Mwanafunzi chuo cha uhasibu Arusha auwawa

Mwanafunzi chuo cha uhasibu Arusha auwawa

gagonza

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2009
Posts
309
Reaction score
98
Mwanafunzi wa chuo cha uhasibu Arusha jina halikuwezakupatikana mara moja,mwanafunzi huyo alikuwa anatoka chuoni usiku anaelekea nyumbani kwake alikutana na vibaka maeneo ya SDA katika msuguano waka mchoma visu vya shingo.
 
Jamani hawa vibaka hawa...rip mwanafunzi
 
kwani amekufa........?

kwan kichwa cha habar ya hii thread kinasemaje?nyinyi ndio mnaanza kufanya mtihan bila kusoma instructions au kwa sababu ameandika auwawa
 
Wanafunzi wanajiandaa kuandamana kwakudai ulinzi chuoni hapo kwakua matukio ya wizi wa Laptop simu za mikononi umeshamiri sana chuoni hapo wakati wanafunzi wakiwa wamekwenda kujisomea! Na hapa nilipo naona maaskari wanajiandaa kushuka kwenda Njiro chuoni hapo kwaajili ya hilo tukio! More updates coming.
 
Wanafunzi wanajiandaa kuandamana kwakudai ulinzi chuoni hapo kwakua matukio ya wizi wa Laptop simu za mikononi umeshamiri sana chuoni hapo wakati wanafunzi wakiwa wamekwenda kujisomea! Na hapa nilipo naona maaskari wanajiandaa kushuka kwenda Njiro chuoni hapo kwaajili ya hilo tukio! More updates coming.

Kwa ajili ya kuzuia maandamano au kutafuta vibaka?
 
Rpc ametoka kuzomewa na wanafunzi hapa.Huyo mwanafunzi aliefariki alikuwa anaitwa Henry.
Kamanda Lema nae amewasili katika chuo hiki.
 
So sad ukianzia familia mpaka taifa kwa ujumla...... Haya matukio kwa wanafunzi kwa kweli yamezidi maana kila chuo ni tatizo kama hili but still serikali yetu imevaa miwani ya mbao haioni wala haisikii
 
Lema anamsubiri Mkuu wa Chuo na anasema asipotokeza anawamrisha wanafunzi wakamchukue aliko!!!
 
matukio ya ubakaji wanafunzi wa kike chuoni hapo yapo pia. wanaingiliwa vyumbani na kubakwa.

inahitajika hatua kwa kweli.
 
Back
Top Bottom