anawaambia Watoto, "ngoja baba yenu arudi!" Na wewe ukirudi unaelezwa na mkeo matatizo ya wanao. Unachukua bakora unawaadhibu watoto bila kujua kuwa unazidi kujenga uhusiano M'BAYA na Wanao.

NGUMU KUMEZA
Ukifika uzeeni, watoto wako hawana KUMBUKUMBU yoyote Ya mema uliyowafanyia.

NA UKUMBUKE KUWA:
MTOTO ANAANZA KULISHWA SUMU YA MANENO KUTOKA KWA MAMAYAKE KUANZIA UMRI WA MIAKA 9 HADI 15.

MWANAUME KUWA MAKINI SANA

ZINGATIA HAYO KWA MAISHA YA UZEENI.
Watoto hawapimi upendo kwa sababu hizo tuu...Baba mwenye upendo kwa watoto ni zaidi ya hayo ya fedha za matumizi au ada..upendo haujifichi au hauwezi kufichwa na maneno fulani ya mama. Mwanaume mwajibikaji hahitaji kujionesha kwa mtoto ni nini katoa au hajatoa.. isipokuwa wale irresponsible fathers wanahitaji sana huo ushauri wako ili wajioneshe kuwa na wao wapo.
Upendo wa baba kwa watoto huwa haujifichi hata iweje..utaonekana tuu.

Watoto wanao uwezo mkubwa mna wa kumtambua mtu anayewapenda na huwezi kumdanyanya hata iweje.mtoto akikuangalia usoni tuu anajua unampenda au unazuga tuu.
Baba unawahi kurudi nyumbani..unacheza na watoto ...unawasaidia homework..unatoka nao mazoezi au matembezi madogo madogo..unaenda nao kanisani au msikitini..unawafundisha kwa vitendo study za kazi..mf.wanakuona unapenda bustani..mifugo..nk watakuiga na kukupenda sana..

Yaani ukirudi tuu kutoka kazini utaona wanavyokukimbilia mpaka wanaanguka ili walao kila mmoja awe wa kwanza kukupokea..
Ukirudi lazima utakuwa umebeba chochote mkononi..mboga..vitafunwa..mahitaji mahitaji madogo madogo ya nyumbani..

Sabuni,sukari,gesi..hata kamfuko ka matunda tuu..sio kila siku bali kila unapojaliwa..

Watoto watakupenda sana tuu..watoto wa kiume watatamani wakiwa wakubwa wawe kama baba yao.

Watoto wa kike watatamani sana wakija kuanza familia Basi wapate mwenzi ambaye anaupendo kama baba yao kwa familia.
Huhitaji kujionesha onesha kwa watoto eti wewe ni baba ndio uliotoa hiki wala kile..

Hata kama mama angekuwa na kipato kikubwa kuliko wewe lakini watoto wanajua unawapenda aaa watakupenda tuu hata mama awafundishe ubaya gani..labda mmoja tuu anaweza akawa against wewe but wengine watakuheshimu tuu..

Wanaume wengi ni timeless na familia..hawana muda na watoto eti kujifanya wapo bize na utafutaji..akipata nafasi anaona ni heri akautumie huo muda..bar, kuangalia mpira,kucheza bao,vijiweni au hata kuzurura tuu kwa marafiki zake eti wanampa dili..

Kuwa Baba wa familia ni zaidi ya kuprovide matumizi au ada..
 
Sipendi show off nitaendelea kumuachia chumbani.
Alichoandika Mtoa mada ni kweli tupu....impact inaonekana uzeeni SAA hii hutaona shida ....ujue kwa nini? Penzi bado lipo subiri mking'oka meno baba!!!!!
 
Kama ni hivyo, basi naomba niseme wazi umeshindwa kuishi na mkeo kwa akili.
Next time akikukosea pia utataka umkanye mkeo mbele ya watoto ili wajue makosa ya mamayao eti wasije wakakutenga uzeeni...[emoji2955][emoji2955]
 
Mimi mama yangu alikuwa anasema kabisa baba yenu kaacha pesa ya hiki na hiki hivyo akirudi jioni shart kwenda kusema asante kuhusu fimbo maza kanichapa sana kuliko hata mzee mwenyewe
Kimsingi mama aliwashirikisha katika kila alilo ona linafaa ili mpate kuwa na ufahamu wa yalio ndani ya uwezo wa wazazi, pamoja na kuwajenga kwenye makuzi
 
Alichoandika Mtoa mada ni kweli tupu....impact inaonekana uzeeni SAA hii hutaona shida ....ujue kwa nini? Penzi bado lipo subiri mking'oka meno baba!!!!!
Mungu anisaidie wakianza maisha yao kila mtu ashike lake.
 
Sipendi show off nitaendelea kumuachia chumbani.
Mleta Mada madeinmusoma bado anaishi yale maisha ya Baba zetu waliouwa wanao kina Mama tegemezi
miaka hii unakuta Mama ni Manager Tawi lla Benki uje kumuachia pesa ya ada sebuleni wakati wewe Baba ni dereva Taxi unabangaiza sijui utamuambiaje mwanao hapo uzeeni
Mwanamume nena Benki kalipe Ada hao ni watoto wako mama akirudi anakuta watoto hawajafukuzwa shule
una mizunguko yako wahisha mboga usishinde kwenye bao au mpira mpakka jioni huji watoto watalalaje
Hao kina mama ni wa kupita ndio maana watoto hawachukui majina yao
 
Fanya hivi ukitaka uishi vizuri uzeeni...

Zawadi kubwa ya kuwapa wanao ni kumpenda mama yao hata kwa kulazimisha, mbusu mbele zao km Mbowe, ili ufanye haya Oa mwanamke mzuriii unaempenda hata iweje!! ili hata akizeeka umpende,

wakisema bwii wajibu ''yule ni mke wangu mnatakaje? kwa kuwa wanampenda usimseme vibaya, ubaya wowote wajibu msameheni mama yenu!

Ukiona unaanza kukomaa umri kusonga jirekebishe umpende mkeo hasa! hata wao wakikupa hela mpasie mkeo mbele zao! Fanya shopping na baadhi yao unawauliza ''hii mama yenu inamtosha?

Ukitoa hela wape kidogo lkn zidisha maradufu kwa mama yao! wape wampelekee!- kuonyesha unamjali.

Kwa Dunia ya kisasa ya ki Beijing, Watoto wa kike wana huruma sana kwa Baba zao! na kuna kamvuto fulani hivi, kati ya me na ke ni msaada sana kwako Baba wapende mnoo! Dume lita pewa Limbwata. mzidishie sifa
 
Watoto hawapimi upendo kwa sababu hizo tuu...Baba mwenye upendo kwa watoto ni zaidi ya hayo ya fedha za matumizi au ada..upendo haujifichi au hauwezi kufichwa na maneno fulani ya mama. Mwanaume mwajibikaji hahitaji kujionesha kwa mtoto ni nini katoa au hajatoa.. isipokuwa wale irresponsible fathers wanahitaji sana huo ushauri wako ili wajioneshe kuwa na wao wapo.
Upendo wa baba kwa watoto huwa haujifichi hata iweje..utaonekana tuu.

Watoto wanao uwezo mkubwa mna wa kumtambua mtu anayewapenda na huwezi kumdanyanya hata iweje.mtoto akikuangalia usoni tuu anajua unampenda au unazuga tuu.
Baba unawahi kurudi nyumbani..unacheza na watoto ...unawasaidia homework..unatoka nao mazoezi au matembezi madogo madogo..unaenda nao kanisani au msikitini..unawafundisha kwa vitendo study za kazi..mf.wanakuona unapenda bustani..mifugo..nk watakuiga na kukupenda sana..

Yaani ukirudi tuu kutoka kazini utaona wanavyokukimbilia mpaka wanaanguka ili walao kila mmoja awe wa kwanza kukupokea..
Ukirudi lazima utakuwa umebeba chochote mkononi..mboga..vitafunwa..mahitaji mahitaji madogo madogo ya nyumbani..

Sabuni,sukari,gesi..hata kamfuko ka matunda tuu..sio kila siku bali kila unapojaliwa..

Watoto watakupenda sana tuu..watoto wa kiume watatamani wakiwa wakubwa wawe kama baba yao.

Watoto wa kike watatamani sana wakija kuanza familia Basi wapate mwenzi ambaye anaupendo kama baba yao kwa familia.
Huhitaji kujionesha onesha kwa watoto eti wewe ni baba ndio uliotoa hiki wala kile..

Hata kama mama angekuwa na kipato kikubwa kuliko wewe lakini watoto wanajua unawapenda aaa watakupenda tuu hata mama awafundishe ubaya gani..labda mmoja tuu anaweza akawa against wewe but wengine watakuheshimu tuu..

Wanaume wengi ni timeless na familia..hawana muda na watoto eti kujifanya wapo bize na utafutaji..akipata nafasi anaona ni heri akautumie huo muda..bar, kuangalia mpira,kucheza bao,vijiweni au hata kuzurura tuu kwa marafiki zake eti wanampa dili..

Kuwa Baba wa familia ni zaidi ya kuprovide matumizi au ada..
 
Mapenzi ya mtoto kwa mama huwezi kuyatenganisha kabeba mimba kwa tabu kazaa kwa shida wabarikiwe wa mama wote
 
Watoto hawapimi upendo kwa sababu hizo tuu...Baba mwenye upendo kwa watoto ni zaidi ya hayo ya fedha za matumizi au ada..upendo haujifichi au hauwezi kufichwa na maneno fulani ya mama. Mwanaume mwajibikaji hahitaji kujionesha kwa mtoto ni nini katoa au hajatoa.. isipokuwa wale irresponsible fathers wanahitaji sana huo ushauri wako ili wajioneshe kuwa na wao wapo.
Upendo wa baba kwa watoto huwa haujifichi hata iweje..utaonekana tuu.

Watoto wanao uwezo mkubwa mna wa kumtambua mtu anayewapenda na huwezi kumdanyanya hata iweje.mtoto akikuangalia usoni tuu anajua unampenda au unazuga tuu.
Baba unawahi kurudi nyumbani..unacheza na watoto ...unawasaidia homework..unatoka nao mazoezi au matembezi madogo madogo..unaenda nao kanisani au msikitini..unawafundisha kwa vitendo study za kazi..mf.wanakuona unapenda bustani..mifugo..nk watakuiga na kukupenda sana..

Yaani ukirudi tuu kutoka kazini utaona wanavyokukimbilia mpaka wanaanguka ili walao kila mmoja awe wa kwanza kukupokea..
Ukirudi lazima utakuwa umebeba chochote mkononi..mboga..vitafunwa..mahitaji mahitaji madogo madogo ya nyumbani..

Sabuni,sukari,gesi..hata kamfuko ka matunda tuu..sio kila siku bali kila unapojaliwa..

Watoto watakupenda sana tuu..watoto wa kiume watatamani wakiwa wakubwa wawe kama baba yao.

Watoto wa kike watatamani sana wakija kuanza familia Basi wapate mwenzi ambaye anaupendo kama baba yao kwa familia.
Huhitaji kujionesha onesha kwa watoto eti wewe ni baba ndio uliotoa hiki wala kile..

Hata kama mama angekuwa na kipato kikubwa kuliko wewe lakini watoto wanajua unawapenda aaa watakupenda tuu hata mama awafundishe ubaya gani..labda mmoja tuu anaweza akawa against wewe but wengine watakuheshimu tuu..

Wanaume wengi ni timeless na familia..hawana muda na watoto eti kujifanya wapo bize na utafutaji..akipata nafasi anaona ni heri akautumie huo muda..bar, kuangalia mpira,kucheza bao,vijiweni au hata kuzurura tuu kwa marafiki zake eti wanampa dili..

Kuwa Baba wa familia ni zaidi ya kuprovide matumizi au ada..
Tena hapo ndiyo uwiii Baba unataka maatizo, mke anachukia kabisa, anaona wivu anaweza asile vizuri kwa kujiuliza, kwa nini unapendwa hivo wewe kuliko yeye, wanawake kama wana asili ya vipepo flani hivi, anaweza hata kuwaroga wabadilishe mwelekeo, au akadhani wewe umewaroga wakupende, kupunguza hii wewe piga misele tu, wakikupenda tank you, wakikunanga tank you!!!!

Wengine hupata watoto ujanani, wa kike hukua faster, Kama kabinti ni kakigori anaweza sema mbovu mbovu ili mradi uchukie tu, akutoe kwenye reli!!! ''kwa nini unaambatana na binti yako sana?? humpi nafasi???

Some times hata anawachungulia kwa kunyata, nyatu!! nyatu!! ili ahakikishe. Au utasikia kuna mapinduzi baridi humu ndani!! utashangaa upendo wa Binti unapoa bila sababu!!! lkn Baba yeye hatilii mashaka Mahusiano ya Mama na watoto wa kiume, siyo wote wako ivo labda uwe na bahati kuwa na mke Msabato,
 
Back
Top Bottom