Mwanamke huyu tumueleweje

Mwanamke huyu tumueleweje

Weza

Senior Member
Joined
Oct 24, 2013
Posts
118
Reaction score
78
Tokea aolewe kwa ndoa na mumewe hata miaka miwili haijapita, kabla alikua yuko poa tu kwenye uchumba japo yalikua mapenzi ya mabali wanakutana kipindi cha likizo au kutembeleana, baada ya kuoana mwanaume kafanya mbinu zote akamuhamishia mke mjini ili awe karibu na yeye na mke kamkuta kaka akiwa na nyumba zake nne tayari na magari mawili akaona isiwe shida akamunulia na mkewe gari ya kwake maana mke alidai anataka gari yake binafsi na ana choice ya gari sio hizo za jamaa.

Jamaa akanunua, wakajaliwa watoto mtoto mmoja, ila cha kushangaza hata kabla ya mimba mwanamke kila siku analalamia ooh, unakoroma, ooh hujui mapenzi, ooh nikiumwa unaacha ku make love na mimi kwa kisingizio unanihurumia.

Kwenda ukweni kwao mume dada anavaa nusu uchi jamaa kamuomba vaa hata vitenge au khanga sio heshima mke anamwambia kama hunitaki narudi kwetu, mkwe kaona aibu kampa kanga vaa hii mama, basi usiku kucha kalia anataka kuondoka hayo sio maisha, basi wamerudi kwao anahama chumba kila siku analala chumba kingine, hamsemeshi mumue, mume akitoka kwenda hata bar kukutana na friends wake atamfuata huko baa atamtukana na kurukia ngumi makucha mradi ugomvi na pete baada ya miezi mitatu toka wafunge ndoa aliivua kisingizio inambana, kwakifupi anakaribia mwaka hawezi kutoa penzi kwa mumewe mpaka mume ambake, huyu jamaa ni rafiki sana wa kakaangu katuomba ushauri afanye nini na kwasasa mwamke kahama chumba kabisaa, outing hua hakubali kutoka na mumewe wala kwenye harusi wala sherehe yeyote. Ushauri

ushauri wenu wadau huyu kaka afanye nini? Maana kajitahidi kufanya kila njia ku mplease mkewe lakini wapi, mshahara wa mke hua hawezi nunua hata nyaya na mume hua hamuulizi, mafuta ya gari ni mume anamuwekea, pesa ya saloon ni mume, nguo na matumizi yote ni mume ila huyo dada hata chumvi hawezi nunua kwa pesa yake mpaka mume arudi, ushauri watu wangu.
 
Jaman hili nalo la kuuliza?? Kwan moyo wake unaaman kuendelea kuishi na mwanamke kama huyu?

Unataka kutuambia kuwa huyo jamaa ameshindwa kabisa nn afanye kwa mwanamke wa aina hyo??
 
mmh ngumu kufanya maamuzi hapa, huyo mwanamke wa aina gani , wengi wetu wakorofi tukichokozwa, ye hata hajachokozwa
 
huyu kaka amwache tu ili ajifunze ila ahakikishe matumizi ya mtoto anampa huyo mtoto that all .... ndoa isiwe kero au ugonjwa ya nini kumlazimisha mtu kujiheshimu ... ili limwanamke pumbafu kabisa jinga sana....... unaamua kuamsha timbirwi tu ndani ya nyumba kuna binadamu uwepo wao wa kufikiri mfupi mno/..... kama hajui mapenzi alikubali ya nini kuolewa nae ...
 
He sasa wataka ushauri gani kwa vituko hivyo piga chini fasta, kunguru hafugiki
 
Sasa ushauri wa nini.....
Ikikushinda ndoa si unatoka?
 
Hahahaa...ilibidi upitie kwanza ili kujua kma wasomaji wataielewa kwa urahisi. Ila
1. Amkanye...asipobadilika
2. Aende kwa wazee waweze kusawazisha...akiendelea
3. Talaka ndo suluhisho ya hayo yote
 
Back
Top Bottom