Mkuu unajua wanaume wengi hua hawapendi wake zao wafanye kazi sababu wanakua na mawazo mengi au kwa wanayo yaona maofisini, mimi binafsi mume wangu hataki nifanye kazi wakati alikunikuta nafanya kazi,nikamwambia tuna watoto kuna leo nakesho,sipendi nilie mumewangu umeniachia watoto ntawaleaje ila nataka nilie sitompata mume kama wewe
ikiwa utatangulia wewe na nikitangulia mimi basi uitakua nimekusaidia japo kidogo kwenye maisha japo kusomesha watoto
lakini kuna siku anaamka kwani lazima uende kazini? hawajua kama una familia sasa haya mambo mkuu ni kila mtu anavyo lichukulia kwenye mawazo yake lakini mimi nakubaliana na wewe kua maisha nikusaidiana na kama mke hana uwezo wakufanya hata biashara basi hata akilea watoto pia nayo sio kazi ndogo..