Judgement
JF-Expert Member
- Nov 13, 2011
- 10,327
- 4,779
Ninachokisema hapa ni serious na naomba comments also seriously! Nina mpenzi wangu nampenda kw dhati, kadhalika kiasi flani nashawishika kuamini nae ananipenda kufatana na mambo flaniflani niyaonayo kwake, moja kubwa linalonifanya nizidikua nae krb ni vl ambavyo amekua si tegemezi kwangu, kwani ameajiriwa. Mimi humpa fund kama za vocha pale ninapojisikia na mara chache hutokea akaniomba pesa au kitu, hatuishi nyumba moja yeye anaishi kwao nami kwangu. TATIZO LANGU NI HILI :- Bibie huyu ni mlevi japo si mlevi (cha pombe) aliepindukia laa, lakini ieleweke kwmb yeye ni mnywaji wkt mimi situmii pombe, nilikua mnywaji lakini takriban nina miaka mitano hv tangu nimeacha pombe, hivyo ndiyo kusema mazingira yote ya ulevini nayajua! Binti huyu ana mashosti wake wawili ambao ndy mara kw mara anakunywa nao, mmoja kt ya hao rafikize tabia zake c nzuri anabadili mabwana km hana akili nzr! Nimejaribu mara kadhaa kumnasihi kwanza aachane na ulevi ambao utampelekea pia kutengana na group la marafiki wale japokua yule rafiki yake wa pili hadi hv cjafanikiwa kujua tabia zake nje ya ulevi. Kinachonikwaza ni pale napokua mi niko hom kitandani natafuta usingizi yawezakua mida ya saa 5- 6 -7 usiku nikimpigia akipokea tu nasikia sauti ama ya Tv au muziki mkubwa ambapo kwao anapoishi hakuna umeme! Nikimwuuliza uko wp? Jibu niko Bar. Kesho yake tukionana nikianza kumlamikia kwmb mimi sipendelei yeye kua klabu hadi mida hiyo na uwezekano wa kupata mwanaume kiulevi unakua mkubwa, yeye hunijibu kw kujiamini kwmb ana uhakika anai'control pombe na hawezi toka na mwanaume. Aidha sijawahi kumfumania lakini je? Mwanamke huyu ananifaa niendelee kua nae?