Fidel80
JF-Expert Member
- May 3, 2008
- 21,947
- 4,444
MKAZI wa jijini Mwanza, Thomas Jilala (22), anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma kwa tuhuma za kumuua anayedaiwa kuwa mpenzi wake, Levina Kiwili (26), mkazi wa Mfaranyaki katika Manispaa ya Songea, ambaye alikutwa akiwa amekufa kwa kunyongwa shingo katika nyumba ya kulala wageni ya Mikumi, mjini Songea.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma, Paulo Mashimbi, alisema tukio hilo lilitokea Oktoba 22 mwaka huu saa 2 asubuhi, huko kwenye nyumba ya kulala wageni chumba namba kumi.
Mashimbi alisema kuwa ililetwa taarifa katika kituo kikuu cha polisi mjini Songea, kuwa katika nyumba ya kulala wageni ya Mikumi chumba namba kumi kilichokuwa kikitumika na watu wawili, alikutwa mwanamke akiwa amefariki huku mwanaume aliyekuwa naye akiwa amekimbia.
Alisema kuwa Oktoba 23 mwaka huu, saa sita usiku mtuhumiwa anayedaiwa kufanya mauaji hayo, ambaye anadaiwa kuwa mpenzi wa marehemu, alikamatwa akiwa anatoroka kuelekea barabara ya Songea-Tunduru maeneo ya Namtumbo.
Alieleza kuwa mtuhumiwa baada ya kukamatwa alikutwa na baadhi ya vitu vya marehemu ikiwemo saa aliyokuwa ameivaa kabla ya kuuawa pamoja na simu mbili za mkononi.
Alifafanua kuwa mtuhumiwa pia alikutwa na vifaa vingine vilivyoibiwa kwenye ofisi aliyokuwa akifanyia kazi marehemu usiku wa kuamkia siku ya tukio.
Hata hivyo vyanzo vya habari vimeeleza kuwa Jilala kabla hajafanya kitendo hicho, alikuwa akionekana mara kwa mara katika ofisi ya marehemu ijulikanayo kwa jina la Mpenda Production kwa madai kuwa amekuja kutengeneza kadi za harusi ya kaka yake.
Aidha Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limesema linaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo na kwamba baada ya uchunguzi huo kukamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu shtaka la mauaji linalomkabili.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma, Paulo Mashimbi, alisema tukio hilo lilitokea Oktoba 22 mwaka huu saa 2 asubuhi, huko kwenye nyumba ya kulala wageni chumba namba kumi.
Mashimbi alisema kuwa ililetwa taarifa katika kituo kikuu cha polisi mjini Songea, kuwa katika nyumba ya kulala wageni ya Mikumi chumba namba kumi kilichokuwa kikitumika na watu wawili, alikutwa mwanamke akiwa amefariki huku mwanaume aliyekuwa naye akiwa amekimbia.
Alisema kuwa Oktoba 23 mwaka huu, saa sita usiku mtuhumiwa anayedaiwa kufanya mauaji hayo, ambaye anadaiwa kuwa mpenzi wa marehemu, alikamatwa akiwa anatoroka kuelekea barabara ya Songea-Tunduru maeneo ya Namtumbo.
Alieleza kuwa mtuhumiwa baada ya kukamatwa alikutwa na baadhi ya vitu vya marehemu ikiwemo saa aliyokuwa ameivaa kabla ya kuuawa pamoja na simu mbili za mkononi.
Alifafanua kuwa mtuhumiwa pia alikutwa na vifaa vingine vilivyoibiwa kwenye ofisi aliyokuwa akifanyia kazi marehemu usiku wa kuamkia siku ya tukio.
Hata hivyo vyanzo vya habari vimeeleza kuwa Jilala kabla hajafanya kitendo hicho, alikuwa akionekana mara kwa mara katika ofisi ya marehemu ijulikanayo kwa jina la Mpenda Production kwa madai kuwa amekuja kutengeneza kadi za harusi ya kaka yake.
Aidha Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limesema linaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo na kwamba baada ya uchunguzi huo kukamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu shtaka la mauaji linalomkabili.
Source: Mwanaume amuua mpenzi wake gesti