Mwanamke wa kitanga

Mwanamke wa kitanga

mahirtwahir

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2013
Posts
614
Reaction score
322
Habari wana MMU

Natumai hamujambo
Kuna mdogo wangu ameanzisha mahusiano na mtoto wa KITANGA kwa kweli anampenda kupita maelezo na lengo ni kufunga nae ndoa haraka iwezekanavyo. Kiuwezo ameshajipanga na kila kitu juu ya harusi yake na huyu bint.

Tatizo linakuja kwa wazazi wake mwanaume hawataki mtoto wao amuowe MTANGA kwa kuamini kua Tanga ushirikina umetawala ukiowa kabila hilo lazima usahau kwenu uwatese ndugu zako si kwa kuwa wako juu kimapenzi tuuuu ila wanaamini kua mapenzi ya Tanga ni ushirikina lazima mwanaume uzibitiwe kisawa sawa.

Jamani ivyo haya maelezo ni ya kweli?
Pia jeee tabia za wanawake hawa ziko vipi ili nipate nafasi ya kumshauri mdogo wangu huyu.

Msaada wenu ni muhimu wana bodi
 
Asisikilize maneno, mazuri na mapungufu ya mwenzie ni yeye ndo anayajua....
 
Sio vyema kuhukumu kabila kwa kosa la watu wachache, mimi ninacho shauri kama wamependana acha waoane. Kuwa mdigo, mzigua, mbondei, msambaa, mshombe, mhandeni haijalishi.
 
haya mambo yamepitwa na wakati jamani,uchawi ni tabia ya mtu na sio kabila
 
Asisikilize maneno, mazuri na mapungufu ya mwenzie ni yeye ndo anayajua....

Evelyn Salt nadhani unaelewa kabisa kuwa wakati wa uchumba huwa tunapigwa upofu kwenye kuona mapungufu..kwahiyo, experience/ ushauri wa wazee usipuuzwe..wazeewetu wameona mengi
 
Hivi lini tutasifiwa wanawake wa kingoni, tanga tanga kila siku..

Swala ni kwamba uchawi ni imani sio kabila
 
Evelyn Salt nadhani unaelewa kabisa kuwa wakati wa uchumba huwa tunapigwa upofu kwenye kuona mapungufu..kwahiyo, experience/ ushauri wa wazee usipuuzwe..wazeewetu wameona mengi

Ushauri Sikiliza lakini cha kuchukua chukua cha kuacha acha....
 
Unamaanisha nini, mbona kama unataka kujibagua au kuulizwa swali. usiwe msaliti

Nimeona watu wajumlisha tu eti "Mtanga" ni kabila nikaona nitoe elimu kidogo kuwa tupo makabila mengi. Haya huo usaliti waja kivipi? Ningetaka kusaliti ndugu zangu si ningesha jitetea na hilo kabila unalohisi najaribu kujitenga nalo? Mbona kama vile wajishuku?
 
Mtakuwa wapare ninyi.Baadhi ya koo za kipare huwa wana hiyo imani(nadhani bado inaendelea) kuwa ni mwiko kuoa Tanga hasa wadigo kwa sababu hizohizo ambazo umezitaja hapo juu.
 
huyu ni mtu mzima inatakiwa awe na msimamo kama wanapendana kwa dhati aoe tu
 
Back
Top Bottom