Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,809
- 15,438
Mara nyingi nimekuwa nikikutana na wanawake walio katika ndoa ambao hujuta sana na kusema kwamba wanajuta kuolewa na laiti wangejua kwamba maisha ya ndoa yako namna hiyo, katu wasingeolewa na wakati mwingine hukumbuka maisha yao kabla ya kuolewa jinsi yalivyokuwa mazuri na ya amani kuliko ilivyo sasa baada ya kuolewa
Lakini pia nimekuwa nikikutana na wadada walio single ambao wanayatamani sana maisha ya ndoa. Umri umekwenda na wamekata tamaa na wanatamani hata ajitokeze mwanaume yeyote yule amtamkie kumuoa ili mradi tu na yeye aingie katika orodha ya wanandoa.
Jambo hili limekuwa likinitatiza sana.
Walio ndani wanatamani kutoka na walio nje wanatamani kuingia. Je hii taasisi ya ndoa mbona imekuwa kizungumkuti hivi?
Naomba wanawake mnipe uzoefu wenu katika jambo hili....