Mwanamke kudaia arudishe pesa

Mwanamke kudaia arudishe pesa

Emc2

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2011
Posts
16,808
Reaction score
16,951
Nawasalimia wana JF

Stori ya kweli
Kuna rafiki yangu (Mimi mwanaume na yeye pia) nimesoma naye shule ya msingi tume kuwa karibu nae sana.

Sasa mambo yenyewe ni kama ifuatavyo:-

Alinieleza walikutana na msichana na akatokea kumpenda, basi akaomba no ya simu na yule msichana akampa.
Basi walianza mawasiliano ya hapa na pale. Baada ya mda alimuuliza huyo msichana kama yuko na mtu, msichana akasema yuko pekee yake (Single). Basi jamaa akatupa karata yake.

Yule msichana akasema yeye ameokoka na anapenda kuenenda katika mapenzi ya kimungu.
Basi rafiki yangu alifurahi sana kukutana na huyo binti, akauliza wapi anakosali, bila kusita msichana akaeleza anasali wapi.

Jumapili moja jamaa yangu akaibukia kanisani na kuona kweli anasali pale, akamtamburisha kwa baadhi ya ndugu zake.

Baada ya muda fulani yule binti akaaza kuwa anaomba pesa. Ok bila kusita jamaa akawa anampa hizo pesa (mara anataka kusuka, anataka kununua viatu, hela ya chakula cha mchana na mengine). "Huyu dada amesoma na ana digrii pia anafanya kazi"

Baada ya muda huyo msichana akaanza kubadilika, walikua wanawasiliana WhatsApp msichana akawa hatoi ushirikiano.

Baada ya muda fulani msichana akablock namba ya huyu rafiki yangu kwa hiyo akawa hawezi tena kuwasiliana naye kwenye simu. Ila alikuwa na simu nyingine akipiga haipokelewi.

Jamaa akawa haelewi nini tatizo, akajaribu kuongea na dada yake, dada yake akasema hatayeye hajui. Basi akajaribu kumuomba waonane waongee, yaani hakutaka kabisa kuonana nae.

Basi siku moja msichana akapiga akasema "Sitaki mawasiliano na wewe". Heee jamaa haelewi nini tatizo.

Baada ya siku moja akapigiwa na mwanaume akisema mimi ndie mpenzi wa huyu msichana mbona unamsumbua.


Kwa kufupisha stori jamaa ameamua arudishiwe pesa zake. Na kwakua msichana hataki kuonana nae, jamaa katinga kwa wazazi wa msichana(Ni wacha Mungu) wameahidi watamrudishia.

Hivi kweli ni sahihi alichofanya huyu jamaa yangu?

Nawasilisha hoja.
 
Mods naomba mbadilisheni heading ni kudaiwa badala ya kudaia
 
Jamaa wa wapi huyo? Bila shaka ni Muha huyo mkaka
 
Kwani alipokuwa anampa kulikuwa na kubaliano yoyote

1.anampa fedha ili wawasiliane
2.anampa pesa kwamba atakuwa mpenziwe
3.anampa fedha kama mkopo.

Kama yote matatu hapo juu hayapo basi alimpa pesa kwakuwa alimwomba tu na yeye aliona ndio njia pekee ya kumpata kwakuwa ni mlokole na ana shida ya hela ALICHOFANYA RAFIKI YAKO SIO SAHIHI
 
I sawa kabisa, maana huyo msichana kajifanya mtoto wa mjini acha na mwenzake pia aonyeshe ya kuwa anaweza react kwa kiwango chake. Hiyo itampunguzia machungu kiasi huyo rafiki yako.

N.B : Though mimi siwezi kufanya huo ukauzu alioufanya jamaa.
 
mmhhh jamani wanaume mmeumbwa na koromeo la nini kama hata uvumilivu hakuna , hivi alimpenda kweli huyo binti au ndo zile nakupa nikikupata utajuutaaaaaaa na kulipia,

kama alitoa kwa mapenzi hakuna mkataba wa maandishi wa kurudishiana hapo, awe tu mstaarabu na kwanza ameenda kwa wazazi wa binti kama nani, alishakua officially mchumba au ndo dharau tu kwa wazazi wa mabinti
 
Jamani hata kama sio sahihi its too late hata tukishauri yeshatokea
 
Mi ndio maana sitaki kabisa mambo ya kuomba omba pesa ya mwanaume..!

Mdada una kazi yako unaendekeza kuomba omba..! Mmmh..!

Sio kazi tu tena bado anaishi nyumbani kwao. (Hana matumizi mengi)
 
Kwani alipokuwa anampa kulikuwa na kubaliano yoyote

1.anampa fedha ili wawasiliane
2.anampa pesa kwamba atakuwa mpenziwe
3.anampa fedha kama mkopo.

Kama yote matatu hapo juu hayapo basi alimpa pesa kwakuwa alimwomba tu na yeye aliona ndio njia pekee ya kumpata kwakuwa ni mlokole na ana shida ya hela ALICHOFANYA RAFIKI YAKO SIO SAHIHI

Mkuu ukisoma maelezo ya jamaa ni kwamba walikubaliana kuwa wapenzi, na msichana akamwambia hayuko tayari kutoa papuchi mpaka watakapoidhinishwa, Ghafla msichana kabadilika na kumtosa jamaa, kama ni wewe ndio mwanamume utafurahia kufanywa zoba.? Yaani hapo kama ni mahakamani hakimu angesoma hukumu ya namna hii:
"kwa kuwa mwanamke huyu alitumia ulaghai ili ajipatie pesa za matumizi toka kwa mwanamume huyu, namhukumu huyu mwanamke kulipa faini na gharama za mwanamume ili iwe fundisho kwake na kwa watu wa aina yake. "
 
Hahaa I cant imagine the look of har parents!!!!!

kwani walikubaliana nini,hizo pesa alikopa si alitoa mwenyewe
hamna haja hata ya kudai ati
 
mpenzi sio mume na hana haki popote , hata uchumba hajafikia anakuja kulialia hapa atupishe
 
umekula vya kwangu, utanibeba leo
kanunua simu kampa dem, walivyoachana kampokonya
jamani tuwe tunaangalia wanaume wa kudate nao lol
 
Why can"t your friend consider the cash given as tax deductible for the service rendered?
 
Hahaa I cant imagine the look of har parents!!!!!

kwani walikubaliana nini,hizo pesa alikopa si alitoa mwenyewe
hamna haja hata ya kudai ati

Heaven on earth Nadhani hujasoma vizuri. Hebu jaribu kusoma na utafakari. Mimi sikuwa na comment zaidi ya kusema dah!!
 
Last edited by a moderator:
mmhhh jamani wanaume mmeumbwa na koromeo la nini kama hata uvumilivu hakuna , hivi alimpenda kweli huyo binti au ndo zile nakupa nikikupata utajuutaaaaaaa na kulipia,

kama alitoa kwa mapenzi hakuna mkataba wa maandishi wa kurudishiana hapo, awe tu mstaarabu na kwanza ameenda kwa wazazi wa binti kama nani, alishakua officially mchumba au ndo dharau tu kwa wazazi wa mabinti

Ndio akome kuishi kwa kuombaomba na ajifunze kuheshimu mahusiano, wewe unaona alichokifanya huyo mwanamke mwenzenu ni sawa.? Hapo tayari fedheha imekwishawakuta ndugu zake na wazazi wake.

Wamekwishatambulishana mpaka kutambulishana kwa ndugu, halafu anakuja kukiuka makubaliano waliyowekeana, wewe unadhani ni sawa.?
 
umekula vya kwangu, utanibeba leo
kanunua simu kampa dem, walivyoachana kampokonya
jamani tuwe tunaangalia wanaume wa kudate nao lol
Halafu jamaa hata gezaulole hakupewa. Kama wewe inakuaje?
 
Back
Top Bottom