Mwanaume ni yupi hapa??

BAK...usisahau pia ni sifa ya kiume kujinyima na sio kuendekeza 'kila kinachotaka moyo'...
sometimes mwanaume huonekana mwanaume kwa kukubali kukikosa 'anachokipenda'kwa faida ya wengine....
sasa hapa je??????

...but not always 🙂 kipenda roho banaaa! Hata malaya hutofautiana kiwango cha umalaya wao na wengine huamua kutulia na kuwa wake wema. Unaweza kuoa huyo usiyempenda ukawa saa zote kiguu na njia na hivyo kutomridhisha naye akaamua kucheza viwanja vya ugenini. Hii kitu ngumu banaa, unaweza ukawa upande wowote ule ukashusha points za uhakika, lakini kipenda roho siku zote hula nyama mbichi na methali hii ina uzito mkubwa sana kwenye mapenzi.
 


unaona...ndo maana mimi naona kama hawa akina Diamonds wamekuwa majasiri zaidi....na pengine watu wengi wanatamani kufanya maamuzi kama hayo......but 'ujasiri' unakosekana....
 

nakubaliana na wewe Mkuu.Jana kuna mtu kapost kwenye jf nukuu ya Steve Jobs(RIP) ambaye alisema(nanukuu) 'life is short,do not live for others' mwisho wa nukuu.
 
nakubaliana na wewe Mkuu.Jana kuna mtu kapost kwenye jf nukuu ya Steve Jobs(RIP) ambaye alisema(nanukuu) 'life is short,do not live for others' mwisho wa nukuu.

life is short?msome King'asti pia amenukuu hivyo hivyo but kupinga hii
 
Daaah!bt hyo rahs braa,ukipnd ujue jamii haina nafas yyte coz hata ikiwa nayo haiwz fny any chngz,ki2 kupnd hata angkua anatembe uch usng ona ajibu!imekutokea nin kaka,fresh kaz moyo uzba maskio ww ndo ulyepnd cyo jamii
 
huyo namba moja, ameoa kitu anapenda na amesimamia hisia zake. Mke ni wake yeye na ataishi nae yeye kwa hyo ndg,jamaa marafiki sio watakaoishi na huyo mke. Ni mwanaume mwenye msimamo ambaye yupo tayari kupigania anachokipenda/taka
 
Daaah!bt hyo rahs braa,ukipnd ujue jamii haina nafas yyte coz hata ikiwa nayo haiwz fny any chngz,ki2 kupnd hata angkua anatembe uch usng ona ajibu!imekutokea nin kaka,ila fresh kaza moyo uzbe maskio ww ndo ulyepnd cyo jamii
 

wanaume wengi huangalia sana suala la sex yaani urahisi wa mwanamke kupatikana pindi mwanaume akihitahitaji na urahisi wa kuonana na mwanamke
 
1.moja unampenda na umeamua kumuoa mwanamke ambae jamii haimuheshimu sana.labda anaonekana 'malaya'
au anatoka out of your class na kadhalika.....

...the boss, kwakuwa "labda anaonekana" ndilo neno lililotumika, nakubaliana na wengine kwamba huyu ndiye
mwenye maamuzi aka mwanaume mwenye maamuzi thabiti.

lakini, angekuwa ameoa mwanamke malaya...anayejulikana naye anamjua...---***** huyo!
 
Uamuzi wa kiume ni ule ambao utakuwa na matokeo mazuri long term.
  1. Ukiamua kuoa mwanamke ambaye ana sifa mbaya katika jamii kwa matarajio kuwa atabadirika au ataendelea na hiyo tabia mbaya (wewe umechagua umalaya) halafu wewe uonekane ndo umefanya uamzi wa kiume ni KUJILISHA UPEPO AT BEST. Sifa mbaya watu hawapewi tu kwa kuwa jamii inawachukia; wanapewa sababu ya matendo yao ambayo hayakubaliki katika jamii iliyostarabika. Yaani yana madhara ya kiafya au ya kijamii. Sasa wewe unapoamua kuoa mwenye tabia mbaya (umalaya) unatarajia nini? Falsafa na busara ya jamii ni kuwa asiyesikia la mkuu huvunjika guu - Na ndoa kama hiyo (ya kuoa malaya) huwa mwishowe ni "tulikuambia hukusikia". Kunguru hafugiki, usitarajie tutakuita mjanja (au mwanaume wa ukweli) kwa kujaribu kufuga Kunguru, watu wengi watakuona fara tu kwani hatima ya hiyo ndoa siku zote inajulikana. Hii "impulse" ya mvuto inayokuwepo mwanzoni itakuja kusambaratika pale utakapojua kuwa tabia hizi za kimalaya ni mbaya na hazivumiliki.
  1. Kuoa Mwanamke aliyekuwa na kulelewa katika maadili na akajitunza ndo falsafa sahihi. Jamii ina mifano ya kutosha sana ya kuthibitisha kuwa ndoa na mahusiano ya hivi yanadumu sana hata kama mwanzoni moyo wako ulikuwa unakudanganya kuwa humpendi. Kumbuka katika ndoa, hicho mnachoita kupendana, kinasambaratika mara moja pale vile vitabia vibovu vinapoanza kujitokeza. Kwa mwanamke decent ambaye anajitunza; tabia yake na matendo yake yatafunika hiyo hali ya kutovutiwa naye mwanzoni. Ni bora uwe na yule anayekupa amani moyoni hata kama mvuto si mkubwa sana - Mbeleni utokuja gundua kuwa ulichagua kilicho chema!
 
"anayeonekana malaya" Haonekani hivyo tu, ila kuna visababishi vinavyosababisha aonekane hivyo! Na kwa kuwa tabia hiyo (umalaya) ni moja wapo ya tabia ambazo ni anti-social; yaani tabia zinazoleta migawanyiko na migogoro katika jamii si uamzi wa KIUME kumuoa. Hata kama utamuoa huyo kwa kisingizio cha kumpenda, hapo mbeleni utakuja kugundua kuwa jamii haikuwa IMEKOSEA. Na hapo ndo itakuwa imeshakula kwako kwani ku-reverse ndoa ni ngumu na gharama zake ni kubwa sana!!

Jamii ina mifano mingi sana ya kushuhudia kuwa ndoa nyingi za namna hii huishia kubaya na hicho kinachoitwa mvuto na kumpenda hapo mwanzoni hakifui dafu kwa vitabia vya ki-"antisocial". Ndoa zote zinazosambaratika mwanzoni watu walisema tunapendana sana; wakadharau viashiria vya wazi. Mojawapo ya viashiria kuwa huyo hakufai ni hiyo ya "kuonekana malaya". Miaka mitano ndani ya ndoa ndo utajua kuwa "kuonekana malaya" ni kitu kibaya na hapo itakuwa umeshachelewa!!
 
Boss naomba nianze kwanza kwa usemi wa kipenda roho hula nyama mbichi

Pili niseme muoaji ni wewe sio ile jamii inayokuzunguka japo nae atakuwa part ya jamii ila wewe ndie utakayakuwa part ya maisha ya muolewaji kwa maisha yake yote.
Kuna vitu ambavyo umeviona kwa huyo dada regardless ya hayo maneno owanayomsema kuwa sio class yako au ni malaya au haendani na wewe

Ila mapenzi hayajali hayo ila unachoangalia je huyo mama pamoja na madhaifu wanayomsema nayo kuwa sio class yako au ni malaya, je ni mwanamke wa kukufaa wewe. Je anatutimiza vigezo vyako ambavyo wewe umejiwekea. JE atakuwa mke mwema maana unachotafuta wewe ni mke wa kukaa nae ndani ya nyumba yako na ambaye atakuzalia watoto awalee watoto wako katika njia ipasayo. Mwanamke atakayetulia na wewe kama mumewe. Kama amekukuta uko kwenye hiyo class ya juu aendane na wewe na abadilike kulingana na mazingira na wakati. Jamii iko pale sio kukusaidia kukaa na mkeo bali kuangalia mapungufu ya mkeo na kuyasema wala hawatakusaidia kwa namna nyingine kumjenga mkeo au kumbadilisha.

Unaweza kuamua kumuoa huyo ambaye wanasema ni wa class yako au sio malaya au anayeendana na wewe ukajikuta umepata matatizo ambayo hukutarajia

Halafu je hebu jiulize huyo dada aliingia kwenye umalaya kwa sababu gani. Nini kilimfanya awe hivyo. Au je hajafikia hiyo class yako kwa sababu gani.

Uamuzi wa kiume nafikiri ni kufanya kile ambacho kunakiamini na kukisimamia bila kujali jamii inasemaje au inakuchukuliaje. Kusimamia jambo unaloliamini licha ya kwamba kuna vipingamizi vingi
 
Hayo ni maisha yako wewe, huishi kwa ajili ya kumfurahisha binadamu mwingine na huwezi mfurahisha kila mtu. Wewe ulimwona ni malaya, katoka ktk low class, lakini umempenda, umeridhika naye, umeamua kuishi naye sababu una hakika utammudu na kustahimili matatizo yake. Mwenye maamuzi ni wewe, na hayo ndo maamuzi ya kiume. Kuishi na mtu usiyempenda ni kuidanganya nafsi yako na ni chanzo cha kuchuma dhambi usizozitarajia.
 

this may be out of topik dada Asha:hivi kuna sababu halali za kina dada 'kuuza 'ile kitu eenh??!nisamehe bure si unajua tena!
 

you are right kin'gasti ,your family is everything mume mke anaweza akakukimbia bt family as family never .........
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…