Son of Gamba
JF-Expert Member
- Oct 26, 2012
- 4,718
- 6,979
Iko hivi ukifa unakuwa umekufa kabisa. Yaani unakuwa haupo kabisa na kinachobakia ni mwili tu ambao nao unaanza kuoza. Roho ya Mwanadamu haina uwezo wa kuona, kusikia, kunusa, kuhisi, kufikiri, kuongea wala kufanya chochote kile. Roho ya Mwanadamu ni pumzi tu unayoivuta ukiwa hai. Kumbuka baada ya MUNGU kumuumba Mwanadamu wa kwanza, alimpulizia puani pumzi ya uhai ndipo Mwanadamu akawa kiumbe hai. Ili Mwanadamu awe kiumbe hai ni lazima mwili wake uungane na pumzi ya MUNGU. Unapokufa ile pumzi inamrudia MUNGU na kuifadhiwa, iwe ulitenda mema au mabaya haijalishi, pumzi zote zinahifadhiwa kwa MUNGU. Kumbuka nimekuambia kuwa pumzi haina ufahamu wowote ule.Kumekua na imani na theories mbali mbali kuelezea maisha ya mwanadamu baada ya kifo. Kila mtu anaamini ktk chake kutokana na alivyoaminishwa.
Huko kwetu uchagani, ipo imani kuwa mtu akifa, hurudi kwa wajomba, hivyo wanafanya mila ya kwenda kumchukua kwa wajomba na kumrudisha kwa baba yake na anakua ancestor ambaye wanakua wakimwomba awasaidie kutatua matatizo pale wanapokumbwa na magumu.
Imani nyingi za kidini zinaeleza kuwa mtu akifa, kama alitenda mema, basi huenda mbinguni kwa Mungu kuishi kwa furaha na kama ulikua mwovu enzi za uhai wako, basi unadimbukizwa jehanamu kwenye everlasting fire..
Wapo wanaoamini kuwa mtu akifa ndo mwisho wake na hakuna maisha mengine baada ya hapo.
Binafsi mimi imani yangu ni ile ya kidini (Ukristo) kwamba mtu ataenda mbinguni baada ya kifo endapo alitenda mema,, na ataenda motoni endapo alitenda maovu..
Vipi wewe kwa upande wako unaamini vipi kuhusu hili?
Sasa kitakachofanyika siku ya mwisho, kwa uwezo alionao MUNGU atapuliza tarumbeta kubwa sana inajulikana kama "PARAPANDA", kwa kuipuliza parapanda hiyo, pumzi zile zilizohifadhiwa zitatoka kwenye parapanda hiyo na kurudi kwenye mifupa yote iliyolala popote pale na kuwafanya wote waliokufa kuwa hai tena. Unaweza ukasema sasa itakuwaje kwa wale waliokufa kwa kuteketea kwenye moto na mifupa yao kuungua kabisa? Jibu ni rahisi sana, MUNGU anauwezo wa kuwarudishia kila kitu, kuanzia mifupa yao na hata mavazi waliyokuwa wamevaa siku ile walipokuwa wakichomwa moto. Kama aliweza kumfinyanga Mwanadamu kutoka kwenye udongo, atashindwaje kuwafanya waliokufa hata kama ni kwa kuteketea kwenye moto kuwa hai tena??
Baada ya wafu kufufuliwa ndipo sasa watu wote watahukumiwa kwa kadiri ya matendo yao. Biblia imeandika vizuri sana kuhusu hili. Isitoshe MUNGU ni mwenye haki sana, hawezi kuwatupa kwenye moto sasa hivi baadhi ya wafu wanapokufa, kisha mwisho wa dunia awafufue na kuwatupa tena kwenye moto kwa mara ya pili? Kwa kuwa MUNGU ni mwenye haki, ndiyo maana ametenga siku moja tu ya hukumu kwa watu wote, wafu na walio hai (kumbuka pia imeandikwa siyo watu wote wataonja mauti, kuna watu hawatakufa kabisa).
Tena kuna watu waliokufa zamani walishafufuliwa tayari. Watu hao ni Ibrahimu, Isaka, na Yakobo. Na wengine ni Musa, Eliya na wengine wengi tu bila kumsahau MESSIAH (YESU KRISTO). Ukitaka kujua kuna watu wamefufuliwa tayari, soma Biblia yako; MATHAYO 27:51-53. Pia ukisoma Biblia yako utaona Yohana anaelezea katika kitabu cha UFUNUO kuwa aliwaona Wazee 24 wakiwa Mbinguni pamoja na MUNGU. UFUNUO 4:4, 5:5. Hivyo basi ili uweze kufika kwa MUNGU ni lazima ufufuliwe kwanza, sababu pia imeandikwa MUNGU siyo MUNGU wa wafu, bali ni MUNGU wa walio hai.
Kuna wengine watasema hapa inakuwaje basi wakati mwingine tunatokewa na ndugu zetu waliokufa? Yule anayekutokea baada ya ndugu yako kufa siyo yeye aliyekufa, bali ni shetani, anajibadilisha na kuwa na sura kama ya ndugu yako na kukutokea ili kukudanganya na kukupoteza ili uamini kuwa watu wakifa wanaendelea kuishi.
Kumbuka shetani alimdanganya HAWA pale Bustanini kwa kumwambia kuwa; akila matunda ya Mti ule hatakufa kabisa, bali atakuwa kama MUNGU akijua mema na mabaya. Sasa ili shetani aendelee kuutetea huu uwongo wake ndiyo maana mtu akifa, shetani hujibadilisha na kujifanya yeye ni yule mtu na kuwatokea ndugu na hata wakati mwingine kuongea nao na kuwaambai ili wafanikiwe kwenye maisha, wafanye mambo fulani fulani, kama kuchinja Mbuzi juu kaburi au kutoa sadaka fulani. Kwa kufanya hivi shetani anakuwa anawadanganya watu hao na wanaanza kuwaabudu wafu badala ya kumwabudu MUNGU. Tena siyo wanawaabudu wafu, hapana bali wanamwabudu shetani mwenyewe bila ya wao kujua.
Biblia imonya kuwa shetani ni mjanja sana na mweruvu. Tunapaswa kumwomba MUNGU sana ili tuing'amue mitego na uwongo wa huyu Ibilisi. Mbaya zaidi uwongo wake huu, ameueneza mpaka kwenye Makanisa. Makanisa mengi sana yanaamini eti mtu akifa anaendelea kuishi wakati siyo kweli. MUNGU alisema hivi; "U mavumbi wewe, na mavumbini utarudi".