MwanaKJJ IJumaa: Kwanini Ni Vigumu Kuamini "Udikteta" Wakisema CHADEMA?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,997
akilizakuambiwa.png
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna msemo wa Kiswahili kwamba Aliyeumwa na nyoka, akiona unyasi anashtuka; msemo huo unafanana maudhui yake na ule wa Kiingereza kuwa Once beaten, twice shy. Misemo yote hii miwili inatukumbusha tu kuwa mtu yeyote aliyefikwa na jambo baya; na hasa jambo ambalo hakulitegemea kabisa basi anakuwa mwoga hasa mazingira yale yale yanapotokea tena kwani anaweza kuhisi jambo lile lile baya linaweza kumtokea tena.

Hili linanikumbusha mojawapo ya michango mikubwa ya Rais Kikwete katika mijadala ya kisiasa na lugha nchini ni pale alipoelezea wakati fulani jambo ambalo lilikuwa kama kichekesho lakini hadi leo limekolea ndani ya hoja za lugha zetu. Ni pale alipowahi kuhutubia huko nyuma na kuwaasa Watanzania kuwa wawe waangalifu kama alivyokuwa Mbayuwayu ambaye alipewa ushauri na ndege Gong’ota na ushauri ule kama angeusikiliza ungekuwa mwisho wake. Kwamba, Mbayuwayu alimuuliza huyo ndege jinsi gani anaweza kutoboa miti kwa midomo yake. Gong’ota akamwambia kuwa inabidi aruke kwa kasi halafu agonge mdomo wake kwenye jiwe mara mbili ndio utakuwa na uwezo wa kutoboa miti. Mbayuwayu akakubali na akaenda kuchukua kasi alipokaribia lile jiwe akajiuliza nini kitamkuta akigonga jiwe; akaona ule ulikuwa ushauri mbaya na hivyo akajisemea “akili za kuambiwa changanya na za kwako”.

Swali langu la leo lina lengo la kujenga hoja tu kwamba huku tunakokwenda kuna watu wanaweza kabisa kutuambia kuwa jinsi ya kutoboa miti ni lazima tugonge midomo yetu kwenye mawe; na wapo ambao kati yetu wako tayari kuanza kuruka kasi na wamejipanga kura kasi kwenda kugonga jiwe ili wawe na uwezo wa kutoboa miti. Swali ni je watachanganya na za kwao?

Kuna watu ambao wanampinga Magufuli na ambao wanaamini kabisa kuwa Magufuli anaunda utawala wa kidikteta na wengine wanatumia hata neno “ufashisti”. Wapo ambao wanasema hivi wakiwa wanaongozwa na misimamo ya ndani kabisa (conviction) na hawafanyi hivi kwa sababu ya siasa. Yawezekana wengi wa hawa ni watu ambao kweli wanasema kwa sababu wanaamini katika wanachokisema. Hawa sina tatizo nao kwani wanaongozwa na imani na misimamo yao.

Kwa wale ambao hawachoki kusoma hoja ndefu UNAWEZA KUSOMA HAPA.
 
Mzee Mwanakijiji, Usipende sana kitu wala kuchukia kitu sana kwani hali hiyo inaweza kukupelekea ushindwe kuwa " Free minded!".

Pia wakati mwingine ni bora ukatulia na kusikiliza wanachosema wengine kuliko kusema wewe, kwani unaposema kwa kawaida unakuwa unarudia jambo ambalo tayari unalijua ndani ya akili yako (liwe sahihi au la!) lakini unapotulia na kusikiliza au kusoma wengine, unakuwa umejitwalia fursa ya kujifunza na kujipa nafasi ya kupata taarifa mpya.
 
akilizakuambiwa.png
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna msemo wa Kiswahili kwamba Aliyeumwa na nyoka, akiona unyasi anashtuka; msemo huo unafanana maudhui yake na ule wa Kiingereza kuwa Once beaten, twice shy. Misemo yote hii miwili inatukumbusha tu kuwa mtu yeyote aliyefikwa na jambo baya; na hasa jambo ambalo hakulitegemea kabisa basi anakuwa mwoga hasa mazingira yale yale yanapotokea tena kwani anaweza kuhisi jambo lile lile baya linaweza kumtokea tena.

Hili linanikumbusha mojawapo ya michango mikubwa ya Rais Kikwete katika mijadala ya kisiasa na lugha nchini ni pale alipoelezea wakati fulani jambo ambalo lilikuwa kama kichekesho lakini hadi leo limekolea ndani ya hoja za lugha zetu. Ni pale alipowahi kuhutubia huko nyuma na kuwaasa Watanzania kuwa wawe waangalifu kama alivyokuwa Mbayuwayu ambaye alipewa ushauri na ndege Gong’ota na ushauri ule kama angeusikiliza ungekuwa mwisho wake. Kwamba, Mbayuwayu alimuuliza huyo ndege jinsi gani anaweza kutoboa miti kwa midomo yake. Gong’ota akamwambia kuwa inabidi aruke kwa kasi halafu agonge mdomo wake kwenye jiwe mara mbili ndio utakuwa na uwezo wa kutoboa miti. Mbayuwayu akakubali na akaenda kuchukua kasi alipokaribia lile jiwe akajiuliza nini kitamkuta akigonga jiwe; akaona ule ulikuwa ushauri mbaya na hivyo akajisemea “akili za kuambiwa changanya na za kwako”.

Swali langu la leo lina lengo la kujenga hoja tu kwamba huku tunakokwenda kuna watu wanaweza kabisa kutuambia kuwa jinsi ya kutoboa miti ni lazima tugonge midomo yetu kwenye mawe; na wapo ambao kati yetu wako tayari kuanza kuruka kasi na wamejipanga kura kasi kwenda kugonga jiwe ili wawe na uwezo wa kutoboa miti. Swali ni je watachanganya na za kwao?

Kuna watu ambao wanampinga Magufuli na ambao wanaamini kabisa kuwa Magufuli anaunda utawala wa kidikteta na wengine wanatumia hata neno “ufashisti”. Wapo ambao wanasema hivi wakiwa wanaongozwa na misimamo ya ndani kabisa (conviction) na hawafanyi hivi kwa sababu ya siasa. Yawezekana wengi wa hawa ni watu ambao kweli wanasema kwa sababu wanaamini katika wanachokisema. Hawa sina tatizo nao kwani wanaongozwa na imani na misimamo yao.

Kwa wale ambao hawachoki kusoma hoja ndefu UNAWEZA KUSOMA HAPA.

Njaa mbaya!
 
Huyu jamaa siku hizi ni kuandika kuhusu chadema tu kama Juliana Shonza. Anashabikia kila kitu anachofanya Magufyli hata km ni ujinga. Amepoteza kabisa ile critical thinking perspective. Kwa Magufuli ni sawa na Mungu kila akifanyacho ni sahihi kwa MM. This is very unfortunate.
 
Mzee Mwanakijiji, Usipende sana kitu wala kuchukia kitu sana kwani hali hiyo inaweza kukupelekea ushindwe kuwa " Free minded!".

Pia wakati mwingine ni bora ukatulia na kusikiliza wanachosema wengine kuliko kusema wewe, kwani unaposema kwa kawaida unakuwa unarudia jambo ambalo tayari unalijua ndani ya akili yako (liwe sahihi au la!) lakini unapotulia na kusikiliza au kusoma wengine, unakuwa umejitwalia fursa ya kujifunza na kujipa nafasi ya kupata taarifa mpya.
Maneno, na ushauri kuntu huu! . Mwenye masikio na asikie! .

Pasco
 
Ni asiyejua tu ambaye haoni katiba na sheria za nchi zinakiukwa!

Ni upuuzi kuendekeza ujinga wa kwa kuwa kasema fulani basi hiyo siyo hoja hata kama ni ukweli unao umma!

Unafiki ni ushetani!
 
Swali langu kwako ni moja tu Mzee Mwanakijiji... honestly speaking, hapa nahitaji busara na weledi wako na wala siulizi kwa unafiki!

SWALI: Je, unadhani utawala wa Rais Magufuli unafuata utawala bora, utawala wa sheria na demokrasia kwa ujumla? Unadhani utawala wa JPM unaheshimu Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo yeye binafsi na walio chini yake waliapa kuilinda?

Nitakushukuru sana, tena sana ili kuniongezea weledi, naomba unijibu with supporting strong examples.
 
Huyu jamaa siku hizi ni kuandika kuhusu chadema tu kama Juliana Shonza. Anashabikia kila kitu anachofanya Magufyli hata km ni ujinga. Amepoteza kabisa ile critical thinking perspective. Kwa Magufuli ni sawa na Mungu kila akifanyacho ni sahihi kwa MM. This is very unfortunate.
Hapa naona unakuja na nadharia za Wachungaji na Maaskofu wapotaka kuhalalisha uovu wao wakisema ...Usiangalie matendo yangu fuata nnacho kwambia na kilichoandikwa kwenye kitabu kitakatifu...wakisahau kua kitabu hiko hiki kimesema kua Imani bila matendo imekufa..!
 
Wakati mwingine mtu huchagua upofu na hivyo basi hujitia upofu, Udikteta wa Chadema Haujustify udiktete wa mzee fulani.
Sasa hivi nchi inakuwa kama police state, wewe umekalia Lowasa nA Chadema
 
Ni ******** na mwendawazimu tu ambaye haoni katiba na sheria za nchi zinakiukwa!

Ni upuuzi kuendekeza ujinga wa kwa kuwa kasema fulani basi hiyo siyo hoja hata kama ni ukweli unao umma!

Unafiki ni ushetani!
Hajasema kua katiba na sheria za nchi hazikiukwi.....alichosema kwa nini tuamini kile wanachokisema CDM, maana baadae wanaweza kuja kutugeuka.... Walituaminisha Lowasa Fisadi kwa maneno yao na watu wakaamini? nini kinasababisha wewe usiamini kua baadae watageuka hiki wanachokisema?
 
Huyu jamaa siku hizi ni kuandika kuhusu chadema tu kama Juliana Shonza. Anashabikia kila kitu anachofanya Magufyli hata km ni ujinga. Amepoteza kabisa ile critical thinking perspective. Kwa Magufuli ni sawa na Mungu kila akifanyacho ni sahihi kwa MM. This is very unfortunate.
I'd like to differ! , hajapoteza kabisa ile critical thinking perspectives kwa sababu haya anayoyandika pia ni very critical ila tatizo ni critical kwa the oppressed, hivyo kuonekana ame side na the oppressors! .

He was very independent and very critical to any form of oppression only when he side's with the oppressed but he is not critical thinker when he sides with the oppressors? !.
I say no! . Once a critical thinker, always a critical thinker kama ilivyo kwa once a Great Thinkers, always a Great Thinker !.

Pasco
 
Mzee Mwanakijiji, Usipende sana kitu wala kuchukia kitu sana kwani hali hiyo inaweza kukupelekea ushindwe kuwa " Free minded!".

Pia wakati mwingine ni bora ukatulia na kusikiliza wanachosema wengine kuliko kusema wewe, kwani unaposema kwa kawaida unakuwa unarudia jambo ambalo tayari unalijua ndani ya akili yako (liwe sahihi au la!) lakini unapotulia na kusikiliza au kusoma wengine, unakuwa umejitwalia fursa ya kujifunza na kujipa nafasi ya kupata taarifa mpya.
Asante sana mkuu...
Huu mchango wako umenifundisha jambo la msingi sana kwenye MAISHA..!
 
Back
Top Bottom