Mwanasheria mpya Zanzibar hataki kurudi nchini

Mwanasheria mpya Zanzibar hataki kurudi nchini

Kwi kwi kwi kwi lol!!!! Hata kazi zake atafanya kwa njia ya simu huku akiendelea kuishi majuu! Only in Tanzania pwagu na pwaguzi's country.


Atamwapisha kwa njia ya simu kama wanaweza kupiga kura za sms watashindwa mwapisha .....
 
watajua wenyewe hakuna kisichowezekana ndani ya ccm kama mfu amepiga kura unategemea nn ccm ni janga la taifa
 
Mwaka 1964 wakati Tanganyika inaimeza Zanzibar mwanasheria mkuu wa Zanzibar Dourado alitimuliwa, mwaka 1984 wakati Tanganyika inataka kuimiliki Zanzibar , Rais wa Zanzibar Jumbe alifukuzwa, mwaka 1988 wakati Tanganyika ikishona koti lake waziri Kiongozi Seif Shariff Hamad alifukuzwa , mwaka 2014 wakati Tanganyika ikishona kanzu ya Muungano badala ya koti mwanasheria mkuu wa Zanzibar Othman Masoud amefukuzwa kazi ......tarakuri ......

...ongeza na yule mbunge aliyefukuzwa,ilikuwa ndo siku Tanganyika ikishona chipi ya muungano...
 
Wazanzibar si kama Wabara. Kuipigia kura ya ndo Katiba inayopendekezwa kwanza wakatae ya kwao. Nani yuko tayari kufanya hilo. Naamini hata Dr. Sheini hayuko tayari!.
 
Wakati Tanganyika inaimeza Zanzibar mwanasheria mkuu wa mwaka 1964 Dourado alitimuliwa , sasa Tanganyika imesababisha tena Othman kufukuzwa .......
Wametimuana wenyewe usiisingizie Tanganyika ambayo ni marehemu kwa sasa.
 
Atamwapisha kwa njia ya simu kama wanaweza kupiga kura za sms watashindwa mwapisha .....

Nchi inayoongozwa na majuha kila jambo linawezekana hata kama sheria haziruhusu zitafanyiwa utaratibu wa kupindishwa ili mambo yaende hata kama wataangamia kwenye shimoni!!!!!Ajabu na kweli.
 
Ataapishwa kwa njia ya fax 📠 ccm wakiamua jambo wanashindwa?
 
Habari nilizogusiwa juu juu tu ,kumbe Dr Shein amemteua Mwanasheria Mkuu Mpya wakati mwanasheria huyo hayupo nchini ,yupo majuu na huenda alijiripua huko japo alikuwa ni chini ya Mwanasheria alieondoshwa ,alikimbia mapema baada ya kuona kuna mtikisiko katika bunge la Katiba na haswa baada ya Othman kukacha kuhudhuria.
Hizo ni tetesi tu kuwa jamaa hayupo nchini na hakuna tamaa ya kurudi tena Zanzibar ,ila kama kuna mwenye uhakika kuwa yupo si vibaya akanisahihisha.

tusubirini tu sasahivi atataja mwingine kukaimu.. NISHIDAAA!!!!!
 
Kwi kwi kwi kwi lol!!!! Hata kazi zake atafanya kwa njia ya simu huku akiendelea kuishi majuu! Only in Tanzania pwagu na pwaguzi's country.

sasa hivi wizara ya mawasiliano,sayansi na teknolojia imeanzisha mfumo wa video conference,lets hope so, atatumia hii tecno mpya hapa tanganyika maana zenj bado inafungwa
 
taarifa ipo juujuu tuu, mtoa taarifa inaelekea nae ni walewale wenye nia ya kumuombea mtu mabaya tuu kwa maslahi binafsi.

We unajua huko nje kafuata nini? Nani kakwambia hatorudi.
Asiporudi kwani atakosekana mtu wa sheria kujaza hiyo nafasi?

wacha unafiq

acha ubazazi soma msg vizuri.. Mbwam weee
 
Mtoa mada kaanza kwa kusema 'habari alizozipata juu juu, kisha kamalizia kwa kusema hizi ni tetesi' Sasa nashauri wote mliokusanyika mtandaoni kujadili umbeya huu tawanyikeni mkafanye shughuli za maendeleo acheni kupotezewa muda sababu muda ni mali.

Hata mbuyu ulianza kama mchicha, tetesi nyingi tu humu baadaye zilithibitika kuwa ni kweli. Mfn wa kutimuliwa kazi Mwanasheria wa Zenji, zilianza kama tetezi wakati hajaenda kupiga kura yake na nilimsikia mnafiki sana Sita anakanusha, baadaye ikawa kweli. Kwa hiyo tujipe muda.
 
hapo chini weka mwaka 2014 wakati Tanganyika ikishona suruali ya muungano baada ya kuvaa koti tupu kwa miaka 50 mwanasheria mkuu Othman Masoud amefukuzwa kazi
 
Msaidizi wote ni sawa ..wote ni wanafunzi wake Abubakar Khamis wote wasomi .wasomi znz na ccm ni ncha mbili hazigusani .
Kwani ccm znz hawataki hoja wao kwao ni Tanganyika kuwalinda kwa gharama yoyote watawale wao na watoto wao....
 
[h=1]Mtoto wa Aliyekuwa ‘Haini’ Ateuliwa kuwa AG[/h] Written by abdisalum


Inashangaza sana kuona uteuzi kama huu umepitishwa na SMZ, serikali ambayo imeshikilia mrengo mkali sana wa kimuhafidhina wa kutokukubali mabadiliko.
Said Hassan Said, ameteuliwa kuwa Mwanasheria Mkuu wa SMZ.
Huyu ni mtoto wa Bwana Hassan Said Mzee (ex-comrade) na aliwahi kushtakiwa au kuhusishwa na kesi ya uhaini ya kumuuwa Mzee Karume, Rais wa kwanza wa Zanzibar.
Nakumbuka kati ya watu walioteswa vibaya sana pale kwa ‘Ba-mkwe’ chumba cha mateso Zanzibar alikuwa huyu Bwana Hassan Said Mzee, Hashil Seif (comrade, former Navy officer) na Shafi Adam Shafi (watu wengi tulidhani wakati huo kuwa hawa wameshakufa kw amateso waliyoyapata). Uhai uko kwa Allah sio kwa Mandera (mtesaji).
Katika mifumo ya ajira v.s security (vetting) ya kidunia na hapa Zanzibar hususan, mtu kama huyu huwezi kumpa nafasi kama hii kubwa na nyeti.
Tuseme leo AG wetu mpya akiamua kupekua mafaili ya huko nyuma — na akaona mambo juu ya mambo na vijambo — itakuaje?
Kuna kesi mbili ttau ninazijuua Tanzania/na Zanzibar kuwa ajira fulani fulani zilifutwa just kwa sababu ya uhusiano wa baba/na mwana katika kesi hii ya uhaini ua kumuuwa Mzee Karume (mmoja amekosa Urais….! na mmoja amekosa Urubani wa ndege ya Rais…n.k n.k) na nyingine nyingi.
Vipi wengine wakoseshwe na wengine wapatiwe???
Najua kuwa Bwana Hassan Said, Mzee wake huyu AG mpya alikuwa comrade, na mpinzani wa dhahir then chini kwa chini; lakini baadaye alibadilika na kuwa pro-system na kufikia kuwa kamishna wa tume ya uchaguzi ya mwanzo ya Zanzibar chini ya Dr.Salmin Amour.
Huenda ikawa hii ni bahshish yake ya matokeo ya uchaguzi ya mwaka 1995. …….you scratch my back….Ashak malizia hapa…….mie sijui kizungu mwanangu weeee’…wenzetu wengine wanasema ‘nipe-nikupe, wengine wanasema ‘ihsani inalipwa kwa ihsani…..wengine ni quid pro quo…….wengine /fadhila …..min fadhilikya……
— tuipokeee katiba mpya kwa mbwemwbe zote ——
Ehhh na vipi ile ibara inayosema kuwa Rais wa Jamhuri ya Mungano wa TZ ndiye atayeteuwa Wakuu wa Mikoa Zbar, ina maana mpaka masheha, maana technically, RC ndiye anayeteuwa masheha hapa kwetu. Je akama aRais wa TZ atateuwa Bwana Rweikiza kutoka Ngara, Kagera, kama ‘anavyoona yeye inafaa’ na masheha pia wataoka huko huko kwa sababu na yeye RC ataona ‘hao wa kwao ndio wanaofaa’ wale akina Vuai, Ame, Simai, jecha na askari wastaafu basi tena….au vipi jamani??
Ashak hebu nisaidie translation ya ibara hii.
Na ile kuwa Rasimu hii inatambua JWTZ na Polisi na JKT tu, vikosi vyetu vya SMZ hamna mle, itakuaje????? Je, tuvivunje vikosi vyetu vya SMZ? Almuradi utamu juu ya utamu mwaka huu??
 
Atamwapisha kwa njia ya simu kama wanaweza kupiga kura za sms watashindwa mwapisha .....
Nimechake saaana. Wanaweza pia kwa Tango na Whattsup! Nchi hii kinachoshindikana ni umasikini tu.
 
hii nayo ni ya kujadili? pambaaaaavu akili za Watz. vipi Maalim Seif kisha jiuzulu?
 
Back
Top Bottom