Mwanamke kamkataa mtoto wangu

Mwanamke kamkataa mtoto wangu

Molembe

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2012
Posts
9,932
Reaction score
11,852
Mtoto wangu wa kwanza ana miaka 8 nilimpata nikiwa mwaka 2 chuo ambapo kutokana na mamake kutokuwa mvumilivu kunisubiria nimalize kusoma aliamua kuolewa na kumuacha nyumbani kwao mtoto, nilipohitimu chuo na baada ya kupata kazi niliamua kumtafuta mwenza wa kuoa ambapo kabla ya yote nilimwambia ukweli kuwa nina mtoto na yeye akakubali atamlea lakini mara baada ya ndoa akanigeuka hataki kumuona mtoto huyo na kule anakokaa mtoto wanataka nimchukue.

Nimetumia kila njia imeshindikana msimamo wake ni hataki kumlea mtoto wa mwanamke mwingine, nifanyeje hapa wakuu maana nikilazimisha (uwezo huo ninao) anaweza kuwa anamtesa mtoto kipindi sipo akamsababishia matatizo ikitegemea huwa nasafiri mara kwa mara na sikai nyumbani sana na kuvunja ndoa siwezi maana ni ya kanisani na tayari tuna watoto
wengine wawili.

Ushauri wakuu
 
Duh, kiubinadam ni ngumu sana kulea mtoto wa kambo coz ankakukumbusha maovu ya mwezi wako aliyoyafanya nyuma. Ni bora umtafute mjane yeyote anayeishi peke ake au na watoto wake tu umlipe hela akusaidie kulea.

.. Kumleta hapo will tear apart your wife, you and even that 'boy'... Ni ngumu sana kuishi na mtoto wa nje kama una roho ndogo. Tafuta mtu ambaye hana collision of interest. hata kama ni ndugu yako, mlipe akulelee mtoto. It will help both of you...
 
Wahenga walituasa "mchawi mpe mtoto wako akulelee". Chukua mtoto wako mlete nyumbani umlee. Kikubwa ni kuwa makini kufatiria kama hanyanyaswi ki- jinsia. Huyo mkeo hana mapenzi na wewe kuwa nae makini. Watu wengi huwatumia watoto wa wenza wao kama ngao au sumaku ya kuvuta mapenzi ya wenza wao.
 
Wahenga walituasa "mchawi mpe mtoto wako akulelee". Chukua mtoto wako mlete nyumbani umlee. Kikubwa ni kuwa makini kufatiria kama hanyanyaswi ki- jinsia. Huyo mkeo hana mapenzi na wewe kuwa nae makini. Watu wengi huwatumia watoto wa wenza wao kama ngao au sumaku ya kuvuta mapenzi ya wenza wao.

Nimeshuhudia mama kambo akimnyanyasa mtoto naogopa sana sipendi mtoto anyanyaswe muda mwingi sipo nyumbani nasafiri mara kwa mara.
 
unless kuna jamboa mbalo wewe hujaliweka wazi mand that is the fact...............ni ngumu sana nkwa mke wa ndoa kumkataa mtoto alomkuta kazaliwa na mkubwa kuliko umri wake wa yy kuwa nkwenye ndoa..............possiblity kubwa ni kwamba hukumwambia na sasa umekuja kutaka ubabe kumleta nyumban, ama ulimwambia lkn si kwa njia sahihi ya kumwabilia.

chunga isije ikawa umemtuma dada yako kumfikishia ujumbe kwamba une mtt na unataka kumleta aish na wewe, ama pia inawezekana mmesha msema sana huyo mama juu ya huyo mtoto kiasi kwamba najua akikubali ndo atakuwa amejipalia makaa ya moto.

kuna scenario unakuta dada wa mwanaume wanajua kaka yao ana mtt nje afu awa madada wanaanza kusema mara ooh ukimleta home kwako mkeo atamtesa, mara ooh mkeo ana roho mbaya sana atamtesa sasa ata kama mkeo alikuwa anajua ila kwa hizi bhr unafkir atamkubali??

cha kufanya mchukue mpeleke kwa mama yako mzazi kama hayuko rudi nikupe ushauri mwingine ila mwache mkeo afurahie ndoa yake...................

ukitaka jibu zuri zaid mpe mkeo huu uzi ausome afu mruhusu atoe yake ya moyoni hapa tutakushauri kisawasawa
 
achana na huyo mwanamke hakufai

acha kuwa too judgmental ivi umewaza kwamba hii ni one side ya story?
ivi mbona huyu hajasema ukweli wake wote kwamba alitumia approach gani kumwambia mkewe kuwa ana mtt?
mbona hajasema ndg zake walisemaje soon alipooa na akasema anataka akae na huyu mtoto?
unaijua nguvu ya ndg wa mume wewe??
ampe mkewe huu uzi ausome afu mke ajisee na yeyey ya kwake ya moyon ndipo sasa tuwashauri wote
 
Mpe option hii, mtoto aje nyumbani au yeye aondoke....achague moja hapo....then msikilizie atajibu nini...mwanaume lazima uwe na msimamo kaka.

hana option ya kutoa aseme ukweli tatizo limetokana na nini??
mkewe hawez kukurupuka tuu kumkataa mtt alomkuta ndoan
 
Tafuta namna yakumlea huyo mwanao nje ya familia yako,.ukitumia mbavu utajuta nduguyangu,.kumbuka upendo haulazimishwi kama huyo mama kamkataa kafanya vizuri kukuonyesha hisia zake vinginevyo angemdhuru,.

Nahuyo mtoto anataka malezi sio kuishi kwako so kumlazimisha mkeo amlee hatompa malezi kama unavyotaraji..
 
Muambie mkeo unahama hapo ukatafute nyumba ukae na mwanao. Yeye mtakuwa mnatembeleana kama mtu na bf wake. gfsonwin, namaanisha hapo sio utani. Hivi wewe kama mtu kakukuta na mwanao na mnaoana anajua huyo ni mwanao. Then anakuambia simtaki huyu mtoto ungefanyaje? I would have done exactly that
 
Last edited by a moderator:
Ngumu ila kama kuna uwezekano wa kukaa huko huko na kuyaboresha maisha yaje huko ni vema akaishi aliko sasa maana huyo mwanamke anaweza kulazimika kumchukua lakini ukaishia kujuta tu.
 
acha kuwa too judgmental ivi umewaza kwamba hii ni one side ya story?
ivi mbona huyu hajasema ukweli wake wote kwamba alitumia approach gani kumwambia mkewe kuwa ana mtt?
mbona hajasema ndg zake walisemaje soon alipooa na akasema anataka akae na huyu mtoto?
unaijua nguvu ya ndg wa mume wewe??
ampe mkewe huu uzi ausome afu mke ajisee na yeyey ya kwake ya moyon ndipo sasa tuwashauri wote

Nilimwambia mapema kabisa kuwa nina mtoto hata kabla ya ndoa tungali wapenzi na tukawa tunamtembelea mtoto tukiwa wote lakini baada ya ndoa akasema hawezi kulea mtoto wa mwanamke mwingine cha ajabu kuna mtoto wa dadangu nakaa nae anaishi nae vizuri tu nongwa inakuwa kwa huyu wangu.
 
Muambie mkeo unahama hapo ukatafute nyumba ukae na mwanao. Yeye mtakuwa mnatembeleana kama mtu na bf wake. gfsonwin, namaanisha hapo sio utani. Hivi wewe kama mtu kakukuta na mwanao na mnaoana anajua huyo ni mwanao. Then anakuambia simtaki huyu mtoto ungefanyaje? I would have done exactly that
King'asti sitak kuamin na wewe unawea kujudge situation kama hii kwa habari za one side............mtoa mada atuambie ukweli kwann huyu mkewe amkatae huyu mtoto...............
hajatuambia mazingira ya kumpatia habari huyo bibie juu ya huyo mtoto yalikuwaje?
je ndg zake hasa madada bada ya kujua kaka yao anaoa mke mwingine walisemaje juu ya huyu mtoto? umesahau kwamba uwezekano wa huyu mkewe kuwa vindicated na kauli za wakwe kwamba atamtesa huyo mtoto ni mkubwa?

nakuambia true story from my blood brother yeye alimkana mwane wa kumzaa kanisan kwan hakuwa amemwambia binti (mke mtarajiwa juu ya huyo wa mashtuzi), sasa ikaja eti akenda kunywa pombe siku moja zikamkolea kisawasawa akarudi home akabreak the cord eti nina mtoto nilimzaab4 na sikutaka kukiri kanisan kwan ingekuwa ni hbr ya kukushtua as nilikuwa sijakwambia..............bibie akamwambia poa just like that

bro akatoka akaenda kwa sista angu mkubwa akammwambia sijui anamtoto so yy sista awe anatake all efforts za huyo kid ili aje home sista naye akaanza kufanya mambo kwa akili za kuendeshwa, na ile dhana mama wa kambo sio mama.

bro akanifuata mimi na hubby akaomba mtoto aje akae kwangu hubby akasema hapana akanipa reason ivi kama ni mwane na mkewe yupo wewe kukaa na huyo mtoto huon kama unajenga hatered kati ya mm na mama?? ivi ipo siku utaweza kutoka wewe na wanao mnakwenda kwa bro?? nilipojitafakari nikaona hapana nikamjibu tu hapana uyo mtoto mpeleke kwa mkeo. Kumbe nayy kashapewadesa baya na sista mkubwa kwamba mkewe atamtesa ile mentality ikaanza kumtafuna huku na huko mkewe siku moja tumekwenda kwake alikuwa mzazi. sister akaja na yule mtoto wa bro, wifi akaualiza kiutan manake ukweli hakuwa anajua uyo mtoto ni nai akasema na huyu ni nani??

sister akasema kwan huyu humjui?? mbona huyu ni mwanao kaka yake na mwanao wewe G? wifi yuko ooh!! just like that
mwaka jana bro akasema sas anamleta B hapa home akaena G mkewe akamwambia tafuta pa kumpeleka niakmsapoti wifi yangu kwani bro toka mwanzo kesha kosea approach.............

  • kwanza kwann asingemweleza mkewe ka utaratibu sahihi hata kama kuna kosa tayari??


  • pili kwann binti wa watiu achafuliwe na kauli za mama wa kambo mbaya b4 hata kumuona mtoto ivi akija kuish nae si ndoa ataambiwa anamlisha mavi kbs?


  • tatu ivi kwann mwanaume usubiri adi watu wa kusaidie kukutatulia matatizo ya home kwako?? uwe basi mwanaume ureason kiume


  • nne ivi je unafkir kwa kauli kwamba atamtesa mtoto huyo mtoto atakuja amejihami kiasi gani??
ngoja nikapikie wanangu narudi baadae kidogo but ukweli mie na side na huyu mama kwani nimeliona jambo kama hili kwa kaka yangu ama pengine ni wewe Molembe lol!!
 
Last edited by a moderator:
Nilimwambia mapema kabisa kuwa nina mtoto hata kabla ya ndoa tungali wapenzi na tukawa tunamtembelea mtoto tukiwa wote lakini baada ya ndoa akasema hawezi kulea mtoto wa mwanamke mwingine cha ajabu kuna mtoto wa dadangu nakaa nae anaishi nae vizuri tu nongwa inakuwa kwa huyu wangu.
sasa niambie vipi je hakuna maneno yyte yanayozunguka kwamba mkeo ni mtesi wa mtoto asokuwa wake?
huyo unayekaa nae mama zake wengine hawasemi vibaya?? kumbuka inaweekana kabisa anasemwa afu wewe hujui na yy hatak kukwambia na ndo mana hatak kujiongeea mzigo wa matatizo

usisahau kwamba maneno ya nje yanauma sana hasa kwa mtu ambaye anakuwa natenda iliyo haki.............chunguza ndg zako juu ya mkeo
 
Nahisi gfsonwin hujanielewa mimi niliweka mambo wazi mapema kabisa enzi mapenzi na hata kumtembelea mtoto tukiwa na bibie tatizo limeanza baada ya ndoa.
 
Last edited by a moderator:
sasa niambie vipi je hakuna maneno yyte yanayozunguka kwamba mkeo ni mtesi wa mtoto asokuwa wake?
huyo unayekaa nae mama zake wengine hawasemi vibaya?? kumbuka inaweekana kabisa anasemwa afu wewe hujui na yy hatak kukwambia na ndo mana hatak kujiongeea mzigo wa matatizo

usisahau kwamba maneno ya nje yanauma sana hasa kwa mtu ambaye anakuwa natenda iliyo haki.............chunguza ndg zako juu ya mkeo

Ndugu zangu hawana matatizo na sijawahi kuyaona halafu huyu mwanamke anampenda huyu mtoto wa dadangu sana na wako karibu sana na huyo dadangu kuhusu ugomvi wa familia haupo kabisa.
 
Sikiliza,ndugu yako ni mtoto na si mkeo,ndoa ya kanisani ni bora kuliko mwanao?
Chukua mwanao ukae nae,hataki aondoke yeye akuachie watoto wako,utatafuta hata hg akuangalizie watoto.
Kwanza dogo mkubwa hyo,lini atapata mapenzi toka kwako,baadae atakukana hyo kwamba hukumlea.
Wanawake wapo tu,lakini huwezi jua hyo mwanao mola kampangia riziki gani.
 
Back
Top Bottom