Mwanaume akikuzalisha asikuoe amekuharibia maisha

Mwanaume akikuzalisha asikuoe amekuharibia maisha

Wengi waliozalishwa na kushindwa kuolewa na baba mtoto/watoto wake huwa wanatabia mbaya sana( 'maraya' au wachepukaji waliokubuhu)
 
Watu huwa hawapangi kuzaa nje ya ndoa
watu huwa hawapangi kuzalisha nje ya ndoa
watu huwa hawapangi kutoku oa waliowazalisha nje ya ndoa
watu huwa hawapangi kutoku olewa na walio zaa nao nje ya ndoa...

kinachotokea kinaitwa 'shit happens' .......

'shit happens' mwanaume wa ukweli ndiyo anajua haya........maisha hayatabiliki.....si kila unachopanga kinakuja kama kilivyo......mengine haujapanga lakini yanatokea.......unachotakiwa kufanya ni kukubali hali halisi na ku move on.........
 
Wengi waliozalishwa na kushindwa kuolewa na baba mtoto/watoto wake huwa wanatabia mbaya sana( 'maraya' au wachepukaji waliokubuhu)

ujue wengine tumetoka kwenye hizo familia lakini mama yetu hakuwa malaya au mchepukaje aliyekubuhu......kwa hiyo unatoa maoni kumbuka kuna watu tumetoka kwenye familia ambazo ......mama zetu hawajaolewa na baba aliyemzalisha........ingawa walikuja kuolewa na wanaume wengine na mpaka leo bado wapo kwenye ndoa....na wajukuu wamepata........
 
Wadada kuweni makini na mahusiano. Mwanaume akikuzalisha na asikuoe hupunguza sana nafasi yako ya kuolewa hasa na mwanaume wa ndoto zako. Mila nyingi zinakataza vijana kuoa mwanamke ambaye amekwisha zalishwa. Kuweni makini na future zenu. Hisia za mioyo yenu zisiwapotoshe...

Lugha ya @kuzalishwa inavyoniudhi! Alibakwa? Hajitambui?
 
Wengi waliozalishwa na kushindwa kuolewa na baba mtoto/watoto wake huwa wanatabia mbaya sana( 'maraya' au wachepukaji waliokubuhu)

Nina wasiwas na uwezo wako wakufikiri. ULISIKIA WAPI MALAYA ANAZAA??????? MALAYA anatoa ili biashara isidode. tabia mbaya unaitathimin kwen lipi??? kwa taarifa yako wanaume ndio washenzi wa adabu, kwanin uzae na mtu kisha umuache??? nahis nikiendelea hapa ban itanihusu.
 
Sitoweza daima kumpa mimba mwanamke ambaye hawezi Kuja kuwa mke wangu, Never on earth.
 
wasichana wengi wanaozalishwa huwa wanadanganywa kwamba kwa kukubali kwao wataolewa na kumbe sio.
 
Wadada wanao zaa na hawaolewi wao, huwa kuna baadhi ya vitu vinavyo wafanya wasi olewe kwa namna moja au nyingine kwa mfano uvivu na kutojituma... lakini mwanamke akiwa mchapa kazi na anajua ni nini anacho kifanya basi hata mwanaume aruke ruke vipi ipo siku atamrudia mwanamke aliye zaa nae....
 
naona Mungu kuumba mwanamke ndo awe anazaaa basi hukumu zote za kuzaa nje ya ndoa zinamwangukia yeye kana kwamba yeye anazaa mwenyewe bila mwanaume. na je wanaume waliozaa nje ya ndoa wao hawashuki thamani ya kuoa?. au kwao ni haki lakini ikitendeka kwa mwanamke ni haramu? tuache mfumo dume. utakuta mwanaume kaoa halafu anamletea mke wake watoto hadi 3alee halafu saa hizo alikuwa hataki mke mwenye mtoto. ukikataaa mwanamke mwenye mtoto nawe usilete wanao
 
Watu huwa hawapangi kuzaa nje ya ndoa
watu huwa hawapangi kuzalisha nje ya ndoa
watu huwa hawapangi kutoku oa waliowazalisha nje ya ndoa
watu huwa hawapangi kutoku olewa na walio zaa nao nje ya ndoa...

kinachotokea kinaitwa 'shit happens' .......

For sure shit happens.....
 
'shit happens' mwanaume wa ukweli ndiyo anajua haya........maisha hayatabiliki.....si kila unachopanga kinakuja kama kilivyo......mengine haujapanga lakini yanatokea.......unachotakiwa kufanya ni kukubali hali halisi na ku move on.........

Unajua kabisa hutaweza muoa...tuseme hukujua basi...ila unajua kabisa ukifanya ngono bila mpira kuna magonjwa na mimba,yanini usivae kondomu?....for godsakes huna sababu on earth kwanini hukutumia condom...

Nipe sababu....c'mon,convince me
 
'shit happens' mwanaume wa ukweli ndiyo anajua haya........maisha hayatabiliki.....si kila unachopanga kinakuja kama kilivyo......mengine haujapanga lakini yanatokea.......unachotakiwa kufanya ni kukubali hali halisi na ku move on.........
condom hazipo?kwanini msitumie
 
Nina wasiwas na uwezo wako wakufikiri. ULISIKIA WAPI MALAYA ANAZAA??????? MALAYA anatoa ili biashara isidode. tabia mbaya unaitathimin kwen lipi??? kwa taarifa yako wanaume ndio washenzi wa adabu, kwanin uzae na mtu kisha umuache??? nahis nikiendelea hapa ban itanihusu.

Wa hivi unawaepuka tu.
 
Ni vigumu kutozalishwa nje ya ndo hadi watakapoacha tamaa ya vitu vya watu;pesa,vyakula,usafiri,mavazi n.k TAMAA GHALI
 
Sio lazima uazae ndani ya ndoo hata nje ya beseni pia.
 
Back
Top Bottom